Life After Life: Je, Wafu huwaita watu kifoni? Kuna walio hai huamua kuwafuata Wafu? Wapenzi mmoja akitangulia, mwenzake anafuata!

Life After Life: Je, Wafu huwaita watu kifoni? Kuna walio hai huamua kuwafuata Wafu? Wapenzi mmoja akitangulia, mwenzake anafuata!

Source yangu sio Bible tuu bali logic.
Bible imehaririwa ili iendane.

Kama zaeni muongezeke ni kabla ya tunda, then dhambi ya asili ni nini?.
Bikira Maria kukingiwa dhambi ya asili na kupata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu kuna maana gani?.
P
Ambaye hana dhambi ya asili ni Yesu na siyo bikra Maria mkuu. Mbona unaniangusha
 
Shetani alijigeuza nyoka ili kupenya tuu bustanini, na alipofanikiwa, alijigeuza mtu kijana handsome boy na kumtokea Eva ndipo kumdanya.

Katika kundanganya kule alimega lile tunda la Eva, [emoji779] ndipo Eva nae akamlazimisha Adam kumega na wakaishia usingizini, si unajua yale mambo ya kufika, ndipo walipoamshwa wakajiona wako uchi baada ya kujua kazi ya mti wa katikati na kumega lile'tunda'.P
Mkuu ina maana Mama yetu kipenzi Hawa alichepuka...[emoji33]OMG



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ambaye hana dhambi ya asili ni Yesu na siyo bikra Maria mkuu. Mbona unaniangusha
Mkuu Mtukutu wa Nyaigela, umechanganya mambo ila sio wewe tuu, bali hata Wakatoliki wenyewe, kwenye Litani ya Bikira Maria kuna sifa nyingi za Bikira Maria zimewekwa lakini sio.

Dhambi ya asili ni kumegwa kwa lile tunda. Ili binaadamu azaliwe ni lazima lile tendo la kumegwa kwa tunda lifanyike.

Hakuna popote nimesema Bikira Maria hana dhambi ya asili, kwasababu naye amezaliwa na dhambi ya asili, kwa lile tendo la kumegwa kwa lile tunda ila Yesu ndiye pekee aliyezaliwa bila dhambi ya asili kwa sababu, kutungwa kwake ni kwa uwezo wa Roho Mtakatifu na sio kwa lile tendo la kumegwa kwa lile tunda. Bikira Maria ndiye binaadamu pekee, aliyekingiwa dhambi ya asili kwa kupata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu bila lile tendo la kumegwa kwa lile tunda.

Tena kwa vile mimi ni Mkatoliki, kuna maisha ya Bikira Maria baada ya kuzaliwa kwa Yesu, Wakatoliki hawayajui kwa sababu waandishi wa Bible waliamua wasiyaingize kwe Bible hivyo kwa Wakatoliki, Bikira Maria anahesabika alibaki bikira daima.

Ndani ya Bible, baada ya Yesu kuzaliwa na kukimbilia Misri, hakuna details za maisha yao huko Misri hadi alipotimu miaka 12 alipokuja hekaluni na kupotea tena hadi miaka 30 aliporejea. Details zipo ila hazikuwekwa, Baba mlezi wa Yesu Joseph alikuwa mwanamume kamili rijali, hivyo...
Tuachie hapo.
P
 
Mkuu mwanzo wa uzi wako umesema kwamba kitendo cha kufa ni roho kuacha mwili na ukasema kinachokufa ni mwili ambao baadae unaoza na kuwa mavumbi na roho huenda kuishi sehemu ulizozitaja ambazo sio ardhini.

Lakini wakati huohuo unasema tena kina mama wajawazito huwa wanazuiliwa kwenda kuzika kwa kuhofia vichanga vyao vinaweza kuitwa na wafu makaburini. Daaah mbona kama mambo mchanganyiko
 
Mkuu ina maana Mama yetu kipenzi Hawa alichepuka...[emoji33]OMG
Sent using Jamii Forums mobile app
Enzi hizo kulikuwa bado hakuna mambo ya michepuko. Alichofanya shetani ni kumrubuni Mama yetu Eva na kumuonyesha namna tunda linavyomegwa.
Unaweza kujiuliza, kama Mungu aliumba mwanamke mmoja tuu, hao Cain na Abeli, walizaa na nani ili kizazi kiongezeke?.
P
 
Mkuu mwanzo wa uzi wako umesema kwamba kitendo cha kufa ni roho kuacha mwili na ukasema kinachokufa ni mwili ambao baadae unaoza na kuwa mavumbi na roho huenda kuishi sehemu ulizozitaja ambazo sio ardhini.

