Mama Sabrina
JF-Expert Member
- Jul 30, 2016
- 16,620
- 27,589
Mungu anatupenda hawezi kutuchoma motoNo kufa lazima wote tutakufa, hakuna probability of death, it's only certenity.
Kukesha ukiomba ni kuiandalia makao mema Roho yako baada ya kuacha mwili, Roho haifi, it's either unakwenda mbinguni peponi kwenye raha ya uzina wa milele, au motoni kwenye jehanum ya moto wa milele .
The choice is yours.
P
Haya ni makubwa zaidi, ni mambo ya reicarnetion.Life is like a video game and the soul is your player. Once it loses in a stage (death), it plays again. Remember that the game character (you) doesn’t realise that he was born and died before.
Sent using Jamii Forums mobile app
Utakuwa humsomi vizuri Huyu Bwana Njaa ngosha pasikali au pasiko....kwenye hizi issue yuko kitambo sana na ana nyuzi zenye nyama kwenye mambo ya spirituality...hebu msake upate darsa lililotukuka ( in ff voice)kaka na kukubali sana kwenye nyanja za siasa,uchumi na kazarika.hayo mambo mwachie mshana jr.sijamaliza kusoma uzi wako.maana naona kichwa cha habari kama
lowasa kumfuta magu ccm
Sent using Jamii Forums mobile app
Soul mate unamjua vizur ww ulishawahi ukaka ukawaza pesa mpaka ukalia huli usingizi hauji kisa pesa kama ishakutokea basi hiyo ndo soul mate yako
Sent using Jamii Forums mobile app
It's true, tena tunaokolewa kwa neema na sio kwa matendo, Mungu baada ya kutuumba, pia ametupa utashi wa kuamua kumfuata yeye tupate uzima wa milele au kumfuata shetani na kwenda kwenye moto wa milele. Motoni sio kwa Mungu ni kwa shetani, anayechomwa ni shetani na wote watakaomfuta, wataungana naye motoni.
Aisee!!.
Kwahiyo na jamaa akaona ma soul mate wake ni wa maana sana kuwafuata wakaendelee kupiga stori kuliko kubaki na watoto japo wakue ndio asepe
Ukiisha zikiliza sauti za ulimwengu wa Roho, you loose touch na ulimwengu wa mwili, ila huko huko walipo, watasimamia show, japo wamewaacha yatima, lakini watoto watatunzwa na watasoma, ila kiukweli kabisa sometimes God is not fair at all, maana mambo mengine ni mambo ya karma, watoto malaika wa Mungu, hawana kosa lolote lakini wanaadhibiwa.Pascal Mayalla, kwanini mwenzi mmoja akitangulia na kisha mwenzie kumfuata, Huko waliko wasiwaite watoto wao pia wawafuate na badala yake wanawaacha hapa duniani wakiteseka na kuhangaika bila msaada wowote?
ThanksMada fikirishi sana, kitabu hiki kinasaidia kutoa mwanga kidogo
Mind and soul is one and the same, mind is controlled by conscious while soul is controlled by the subconscious and its immortal
P
Millions of years tinamtumia kama mafutaVitu vya kufikirika, hakuna aliye na proof, kila mtu anaongea lake tu. Mtu akifa amekufa, anakua decomposed basi, millions of years baadaye tunamtumia kama mafuta.
Roho za waovu zitateswa kwa muda kisha zitaharibiwa, Uzima wa milele ni kwa wale walioishi kwa kufuata mapenzi ya Mungu tu!!Mkuu pascal umeandika kitu kizoto sana japo kimejaa mikanganyiko mingi sana.Unasema mtu akifa mwili hubaki duniani(physical world) na roho huenda kuishi katika spiritual world ambako huko haifi milele.
Unataka kusema wale wote waliokufa na watakaokufa badae wote wataishi huko vipi kuhusu hizo roho zinaweza kuishi bila miili.
iPhone 7plus
Okey mkuu, please ukiifungua tag meKokutona, it's long, nitaifungulia thread yake.
