Leveling na kuanza ujenzi

Leveling na kuanza ujenzi

Mkuu kama ni nyumba kubwa kwa aina ya viwanja hivyo basi amini kwamba utazika nyumba nyingine kwenye msingi tu.

Hapo mbinu nzuri ilikuwa ni kuitafuta level kwa kunyanyua msingi mrefu (kutoka kwenye ardhi halisia uliyoikuta) upande wenye slope mpaka ulingane na ule upande ulioko kwenye muinuko, baada ya hapo yale mashimo marefu yatakayopatikana kwenye partition za msingi ndo ujaze vifusi utakavyo mpaka palingane.


Lakini pia kifusi utakachojaza kwenye hizo partition za msingi kakikisha zinashindiliwa vizuri kabida either kwa kuziacha muda fulani au kama upo vizuri mfukoni na una haraka za kuanza ujemzi, jaza maji mengi kabisa kwenye hizo partition ili udogo utitie vizuri na ujishindilie kisha leta comprassor shindilia tena.

Kama msingi ni wa tofali (nashauri ziwe nchi sita), kabla haujaanza kunyanyua boma basi funga beam na umwage zege, weka PVC halafu anza kupandisha boma sasa.


Kujenge kwenye viwanja vyenye miteremko ni gharama sana ikiwa utataka kujenga nyumba yenye standard, kwakua gharama za kuset msingi tu zinaweza kulingana au kuzudi kabisa gharama za kunyanyua boma kwenye kiwanja ambacho ni tambarare.

NB: Msingi wako upigwe maji ya kutosha na ratio ya cement isiwe ya kinyemela (ndoo 12 ndogo za mchanga kwa mfuko mmoja wa cement)
Naona nimeshakosea. Napaswa kupasahau kidogo ili nifanye Mambo mengine. Au kuamua alternative nyingine ya kupauza kabisa nikatafute kwingine
 
Mkuu kwa swala la muda sio kipaumbele sana...BUT hapo lazima uache for at least miaka 3+ ili ardhi ikae sawa kidogo,,,na hapa ni kwa ujenzi wa nyumba ndogo tu ya kuishi...

Kama uko speed Hakikisha msingi wako unaanzia kwenye Ardhi asilia....

Ukifanikisha hilo anza kujenga...Otherwise usipofika chini msingi utaelea..

Nitakuja na picha
Naona nishachemsha. Inabid nijipe muda wa kutafakar nione Cha kufanya Kama Ni kuuza au kuvumilia huku nikifanya shughul nyingine
 
Ulifanya kuosa, ungetafuta wataalamu wa ujenzi wangekusaidia sana. Pia punguza gharama kwa kujenga kutokana na eneo lilivo. Unaweka steps tu
Sikufikiria vizur ndugu yangu. Nishakosea
 
Daah. Umekosa sana mkuu. Hizo gharama za levelling bora ungeingia gharama kunyanyua msingi tu. Nimefanya kama ulivyofanya wewe ila ni baada ya kujenga nyumba ndogo na kuacha matolea. Kwa Sasa imepita miaka mitatu ila bado Sina Imani ya kuvuta hii nyumba. Nawaza kupiga underground tu

Ukiangalia huku nyuma niliacha matoleo lengo ni kuja kuweka sebule, dining, Jiko na vyoo ila bado Sina Imani maana hii ya juu tu tayari Ina ufaView attachment 2123224
 
Naona nishachemsha. Inabid nijipe muda wa kutafakar nione Cha kufanya Kama Ni kuuza au kuvumilia huku nikifanya shughul nyingine

Hujachemsha mkuu,, Leveling uliyofanya si umejaza upande mmoja ambao kama ungejenga kawaida huo upande msingi ungekuwa mrefu kidogo....

Kama nature ya eneo ilikuwa na mwinuko sana huna namna,,, hapo lazima msingi uwe kama nyumba nyingine (idadi ya tofali za msingi inaweza kuwa sawa na tofali za kupandisha)....

Jipe muda na fanya maamuzi sahihi,,, Kosa la kwanza sio kosa,, ila kurudia kosa ni kuonyesha kwamba hutaki kujifunza, na Dunia itakufunza zaidi kwa Vitendo..

Kila la heri liwe upande wako ufanikishe Ujenzi.
 
Daah. Umekosa sana mkuu. Hizo gharama za levelling bora ungeingia gharama kunyanyua msingi tu. Nimefanya kama ulivyofanya wewe ila ni baada ya kujenga nyumba ndogo na kuacha matolea. Kwa Sasa imepita miaka mitatu ila bado Sina Imani ya kuvuta hii nyumba. Nawaza kupiga underground tu

Ukiangalia huku nyuma niliacha matoleo lengo ni kuja kuweka sebule, dining, Jiko na vyoo ila bado Sina Imani maana hii ya juu tu tayari Ina ufaView attachment 2123224
Picha haifunguki. Ila Asante kwa maelezo
 
Hujachemsha mkuu,, Leveling uliyofanya si umejaza upande mmoja ambao kama ungejenga kawaida huo upande msingi ungekuwa mrefu kidogo....

Kama nature ya eneo ilikuwa na mwinuko sana huna namna,,, hapo lazima msingi uwe kama nyumba nyingine (idadi ya tofali za msingi inaweza kuwa sawa na tofali za kupandisha)....

Jipe muda na fanya maamuzi sahihi,,, Kosa la kwanza sio kosa,, ila kurudia kosa ni kuonyesha kwamba hutaki kujifunza, na Dunia itakufunza zaidi kwa Vitendo..

Kila la heri liwe upande wako ufanikishe Ujenzi.
Amina Asante. Nimepata wazo la kumtafuta mtaalam Kwanza nimpeleke akanishaur. Nikiona Mambo yatakuwa mengi Sana nitauza nikanunue kwingine kusiko na changamoto hiyo
 
Nilipewa kiwanja na bi. Mkubwa ambao una mtelemko, ujenzi wa msingi peke yake ambao upande wa mtelemko lazima ujenge underground uligharimu Tsh. Milioni saba na something. Nyumba ni ya vyumba viwili, sebule, jiko na vyoo viwili master na kawaida. Ukichanganya na kile chumba cha underground unapata vyumba vitatu maana ni chumba kilichokamilika kabisa mtu anaweza kuishi. Hizi gharama nilizotumia za msingi ingekuwa kiwanja cha tambalale ningenyanyua pagale kabisa. Kujenga kwenye viwanja vya mtelemko ni gharama sana.
 
jaymaudaku_164527919395523.jpg
 
Habar zenu. Nimefanya leveling mwez January mwaka huu kwenye kiwanja kilichokuwa na mteremko. Kama haitoshi nimemwaga vifusi kadhaa vya udongo ili kusawazisha kiwanja kile kwan hata baada ya kulevo Bado mteremko uliendelea kuwepo .
Kwa wazoefu na wajuzi Ni muda gani mzuri naweza kuanza ujenzi na kusiwe na athar za kutitia kwa jengo?
Kuliko kumwaga kifusi, bora ungechimba usawazishe tu
 
Back
Top Bottom