LHRC - Ripoti ya Utekelezaji Mwaka 2023 : Kati ya masuala ambayo tuliyafuatilia ni asilimia 12 yaliyofanikiwa kutatuliwa

LHRC - Ripoti ya Utekelezaji Mwaka 2023 : Kati ya masuala ambayo tuliyafuatilia ni asilimia 12 yaliyofanikiwa kutatuliwa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Snapinsta.app_448363131_18327325285133657_363035294597025116_n_1080.jpg
Ripoti Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) ya Utekelezaji kwa Mwaka 2023, inayoonesha mafanikio ya Mpango Mkakati wa Miaka Sita (2019-2024), imeeleza kupitia Mfumo wa Haki Kiganjani, LHRC ilifanyia kazi asilimia 50 ya matukio ya ukiukwaji wa Haki za Binadamu ulioripotiwa kati ya jumla ya matukio 1,919.

Akizungumzia ripoti hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Wakili Anna Henga, Juni 13, 2024 alisema uchambuzi ulionesha katika takwimu hizo Wanawake walikuwa manusura wakuu kwa asilimia 56, ikilinganishwa na Wanaume walio na asilimia 44.

Mkurugenzi huyo amesema licha ya mafanikio hayo katika kuripoti matukio kupitia mfumo huo wa Kidigtali, anadai bado kuna vikwazo mbalimbali ambavyo vimekuwa vikiwaweka mbali Wanawake kwa muda mwingi katika matumizi ya vifaa vya Kidigtali, ikiwemo muda mwingi kuhusika katika shughuli za malezi Kifamilia.

Aidha, aliongeza kuwa katika masuala yaliyofuatiliwa na Kituo hicho asilimia 12 yametatuliwa katika ngazi mbalimbali.
Snapinsta.app_448252563_18327325276133657_4581202235073958556_n_1080.jpg
“Masuala mengi yaliyofuatiliwa na LHRC bado yanashughulikiwa katika vituo vya polisi, hasa yakihusisha masuala ya jinai ambayo hayako chini ya Mamlaka ya LHRC.

"Takriban asilimia 12 ya masuala yamefanikiwa kutatuliwa, yakihusisha ngazi za familia, polisi na mahakama. Karibu asilimia 29% ya kesi zilielekezwa kwa msaada wa kisheria, hususani kwa msaada wa kisheria kwa uwakilishi wa mahakamani au kuwawezesha kujitetea wenyewe, hasa katika masuala yanayohusiana na ardhi,” alisema Henga

Lakini pia Ripoti hiyo inaonesha kuwa katika kipindi cha utekelezaji, wameona ufanisi katika Uwajibikaji wa makampuni ambayo kituo hicho kilifanya nayo kazi, hasa Mgodi wa Dhahabu wa North Mara, kufuatia mapendekezo ya viwango vya Haki za Binadamu.

Henga amesema maendeleo hayo ni matokeo ya ushirikiano na mgodi kuhusu jinsi ya kufuata viwango vya haki za binadamu kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.
 
Back
Top Bottom