Lakini wakati huohuo unasema tena kina mama wajawazito huwa wanazuiliwa kwenda kuzika kwa kuhofia vichanga vyao vinaweza kuitwa na wafu makaburini. Daaah mbona kama mambo mchanganyiko
Maisha ya hapa duniani ni mafupi sana tena yamejaa shida, ila tunachukua muda mrefu sana na kutumia kila linalowezekana kusoma elimu itakayotusaidia kuyamudu. Ila tunasahau sana kusoma elimu ambayo inaaminika itatuelekeza kwenye maisha ya MILELE ,yenye raha na kutokufa tena. Tumewaachia viongozi watufundishe. Saa nyingine wanatudanganya kwa kutufundisha vitu tofauti na biblia inavyosema,kwa masilahi yao.
 
Mkuu mwanzo wa uzi wako umesema kwamba kitendo cha kufa ni roho kuacha mwili na ukasema kinachokufa ni mwili ambao baadae unaoza na kuwa mavumbi na roho huenda kuishi sehemu ulizozitaja ambazo sio ardhini.

Lakini wakati huohuo unasema tena kina mama wajawazito huwa wanazuiliwa kwenda kuzika kwa kuhofia vichanga vyao vinaweza kuitwa na wafu makaburini. Daaah mbona kama mambo mchanganyiko
Mkuu Magallah, mwili ukiishafukiwa ardhini, unaoza na kugeuka kuwa mavumbi, kaburi ni ishara tuu, as just an rv ya kukutania, lakini roho zinakwenda kwenye ulimwengu wa roho, huko hakuna tena mass, distance wala time, kwa vile roho ni semu ya Mungu, then roho hizo ni omnipotent, omnipresent na omniscience.

Kitendo cha wamama wajawazito kwenda kaburini, vichanga vinamawasiliano na ulimwengu wa Roho, hivyo its just superstition tuu kuwa vikienda makaburini ndio vitaitwa, vinaweza kuitwa tuu vikiwa popote, ila kule kuona makundi ya watu wakilia, wakihuzunika, vinaweza kushawishika, kwa nini nije duniani kisha nije kuliza watu?, bora...
P.
 
Wanabodi,
Kifo cha Ephraim Kibonde kimeibua simanzi kubwa kwa sababu katika uhai wake hakuwahi kuugua, amekufa ghafla, hivyo watu kubaki na maswali mengi.
Katika bandiko la Tribute to Kibonde, kuna mwana JF kaandika maneno haya kumhusu Kibonde.


Kufuatia kuyasoma hayo, nimeona nizungumze kitu kuhusu uhai, kifo na maisha baada ya kifo.

Uhai ni Nini na Kifo ni Nini?.
Mwili wa binadamu una sehemu mbili, sehemu ya kwanza ni huu mwili wa nyama, ambao umeumbwa kwa mavumbi, na siku ukifa, kinachokufa ni mwili huu wa nyama, unazikwa kaburini, humo ndani unaoza na kurudi kuwa mavumbi. Sehemu ya pili ya mwili ni uhai, uhai hii ni pumzi Mungu aliyoipulizia kwenye ule udongo hivyo mwili kupata uhai. Hii ni Roho ya Mungu, the spiritual body, the astra body, mwili unapokufa, roho haifi, bali huacha mwili na kurudi kwa Mungu. Hivyo kifo ni kitendo cha roho kuacha mwili.

Jee Baada ya Kifo, hiyo Roho inakwenda Kuishi Wapi?.
Kama ulivyo mwili una sehemu mbili ya mwili wa nyama na mwili wa roho, vivyo hivyo dunia ina sehemu mbili, Ulimwengu wa Kidunia, the physical world, na Ulimwengu wa Roho, the Spiritual World, mtu akifa, roho ikiacha mwili, mwili unabaki kwenye ulimwengu wa dunia, unazikwa unaoza na kugeuka kuwa mavumbi, Roho inakwenda kwenye ulimwengu wa Roho kuendeleo kuishi milele, being mbinguni, peponi, kuzimu, toharani, au jehanum kwenye moto wa milele, hii subject nyingine lakini roho hazifi kwa sababu roho ni Mungu.

