LHRC: Chalamila achuliwe hatua za kinidhamu kwa kauli ya kutweza utu wa Mwanamke

LHRC: Chalamila achuliwe hatua za kinidhamu kwa kauli ya kutweza utu wa Mwanamke

Mashamba Makubwa Nalima

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2024
Posts
4,978
Reaction score
2,411
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimetoa wito kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kumchukulia hatua za kinidhamu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila kutokana na kauli yake anayodaiwa kuitoa hivi karibuni ambayo wamedai kuwa inatweza utu wa Mwanamke.

Aidha kufuatia kauli hiyo, LHRC kupitia Mkurugenzi Mtendaji, Dr. Anna Henga wametoa wito kwa Sekretariati ya Maadili ya Viongozi wa Umma kumuita na kumuhoji Chalamila kufuatia kauli yake.

Itakumbukwa hivi karibuni Chalamila alinukuliwa kupitia picha mjongeo akitoa kauli ambayo iliibua gumzo mtandaoni kuhusu Mwanamke ambaye alimpigia akiwa hospitalini kuhoji gharama za kujifungua alizotakiwa kulipia.

Soma: RC Chalamila asema mjamzito anayegoma kununua gloves akajifungulie nyumbani. Hafai kuendelea kubaki madarakani
 
Nilidhani LHCR wataanzisha uchunguzi WA kwanini hospitali hazina vifaa!

Pumbavu zenu, ulizeni serikali fungu la pesa za basket fund kwanini zimepungua kwa zaidi ya asilimia 60 tangu awamu hii imeingia madarakani? Ulizeni pesa za uchangiaji wa matibabu kwenye vituo vya serikali mbona zina mlolongo mrefu wakati vituo vikiomba kuzitumia kunulia vifaa tiba vya dharula....
 
Baada ya Chalamila kujikanyaga na kusema kuwa Wajawazito wanaogoma kununua gloves wakajifungulie nyumbani watu wamechachamaa
---------------------------------------------------------------

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimekemea vikali kauli ilizozitaja kuwa za
udhalilishaji na zinazotweza utu wa mwanamke zinazodaiwa kutolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, wakati wa hafla ya hadhara iliyofanyika wilayani Temeke, Dar es Salaam.

LHRC imetoa wito kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya Albert Chalamila kwa kauli zake zilizotajwa kuwa za udhalilishaji. Pia, LHRC imeitaka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kumhoji Chalamila iwapo hatua za kinidhamu hazitachukuliwa.

Zaidi
 
Mkuu huwezi kuwa kiongozi ukawa unatoa majibu ya ovyo hivyo. Wengine watajifunza kwake
Kauli zake nyingi anazotoa ni kama he is doing us a favor au kalazimishwa aongoze
Kazidisha sifa hadi ana haribu sasa
Sahihi
 
Mkuu huwezi kuwa kiongozi ukawa unatoa majibu ya ovyo hivyo. Wengine watajifunza kwake
Kauli zake nyingi anazotoa ni kama he is doing us a favor au kalazimishwa aongoze
Kazidisha sifa hadi ana haribu sasa
Sawa ata acha ukuu wa mkoa atamia kwenye ubunge mwisho wa siku anakuwa waziri unafiriki ilo ndio suluiisho?
 
Mkuu huwezi kuwa kiongozi ukawa unatoa majibu ya ovyo hivyo. Wengine watajifunza kwake
Kauli zake nyingi anazotoa ni kama he is doing us a favor au kalazimishwa aongoze
Kazidisha sifa hadi ana haribu sasa
Mbona kasema ukweli shida yenu mmejaaa unafiki
 
Mama sauti yako too soft and romantic hii kenge haitasikia mpe hii presentation mpatie heche akiwashe
 
Huyo jamaa hajawahi kuwa na matumizi mazuri ya mdomo. Historia inamhukumu.
 
Chura hana muda n watanganyika tujipange sana.
KAZI ni kipimo cha UTU
 

Attachments

  • VID-20250128-WA0033.mp4
    3.9 MB
Sawa ata acha ukuu wa mkoa atamia kwenye ubunge mwisho wa siku anakuwa waziri unafiriki ilo ndio suluiisho?
Mkuu alitakiwa ashtakiwe kwa uchochezi. Mbona viongozi wa upinzani wanashtakiwa kwa kutoa kauli za uchochezi na ukizisikia hazina utofauti na za huyu Mkuu wa mkoa wa Dar.
 
Back
Top Bottom