P
Not fare at all kwakwel.Sema ndio hivyo tena ushaseema Mungu kwahiyo inabid ukubal hata kama ina painUkiisha zikiliza sauti za ulimwengu wa Roho, you loose touch na ulimwengu wa mwili, ila huko huko walipo, watasimamia show, japo wamewaacha yatima, lakini watoto watatunzwa na watasoma, ila kiukweli kabisa sometimes God is not fair at all, maana mambo mengine ni mambo ya karma, watoto malaika wa Mungu, hawana kosa lolote lakini wanaadhibiwa.
"The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa Duniani!, Unahukumiwa kwa Matendo Yako! - JamiiForums
P
Wanabodi,
Kifo cha Ephraim Kibonde kimeibua simanzi kubwa kwa sababu katika uhai wake hakuwahi kuugua, amekufa ghafla, hivyo watu kubaki na maswali mengi.
Katika bandiko la Tribute to Kibonde, kuna mwana JF kaandika maneno haya kumhusu Kibonde.
Kufuatia kuyasoma hayo, nimeona nizungumze kitu kuhusu uhai, kifo na maisha baada ya kifo.
Uhai ni Nini na Kifo ni Nini?.
Mwili wa binadamu una sehemu mbili, sehemu ya kwanza ni huu mwili wa nyama, ambao umeumbwa kwa mavumbi, na siku ukifa, kinachokufa ni mwili huu wa nyama, unazikwa kaburini, humo ndani unaoza na kurudi kuwa mavumbi. Sehemu ya pili ya mwili ni uhai, uhai hii ni pumzi Mungu aliyoipulizia kwenye ule udongo hivyo mwili kupata uhai. Hii ni Roho ya Mungu, the spiritual body, the astra body, mwili unapokufa, roho haifi, bali huacha mwili na kurudi kwa Mungu. Hivyo kifo ni kitendo cha roho kuacha mwili.
Jee Baada ya Kifo, hiyo Roho inakwenda Kuishi Wapi?.
Kama ulivyo mwili una sehemu mbili ya mwili wa nyama na mwili wa roho, vivyo hivyo dunia ina sehemu mbili, Ulimwengu wa Kidunia, the physical world, na Ulimwengu wa Roho, the Spiritual World, mtu akifa, roho ikiacha mwili, mwili unabaki kwenye ulimwengu wa dunia, unazikwa unaoza na kugeuka kuwa mavumbi, Roho inakwenda kwenye ulimwengu wa Roho kuendeleo kuishi milele, being mbinguni, peponi, kuzimu, toharani, au jehanum kwenye moto wa milele, hii subject nyingine lakini roho hazifi kwa sababu roho ni Mungu.
Jee Roho za Waliokufa Zinaweza Kuwaita Walio Hai?.
Jibu ni yes, ndio maana kwa baadhi ya mila, wamama wajawazito hawaruhusiwi kwenda makaburini, ili waliolala wasije wakaviita vichanga, na matokeo yake vikaitika na kupata still born.
Kwenye mahusiano kuna kitu kinaitwa Soul Mates, na hii ndio subject matter ya uzi wangu huu.
Mahusiano ya Mapenzi, ya Aina Mbili Kuna Mapenzi ya Mwili, na Mapenzi ya Roho ambayo Ndio Mapenzi ya Kweli.
Kama ulivyo mwili una mwili wa nyama, na mwili wa roho, vivyo hivyo kwenye mapenzi, kuna mapenzi ya mwili, physical love, na mapenzi ya Roho, spiritual love, emotional love.