Jee Roho za Waliokufa Zinaweza Kuwaita Walio Hai?.
Jibu ni yes, ndio maana kwa baadhi ya mila, wamama wajawazito hawaruhusiwi kwenda makaburini, ili waliolala wasije wakaviita vichanga, na matokeo yake vikaitika na kupata still born.
Kwenye mahusiano kuna kitu kinaitwa Soul Mates, na hii ndio subject matter ya uzi wangu huu.

Mahusiano ya Mapenzi, ya Aina Mbili Kuna Mapenzi ya Mwili, na Mapenzi ya Roho ambayo Ndio Mapenzi ya Kweli.
Kama ulivyo mwili una mwili wa nyama, na mwili wa roho, vivyo hivyo kwenye mapenzi, kuna mapenzi ya mwili, physical love, na mapenzi ya Roho, spiritual love, emotional love.
Mapenzi ya physical love, ni yale mapenzi ya mambo ya mwilini, yanajumuisha mapenzi ya kutamani mwili na kufanya lile tendo la sex, sometimes ni needs, tamaa, infatuation, kila kiumbe mwenye viungo timilifu vya uzazi, anaweza kufanya physical love na kuridhika na tendo na kutoshelezeka, mechanically, lakini hakuna emotional na spiritual love, na hiki ndicho mara nyingi hufanyika kwenye biashara ya mapenzi, wale wadada wanaojiuza, hufanya physical love tuu kwa uhitaji wa pesa, lakini hakuna true love, emotional love wala spiritual love.

Mapenzi ya Kweli ni zaidi ya Sex, ni True love, Emotional na Spiritual.
Ili kupata mpenzi wa kweli na kufanya mapenzi ya kweli, yule mpenzi unaekutana nae lazima awe ndie soul mate wako uliyepangiwa ile siku unazaliwa. Yaani mtu uliyeumbiwa wewe kuwa parner wako wa maisha ya kimwili na kiroho, hivyo mkifanya sex, sio tuu mnafanya tendo, bali mnaunganika na kuwa mwili mmoja in spiritual body, na kutengeneza a special bond, hivyo mahusiano ya hivi, mmoja akitangulia, yule aliyebaki duniani hawezi kuishi muda mrefu, atamfuata tuu mwenzake, na mapenzi yao yataendelea kwenye the spiritual world kutokana na ile bond ambayo haiwezi kukatika.

Je Utajuaje Mpenzi Uliyenae Kama Ndie Soul Mate Wako?.
Haya sasa ni mambo ya Roho, naomba nisiyazungumze hapa.

Roho za Wafu, Zinaweza Kuziita Roho za Walio Hai Au Walio Hai, Wakajipeleka Wenyewe Kifoni.
Watu walikufa ambao roho zao zinaishi kwenye ulimwengu wa Roho, wanaweza kuwaita watu wowote wenye strong bond nao, kutoka duniani na kuwafuata kifoni, wengi wa watu wanaitwa kwa namna hii, hufa ghafla. Wengi ni pale mmoja anapotangulia, mwingine hawezi ku recover hivyo ni ama ni yeye mwenyewe aliye hai anaona maisha bila ya mwenzake hayana maana, hivyo kutamani kumfuata, ama aliyekufa anamuita mwenza wake kifoni, hivyo mwenza kumfuata. Hii pia hutokea kwa identical twins kama wanaushi karibu, na twin mmoja akitangulia, kuna mila inafanywa ili kumkinga twin aliyebaki asimfuate.

Hivyo kama ni kweli Ephraim Kibonde alisema mke wake ni soul mate wake, usikute Ruge ndio alikuwa kila kitu kwa Ephraim Kibonde, hivyo baada ya kifo cha mke wake, Ephraim aliweza kuendelea kuishi kwa vile Ruge yupo, ilipotokea na Ruge amekufa, katika kuushughulikia msiba huo, roho ya Ruge na Roho ya Mke wa Kibonde, zikakutana na kumuita Ephraim kuwa sisi tuko huku, wewe huko unangoja nini?, hivyo Roho ya Ephraim, ikasikia sauti hizo, na yeye mwenyewe ku will, kuwa nitawafuata. Baada ya ku will kuwa uko tayari kuwafuata, powers of will hutafuta sababu yoyote ya kukuchomoa, kikawaida ikikosekana sababu yoyote, iwe ni ugonjwa wa ghafla, ajali, or majanga yoyote ya kuondoa roho, then mtu alikuwa ni mzima, analala usingizini, kesho yake haamki. Pamoja na uwepo wa hiyo bond, ili kumfuata aliyetangulia ni lazima will yako ikubali.

