Licha ya tabia mbaya za bodaboda tusiache kuwatetea wanapoonewa

Licha ya tabia mbaya za bodaboda tusiache kuwatetea wanapoonewa

Hakuna anayejali

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2023
Posts
418
Reaction score
526
Mimi siwaiti madereva bali waendesha pikipiki za biashara wanapitia changamoto za uonevu toka kwa mabosi wao na jeshi la polisi.

Niliwahi kuelezwa kisa kimoja cha boda aliyekuwa anaendesha boda ya mkataba. Ishu ilikuwa hivi: huyu boda anaendesha boda ya tati kwa bosi mmoja, sasa akakodiwa mahala huko akashambuliwa na washambuliaji wakapora pikipiki.

Sasa kijana alipomjulisha bosi baada ya tukio, bosi akamtia ndani bila kijana kupata haki ya matibabu, na akazuia dhamana kwa hoja kuwa kijana atakuwa amepanga mpango wa kumuibia pikipiki. Polisi nao wakakubali kubaka haki ya dhamana ya mtuhumiwa.

Mama mwenye mtoto alijitahidi kudhamini akakataliwa na mwisho bosi akamtafuta mama wa kijana na kumwambia waende kwa mwanasheria wakaandikishane lini atalipa boda.

Hapa ndipo penye hoja: Kwanini kijana anyimwe haki ya tiba, kwanini anyimwe haki ya dhamana? Hao polisi na bosi wanaosema kijana hajapasuka ila kavimba tu, je, wao ni wataalam wa afya?

Je, ikiwa bosi ndiye alipanga njama ili kupora na hatimaye kumlimbikizia deni? Hayo ni mtazamo wangu, je ninyi mnaonaje?
 
Sikubaliani na alichokifanya bosi ila yote yanawezekana . Uaminifu ni changamoto sana kwa bodaboda wamekuwa na tabia za kutiliwa mashaka sana.

Nmewahi shuhudia janjajanja za bodaboda kufake kuibiwa pikipiki na alivyokamatwa akasema aliiuza ili alipe deni alilokuwa anadaiwa kwenye makamari.

Maboss nao kuna muda wana tabia za kishenzi, wakiona mkataba unaisha roho zinawauma sana na kuanza figisu za dhuluma.

Kuna wale maboss washenzi sana wa tabia, kwa sababu chombo ni chake akikutuma halipi na hataki ikatwe kwenye hesabu yake na akikomaliwa alipe anaomba funguo ya chombo, hii sio sawa kabisa.
Nawasilisha
 
Mimi siwaiti madereva bali waendesha pikipiki za biashara wanapitia changamoto za uonevu toka kwa mabosi wao na jeshi la polisi.Niliwahi kuelezwa kisa kimoja cha boda aliyekuwa anaendesha boda ya mkataba.Ishu ilikuwa hivi huyu boda anaendesha boda ya tati kwa bosi mmoja,sasa akakodiwa mahala huko akashambuliwa na washambuliaji wakapora pikipiki.Sasa kijana alipomjulisha bosi baada ya tukio bosi akamtia ndani bila kijana kupata haki ya matibabu,na akazuia dhamana kwa hoja kuwa kijana atakuwa amepanga mpango wa kumuibia pikipiki na polisi nao wakakubali kubaka haki ya dhamana ya mtuhumiwa.Mama mwenye mtoto alijitahidi kudhamini akakataliwa na mwisho bosi akamtafuta mama wa kijana nakumwambia waende kwa mwanasheria wakaandikishane lini atalipa boda.Hapa ndipo penye hoja kwanini kijana anyimwe haki ya tiba,kwanini anyimwe haki ya dhamana,hao polisi na bosi wanaosema kijana hajapasuka ila kavimba tu je wao ni watalam wa afya?Je ikiwa bosi ndiye alipanga njama ili kupora na hatimaye kumlimbikizia deni?Hayo ni mtazamo wangu je ninyi mnaonaje?
I can guarantee you 97.6% huyo kijana kafanya mpango wa kuipora hyo pikipiki!Niliwahi kuwa mahabusu na kuna kijana nilimkuta amepigwa na polisi kwenye chumba maalumu cha upelelezi na alivyorudishwa alikuwa half dead!!Polisi ilibidi wampeleke hospitali baadae akarudishwa rumande.

Ilibidi wengine wawe wanampaka dawa vidonda mwili mzima alikuwa amechanika karibu kila sehemu,you can literally see veins!!!

Siku kadhaa baadae alianza kupona na kila askari wakija kum'interrogate alikuwa anakataa kuhusika na wizi wa pikipiki.Baadae siku moja usiku alituambia tukiwa wanne kuwa alihusika na mtuhumiwa mmoja miongoni mwetu(wa kesi ya mauaji) alimpa mbinu na moyo kuwa akipelekwa mahakamani aseme nn na hatakuwa na kesi ya kufanya na alituambia pikipiki iko wapi!!!!!!

Imagine alipigwa half dead lakini wapi.

Siku kadhaa baadae alikuja mwingine na similar case!! The same. Huyu mama yake alikuja
akawa analia mbele ya maaskari kuwa mwanae si mwizi hajawah kuiba mama mpaka akawa anagalagala mbele ya polisi

Jamaa alipigwa sana jioni yake baadae chamber masela wakampa moyo kwamba atateseka only one month na akitoka pikipiki ni yake!
 
Sheria inaruhusu kumtuma dhamana na kumtuma mtuhumiwa haki ya matibabu?
 
Back
Top Bottom