Mapenzi ya physical love, ni yale mapenzi ya mambo ya mwilini, yanajumuisha mapenzi ya kutamani mwili na kufanya lile tendo la sex, sometimes ni needs, tamaa, infatuation, kila kiumbe mwenye viungo timilifu vya uzazi, anaweza kufanya physical love na kuridhika na tendo na kutoshelezeka, mechanically, lakini hakuna emotional na spiritual love, na hiki ndicho mara nyingi hufanyika kwenye biashara ya mapenzi, wale wadada wanaojiuza, hufanya physical love tuu kwa uhitaji wa pesa, lakini hakuna true love, emotional love wala spiritual love.
Mapenzi ya Kweli ni zaidi ya Sex, ni True love, Emotional na Spiritual.
Ili kupata mpenzi wa kweli na kufanya mapenzi ya kweli, yule mpenzi unaekutana nae lazima awe ndie soul mate wako uliyepangiwa ile siku unazaliwa. Yaani mtu uliyeumbiwa wewe kuwa parner wako wa maisha ya kimwili na kiroho, hivyo mkifanya sex, sio tuu mnafanya tendo, bali mnaunganika na kuwa mwili mmoja in spiritual body, na kutengeneza a special bond, hivyo mahusiano ya hivi, mmoja akitangulia, yule aliyebaki duniani hawezi kuishi muda mrefu, atamfuata tuu mwenzake, na mapenzi yao yataendelea kwenye the spiritual world kutokana na ile bond ambayo haiwezi kukatika.
Je Utajuaje Mpenzi Uliyenae Kama Ndie Soul Mate Wako?.
Haya sasa ni mambo ya Roho, naomba nisiyazungumze hapa.
Roho za Wafu, Zinaweza Kuziita Roho za Walio Hai Au Walio Hai, Wakajipeleka Wenyewe Kifoni.
Watu walikufa ambao roho zao zinaishi kwenye ulimwengu wa Roho, wanaweza kuwaita watu wowote wenye strong bond nao, kutoka duniani na kuwafuata kifoni, wengi wa watu wanaitwa kwa namna hii, hufa ghafla. Wengi ni pale mmoja anapotangulia, mwingine hawezi ku recover hivyo ni ama ni yeye mwenyewe aliye hai anaona maisha bila ya mwenzake hayana maana, hivyo kutamani kumfuata, ama aliyekufa anamuita mwenza wake kifoni, hivyo mwenza kumfuata. Hii pia hutokea kwa identical twins kama wanaushi karibu, na twin mmoja akitangulia, kuna mila inafanywa ili kumkinga twin aliyebaki asimfuate.
Hivyo kama ni kweli Ephraim Kibonde alisema mke wake ni soul mate wake, usikute Ruge ndio alikuwa kila kitu kwa Ephraim Kibonde, hivyo baada ya kifo cha mke wake, Ephraim aliweza kuendelea kuishi kwa vile Ruge yupo, ilipotokea na Ruge amekufa, katika kuushughulikia msiba huo, roho ya Ruge na Roho ya Mke wa Kibonde, zikakutana na kumuita Ephraim kuwa sisi tuko huku, wewe huko unangoja nini?, hivyo Roho ya Ephraim, ikasikia sauti hizo, na yeye mwenyewe ku will, kuwa nitawafuata. Baada ya ku will kuwa uko tayari kuwafuata, powers of will hutafuta sababu yoyote ya kukuchomoa, kikawaida ikikosekana sababu yoyote, iwe ni ugonjwa wa ghafla, ajali, or majanga yoyote ya kuondoa roho, then mtu alikuwa ni mzima, analala usingizini, kesho yake haamki. Pamoja na uwepo wa hiyo bond, ili kumfuata aliyetangulia ni lazima will yako ikubali.
Hitimisho.
Kwa vile kwa sisi binadamu wote hapa duniani tuko safari tuu, kuelekea kwenye maisha ya milele, tusiwalilie waliotangulia na kuhuzunika saana kwa kuwakosa, tuhunike kibinaadamu, tulie kwa kiasi, maisha ni lazima yaendelee, bali tujiangalie sisi wenyewe, kwa nafsi zetu, jee tumejiandaa kuitika wito wakati siku yetu na saa yetu ikitakapofika?.