Hitimisho.
Kwa vile kwa sisi binadamu wote hapa duniani tuko safari tuu, kuelekea kwenye maisha ya milele, tusiwalilie waliotangulia na kuhuzunika saana kwa kuwakosa, tuhunike kibinaadamu, tulie kwa kiasi, maisha ni lazima yaendelee, bali tujiangalie sisi wenyewe, kwa nafsi zetu, jee tumejiandaa kuitika wito wakati siku yetu na saa yetu ikitakapofika?.

Kesheni mkiomba kwa maana hamjui siku wala saa.
RIP Ephraim Kibonde na Ruge Mutahaba na wengine wote waliotangulia, nyinyi mbele sisi tuko nyuma yenu, sote sisi ni wa Kwake na Kwake tutarejea.

Paskali
Nakuelewaga saaana bro, asante kwa somo hili adimu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanabodi,
Kifo cha Ephraim Kibonde kimeibua simanzi kubwa kwa sababu katika uhai wake hakuwahi kuugua, amekufa ghafla, hivyo watu kubaki na maswali mengi.
Katika bandiko la Tribute to Kibonde, kuna mwana JF kaandika maneno haya kumhusu Kibonde.


Kufuatia kuyasoma hayo, nimeona nizungumze kitu kuhusu uhai, kifo na maisha baada ya kifo.

Uhai ni Nini na Kifo ni Nini?.
Mwili wa binadamu una sehemu mbili, sehemu ya kwanza ni huu mwili wa nyama, ambao umeumbwa kwa mavumbi, na siku ukifa, kinachokufa ni mwili huu wa nyama, unazikwa kaburini, humo ndani unaoza na kurudi kuwa mavumbi. Sehemu ya pili ya mwili ni uhai, uhai hii ni pumzi Mungu aliyoipulizia kwenye ule udongo hivyo mwili kupata uhai. Hii ni Roho ya Mungu, the spiritual body, the astra body, mwili unapokufa, roho haifi, bali huacha mwili na kurudi kwa Mungu. Hivyo kifo ni kitendo cha roho kuacha mwili.

Jee Baada ya Kifo, hiyo Roho inakwenda Kuishi Wapi?.
Kama ulivyo mwili una sehemu mbili ya mwili wa nyama na mwili wa roho, vivyo hivyo dunia ina sehemu mbili, Ulimwengu wa Kidunia, the physical world, na Ulimwengu wa Roho, the Spiritual World, mtu akifa, roho ikiacha mwili, mwili unabaki kwenye ulimwengu wa dunia, unazikwa unaoza na kugeuka kuwa mavumbi, Roho inakwenda kwenye ulimwengu wa Roho kuendeleo kuishi milele, being mbinguni, peponi, kuzimu, toharani, au jehanum kwenye moto wa milele, hii subject nyingine lakini roho hazifi kwa sababu roho ni Mungu.

Jee Roho za Waliokufa Zinaweza Kuwaita Walio Hai?.
Jibu ni yes, ndio maana kwa baadhi ya mila, wamama wajawazito hawaruhusiwi kwenda makaburini, ili waliolala wasije wakaviita vichanga, na matokeo yake vikaitika na kupata still born.
Kwenye mahusiano kuna kitu kinaitwa Soul Mates, na hii ndio subject matter ya uzi wangu huu.

Mahusiano ya Mapenzi, ya Aina Mbili Kuna Mapenzi ya Mwili, na Mapenzi ya Roho ambayo Ndio Mapenzi ya Kweli.
Kama ulivyo mwili una mwili wa nyama, na mwili wa roho, vivyo hivyo kwenye mapenzi, kuna mapenzi ya mwili, physical love, na mapenzi ya Roho, spiritual love, emotional love.
Mapenzi ya physical love, ni yale mapenzi ya mambo ya mwilini, yanajumuisha mapenzi ya kutamani mwili na kufanya lile tendo la sex, sometimes ni needs, tamaa, infatuation, kila kiumbe mwenye viungo timilifu vya uzazi, anaweza kufanya physical love na kuridhika na tendo na kutoshelezeka, mechanically, lakini hakuna emotional na spiritual love, na hiki ndicho mara nyingi hufanyika kwenye biashara ya mapenzi, wale wadada wanaojiuza, hufanya physical love tuu kwa uhitaji wa pesa, lakini hakuna true love, emotional love wala spiritual love.

Mapenzi ya Kweli ni zaidi ya Sex, ni True love, Emotional na Spiritual.
Ili kupata mpenzi wa kweli na kufanya mapenzi ya kweli, yule mpenzi unaekutana nae lazima awe ndie soul mate wako uliyepangiwa ile siku unazaliwa. Yaani mtu uliyeumbiwa wewe kuwa parner wako wa maisha ya kimwili na kiroho, hivyo mkifanya sex, sio tuu mnafanya tendo, bali mnaunganika na kuwa mwili mmoja in spiritual body, na kutengeneza a special bond, hivyo mahusiano ya hivi, mmoja akitangulia, yule aliyebaki duniani hawezi kuishi muda mrefu, atamfuata tuu mwenzake, na mapenzi yao yataendelea kwenye the spiritual world kutokana na ile bond ambayo haiwezi kukatika.

Je Utajuaje Mpenzi Uliyenae Kama Ndie Soul Mate Wako?.
Haya sasa ni mambo ya Roho, naomba nisiyazungumze hapa.

Roho za Wafu, Zinaweza Kuziita Roho za Walio Hai Au Walio Hai, Wakajipeleka Wenyewe Kifoni.
Watu walikufa ambao roho zao zinaishi kwenye ulimwengu wa Roho, wanaweza kuwaita watu wowote wenye strong bond nao, kutoka duniani na kuwafuata kifoni, wengi wa watu wanaitwa kwa namna hii, hufa ghafla. Wengi ni pale mmoja anapotangulia, mwingine hawezi ku recover hivyo ni ama ni yeye mwenyewe aliye hai anaona maisha bila ya mwenzake hayana maana, hivyo kutamani kumfuata, ama aliyekufa anamuita mwenza wake kifoni, hivyo mwenza kumfuata. Hii pia hutokea kwa identical twins kama wanaushi karibu, na twin mmoja akitangulia, kuna mila inafanywa ili kumkinga twin aliyebaki asimfuate.

Hivyo kama ni kweli Ephraim Kibonde alisema mke wake ni soul mate wake, usikute Ruge ndio alikuwa kila kitu kwa Ephraim Kibonde, hivyo baada ya kifo cha mke wake, Ephraim aliweza kuendelea kuishi kwa vile Ruge yupo, ilipotokea na Ruge amekufa, katika kuushughulikia msiba huo, roho ya Ruge na Roho ya Mke wa Kibonde, zikakutana na kumuita Ephraim kuwa sisi tuko huku, wewe huko unangoja nini?, hivyo Roho ya Ephraim, ikasikia sauti hizo, na yeye mwenyewe ku will, kuwa nitawafuata. Baada ya ku will kuwa uko tayari kuwafuata, powers of will hutafuta sababu yoyote ya kukuchomoa, kikawaida ikikosekana sababu yoyote, iwe ni ugonjwa wa ghafla, ajali, or majanga yoyote ya kuondoa roho, then mtu alikuwa ni mzima, analala usingizini, kesho yake haamki. Pamoja na uwepo wa hiyo bond, ili kumfuata aliyetangulia ni lazima will yako ikubali.

Hitimisho.
Kwa vile kwa sisi binadamu wote hapa duniani tuko safari tuu, kuelekea kwenye maisha ya milele, tusiwalilie waliotangulia na kuhuzunika saana kwa kuwakosa, tuhunike kibinaadamu, tulie kwa kiasi, maisha ni lazima yaendelee, bali tujiangalie sisi wenyewe, kwa nafsi zetu, jee tumejiandaa kuitika wito wakati siku yetu na saa yetu ikitakapofika?.

Kesheni mkiomba kwa maana hamjui siku wala saa.
RIP Ephraim Kibonde na Ruge Mutahaba na wengine wote waliotangulia, nyinyi mbele sisi tuko nyuma yenu, sote sisi ni wa Kwake na Kwake tutarejea.

Paskali
Ujanjaujanja tu wa kucheza na maneno na hisia za watu ila kiuhalisia hamna ukweli wowote juu ya insha hii bro.
 
Mungu ni Roho nao wamubuduo yawapasa kumwamubudu katika roho na kweli.