Kesheni mkiomba kwa maana hamjui siku wala saa.
RIP Ephraim Kibonde na Ruge Mutahaba na wengine wote waliotangulia, nyinyi mbele sisi tuko nyuma yenu, sote sisi ni wa Kwake na Kwake tutarejea.
Paskali
Mkuu nadhani haya uliyoandika ni masimulizi uliyoyapata kutoka kwenye mapokeo ya kabila lako (Culture beliefs)Wanabodi,
Kifo cha Ephraim Kibonde kimeibua simanzi kubwa kwa sababu katika uhai wake hakuwahi kuugua, amekufa ghafla, hivyo watu kubaki na maswali mengi.
Katika bandiko la Tribute to Kibonde, kuna mwana JF kaandika maneno haya kumhusu Kibonde.
Kufuatia kuyasoma hayo, nimeona nizungumze kitu kuhusu uhai, kifo na maisha baada ya kifo.
Uhai ni Nini na Kifo ni Nini?.
Mwili wa binadamu una sehemu mbili, sehemu ya kwanza ni huu mwili wa nyama, ambao umeumbwa kwa mavumbi, na siku ukifa, kinachokufa ni mwili huu wa nyama, unazikwa kaburini, humo ndani unaoza na kurudi kuwa mavumbi. Sehemu ya pili ya mwili ni uhai, uhai hii ni pumzi Mungu aliyoipulizia kwenye ule udongo hivyo mwili kupata uhai. Hii ni Roho ya Mungu, the spiritual body, the astra body, mwili unapokufa, roho haifi, bali huacha mwili na kurudi kwa Mungu. Hivyo kifo ni kitendo cha roho kuacha mwili.
Jee Baada ya Kifo, hiyo Roho inakwenda Kuishi Wapi?.
Kama ulivyo mwili una sehemu mbili ya mwili wa nyama na mwili wa roho, vivyo hivyo dunia ina sehemu mbili, Ulimwengu wa Kidunia, the physical world, na Ulimwengu wa Roho, the Spiritual World, mtu akifa, roho ikiacha mwili, mwili unabaki kwenye ulimwengu wa dunia, unazikwa unaoza na kugeuka kuwa mavumbi, Roho inakwenda kwenye ulimwengu wa Roho kuendeleo kuishi milele, being mbinguni, peponi, kuzimu, toharani, au jehanum kwenye moto wa milele, hii subject nyingine lakini roho hazifi kwa sababu roho ni Mungu.
Jee Roho za Waliokufa Zinaweza Kuwaita Walio Hai?.
Jibu ni yes, ndio maana kwa baadhi ya mila, wamama wajawazito hawaruhusiwi kwenda makaburini, ili waliolala wasije wakaviita vichanga, na matokeo yake vikaitika na kupata still born.
Kwenye mahusiano kuna kitu kinaitwa Soul Mates, na hii ndio subject matter ya uzi wangu huu.
Mahusiano ya Mapenzi, ya Aina Mbili Kuna Mapenzi ya Mwili, na Mapenzi ya Roho ambayo Ndio Mapenzi ya Kweli.
Kama ulivyo mwili una mwili wa nyama, na mwili wa roho, vivyo hivyo kwenye mapenzi, kuna mapenzi ya mwili, physical love, na mapenzi ya Roho, spiritual love, emotional love.
Mapenzi ya physical love, ni yale mapenzi ya mambo ya mwilini, yanajumuisha mapenzi ya kutamani mwili na kufanya lile tendo la sex, sometimes ni needs, tamaa, infatuation, kila kiumbe mwenye viungo timilifu vya uzazi, anaweza kufanya physical love na kuridhika na tendo na kutoshelezeka, mechanically, lakini hakuna emotional na spiritual love, na hiki ndicho mara nyingi hufanyika kwenye biashara ya mapenzi, wale wadada wanaojiuza, hufanya physical love tuu kwa uhitaji wa pesa, lakini hakuna true love, emotional love wala spiritual love.
Mapenzi ya Kweli ni zaidi ya Sex, ni True love, Emotional na Spiritual.
Ili kupata mpenzi wa kweli na kufanya mapenzi ya kweli, yule mpenzi unaekutana nae lazima awe ndie soul mate wako uliyepangiwa ile siku unazaliwa. Yaani mtu uliyeumbiwa wewe kuwa parner wako wa maisha ya kimwili na kiroho, hivyo mkifanya sex, sio tuu mnafanya tendo, bali mnaunganika na kuwa mwili mmoja in spiritual body, na kutengeneza a special bond, hivyo mahusiano ya hivi, mmoja akitangulia, yule aliyebaki duniani hawezi kuishi muda mrefu, atamfuata tuu mwenzake, na mapenzi yao yataendelea kwenye the spiritual world kutokana na ile bond ambayo haiwezi kukatika.
Je Utajuaje Mpenzi Uliyenae Kama Ndie Soul Mate Wako?.
Haya sasa ni mambo ya Roho, naomba nisiyazungumze hapa.
Roho za Wafu, Zinaweza Kuziita Roho za Walio Hai Au Walio Hai, Wakajipeleka Wenyewe Kifoni.
Watu walikufa ambao roho zao zinaishi kwenye ulimwengu wa Roho, wanaweza kuwaita watu wowote wenye strong bond nao, kutoka duniani na kuwafuata kifoni, wengi wa watu wanaitwa kwa namna hii, hufa ghafla. Wengi ni pale mmoja anapotangulia, mwingine hawezi ku recover hivyo ni ama ni yeye mwenyewe aliye hai anaona maisha bila ya mwenzake hayana maana, hivyo kutamani kumfuata, ama aliyekufa anamuita mwenza wake kifoni, hivyo mwenza kumfuata. Hii pia hutokea kwa identical twins kama wanaushi karibu, na twin mmoja akitangulia, kuna mila inafanywa ili kumkinga twin aliyebaki asimfuate.
Hivyo kama ni kweli Ephraim Kibonde alisema mke wake ni soul mate wake, usikute Ruge ndio alikuwa kila kitu kwa Ephraim Kibonde, hivyo baada ya kifo cha mke wake, Ephraim aliweza kuendelea kuishi kwa vile Ruge yupo, ilipotokea na Ruge amekufa, katika kuushughulikia msiba huo, roho ya Ruge na Roho ya Mke wa Kibonde, zikakutana na kumuita Ephraim kuwa sisi tuko huku, wewe huko unangoja nini?, hivyo Roho ya Ephraim, ikasikia sauti hizo, na yeye mwenyewe ku will, kuwa nitawafuata. Baada ya ku will kuwa uko tayari kuwafuata, powers of will hutafuta sababu yoyote ya kukuchomoa, kikawaida ikikosekana sababu yoyote, iwe ni ugonjwa wa ghafla, ajali, or majanga yoyote ya kuondoa roho, then mtu alikuwa ni mzima, analala usingizini, kesho yake haamki. Pamoja na uwepo wa hiyo bond, ili kumfuata aliyetangulia ni lazima will yako ikubali.
Hitimisho.
Kwa vile kwa sisi binadamu wote hapa duniani tuko safari tuu, kuelekea kwenye maisha ya milele, tusiwalilie waliotangulia na kuhuzunika saana kwa kuwakosa, tuhunike kibinaadamu, tulie kwa kiasi, maisha ni lazima yaendelee, bali tujiangalie sisi wenyewe, kwa nafsi zetu, jee tumejiandaa kuitika wito wakati siku yetu na saa yetu ikitakapofika?.
Kesheni mkiomba kwa maana hamjui siku wala saa.
RIP Ephraim Kibonde na Ruge Mutahaba na wengine wote waliotangulia, nyinyi mbele sisi tuko nyuma yenu, sote sisi ni wa Kwake na Kwake tutarejea.