Well; wewe na wenzako hamuwezi kuamini haya especially kama mungu wenu mnaemuabudu ni yule anaemuombea mtume wake, mwenye uso, miguu na mikono yote ya kushoto.
Umeshasema hatuamini.... obvious ikishakuwa imani tayari hayo ni mashaka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hamna ukweli wowote juu ya bandiko hili,umetumia mfano mmoja tu ambayo hauna ushahidi wowote.
Umeujengea hoja mfano wako kwa hisia ya tukio husika kwa kuutafutia maneno ya kiraghai.

Wote tutakufa yes,lakini sio kwa kuitana bali ni kwa mapenzi yake Mwenyezi Mungu.

Hapa nimekutaa Bro.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hamna ukweli wowote juu ya bandiko hili,umetumia mfano mmoja tu ambayo hauna ushahidi wowote.
Umeujengea hoja mfano wako kwa hisia ya tukio husika kwa kuutafutia maneno ya kiraghai.

Wote tutakufa yes,lakini sio kwa kuitana bali ni kwa mapenzi yake Mwenyezi Mungu.

Hapa nimekutaa Bro.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Losser Bad, kwanza ni kweli, aliyetuumba, na kutupa uhai, ndiye pekee mwenye mamlaka kuruhusu Roho iache mwili kwa kifo, mwili urudi kuwa mavumbi na Roho iende kwenye ulimwengu wa roho.

Hayo yote ni mipango na mamlaka ya Mungu, ila zaidi ya miili yetu kuwa na Roho wa Mungu, pia Mungu ametupa utashi, conscious ya kuamua, tumfuate yeye na kuzishika amri zake tuishi milele, au tumfuate shetani na mambo yake, tufe. Wazazi wetu wa mwanzo waliamua kutenda dhambi iliyotuumbia kifo, hivyo japo kifo ni kwa mapenzi ya Mungu, lakini kuna vifo vingi ni mipango ya mwovu shetani, japo anayetoa kibali sasa Roho iache mwili ni Mungu pekee.

Katika ule utashi, conscious Mungu aliotupa kuamua, ndani yake kuna powers za maamuzi zinaitwa "will Powers" ambazo ndicho kitu chenye nguvu kuliko kitu chochote duniani, hizo Will Powers, ni nguvu za Mungu zilizo ndani yetu na kila mtu anazo, nguvu hizi ndizo huamua hatima yetu, nikimaanisha sisi tuna nguvu za Kimungu ndani yetu, na shetani yupo kiturubuni tumuasi Mungu, kwa kutenda dhambi na kumfuata yeye. Mungu baada ya kutupa amri zake, pia ametupa utashi wa kuamua kumfuata yeye Mungu au kumfuata shetani, hivyo kuna baadhi ya matendo ya dhambi tunazotenda, yanasababisha vifo, japo Roho kutoka ni kazi ya Mungu.

Mfano ukiamua kumuua mtu kwa kumpiga risasi, huo ni ushetani, na kikawaida, risasi moja tuu inatosha kutoa roho ya mtu, lakini kama Mungu hajaruhusu Roho ile itoke, hata ukifanya ushetani mkubwa wa kumfyatulia mtu risasi 16, kama Mungu hajaruhusu Roho ile itoke, then mtu huyo atapona, na hata kama ingetokea akafa, huwezi kusema risasi zile ni mpango wa Mungu, no ni mpango wa shetani japo kibali cha Roho kutoka ni kazi ya Mungu

Hivyo kuna vifo vingi ni mipango ya shetani, ajali, maradhi, majanga, etc, na ndani ya vifo hivyo kuna vingine ni mtu mwenyewe ame will afe, kwa kukubali kuitwa na walio kifoni na yeye kukubali, hivyo ugonjwa, ajali, majanga ni kutafuta tuu sababu ya kuhalisha kifo ili tuu mtu uchomoke, lakini unaweza kuitwa kifoni, kwa kupitia will yako ukakataa kuitika, utaendelea kuishi

Watu walio karibu na wagonjwa mahututi, hufikia kipindi, mgonjwa anauona ulimwengu wa roho, anatamka kuwaona baadhi ya watu waliokufa zamani wanamfuata, atawataja kwa majina, kwa vile na nyinyi mko na mgonjwa wenu, na nyinyi hamuwaoni hao watu, basi mnamuona mgonjwa wenu kama anaona maluweluwe kisha mnanuona kama anaweweseka, kumbe ndio safari, kuitwa, kaitika, safari kimoja jumla

P.
Rejea
 
Back
Top Bottom