Paskali
Twende mdogo mdogo, maadam unajua kuwa tulipuliziwa pumzi ya Mungu tukapata uhai, hiyo pumzi ya uhai ndio Roho, hivyo kifo ni kukata Roho, pale Roho hivyo inapoacha mwili, unakuwa ni mwisho wa uhai kwa mwili tuu, Roho ambayo ni spirit, haina mwisho, it's eternal.Mkuu
Kwa mujibu wa biblia ,nafsi hai ni muunganiko wa udongo na pumzi ya Mungu. Tunapoongelea uhai(nafsi hai) ni kuwa mwili Hivyo huwa hakuna uhai ikitokea hivi vitu viwili vikitengana.
Roho inayomrudia Mungu wakati wa kufa ni ile pumzi ya uhai. Hakuna mahali katika Biblia ambapo roho inaelezwa kuwa ina uhai, hekima au hisia baada ya mtu kufa. Ni “pumzi ya uhai”, si Zaidi.
Kuna vitu vimeandikwa kwenye Bible kwa mafumbo na kuleta to coherence ili kupunguza contradictions.Mkuu
Uongo wa kwanza kabisa wa Ibilisi ni upi?
“Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa.” Mwa. 3:4. “Yule joka… yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote.” Ufu. 12:9.
Kwa hiyo mkuu Pascal Ukiamini kuwa kuna some sort of life inaendelea somewhere, maana yake unaungana na shetani aliyemwambia Hawa kuwa hata akila lile tunda hatakufa.
Mkuu kuzaa na kuongezeka kuliagizwa kabla ya kula tunda. Soma upya biblia yako.Kuna vitu vimeandikwa kwenye Bible kwa mafumbo na kuleta to coherence ili kupunguza contradictions.
Mungu alimuumba Adam na Eva, lile tunda la mti wa katikati, wa mema na mabaya sio tunda tunda bali ni lile 'tunda', na ule mti wa katikati sio mti mti bali ni 'mti'.
Adam na Eva wakaambiwa fanyeni yote, kuleni vyote, lakini wewe Adam usitumie mti kumega lile 'tunda' la Eva, na wewe Eva, usitoe 'tunda' limegwe na Adam.
Shetani alijigeuza nyoka ili kupenya tuu bustanini, na alipofanikiwa, alijigeuza mtu kijana handsome boy na kumtokea Eva ndipo kumdanya.
Katika kundanganya kule alimega lile tunda la Eva, ndipo Eva nae akamlazimisha Adam kumega na wakaishia usingizini, si unajua yale mambo ya kufika, ndipo walipoamshwa wakajiona wako uchi baada ya kujua kazi ya mti wa katikati na kumega lile'tunda'.
Tangu hapo sasa ndio wakaadhibiwa na kuruhusiwa kuzaa kuongezeka kuijaza nchi yote na hilo 'tendo' ndio dhambi ya asili.
Yaani ili binaadamu azaliwe ni lazima kwanza dhambi ya asili itendwe, tunda limegwe ndipo mimba itungwe.
Mtu pekee aliyezaliwa bila dhambi ya asili ni Bwana wetu Yesu Kristo, kwa Bikira Maria kukingiwa dhambi ya asili kwa kupata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, bila tunda tunda kumegwa na dhambi kutendwa.
Jee uliyajua hayo?. Vivyo hivyo kifo ni mwili tuu, Roho haifi na sio ushetani.
Yesu alisema ukifa siku moja ni kama miaka elfu moja na miaka elfu moja ni ni kama siku moja. Wanaokufa leo, jana, juzi, na watakaokufa kesho, wote wanalipwa the same, kwenye ulimwengu wa Roho, hakuna mass, distance and time.
P
Source yangu sio Bible tuu bali logic.Mkuu kuzaa na kuongezeka kuliagizwa kabla ya kula tunda. Soma upya biblia yako.