Ligi Kuu Bara: Yanga vs Simba - Uwanja wa Taifa (1-1)

Dah mabomu ya machozi balaa, Pale pale nilipokaa Ndio limetua mguuni kwangu, balaa tu
 
Ongeza nyama mkuu.
Mzee lilipotua miguuni nikahisi pumzi inakata, mbele yangu kuna dada anachupa ya maji nikampokonya nikanawa, mwingine kalala Chini ya viti, ilibidi nipande juu kabisa, pumzi ilikata kabisa, nikahisi network search
 
Kwani hili linataka mjadala....si ilikuwa wazi kuwa Yanga kabebwa na mbeleko ya bati......

Kujadili mechi ambayo ni dhahiri kuwa refa na wasaidizi wake waliingia na matokeo yao ni kuupoteza tu muda......
 
Shabiki wa simba ambaye hawezi kuvunja viti anitafute kwa namba hii 07_93888_8. Namba nyingine malizia.
 
Kiukweli refa aliyumba kidogo kipindi cha kwanza,
Lakini tukumbuke kuwa ushabiki wa Simba na Yanga upo ndani ya mioyo ya watu,
Nivigumu kuuchambua mpira wa simba na Yanga ukaweza kuacha ushabiki.

Mie nashukuru ndroo hii maana hali ingekuwa tete sana
Nilimuona Mwigulu akihamanika Leo Mara baada ya simba kurudisha
Sijui alitakaje!!!
Mpira ni mchezo usio tabirika kabisa .

SIMBA DAIMA
 
Hakika Vurugu za mashabiki wa soka Leo Uwanja wa Taiga zimesababishwa Na Refa wa mchezo wa Leo aliyekubali Goli la mkono lililofungwa Na Mchezaji Tambwe wa Yanga .Inashangaza sana kuona Refa amelikubali goli hilo wakati aliliona kwani alikuwa karibu Na Huyo mchezaji lakini Kwa makusudi alilikubaki.Jama haitoshi Refa huyo akampa kadi nyekundu Nahodha wa Klabu ya Simba hali ambayo iliamsha hasira Kwa Mashabiki wa Simba Na kusababisha vurugu kubwa.Wakati umefika Kwa TFF kutafuta Marefa nje ya Tanzania kwani Marefa wetu wanachezesha Kwa Ushabiki.
 
Shukran hapana mambo yaliingiliana kibarua kilikaba hapa nimepitia ndo nikaona nikupe pongezi game ilikuwa ngumu ila muwe na subira na uvumilivu pia haya mambo ya vurugu hayana nafasi karne hii
Hahahaah kweli mkuu ni washabiki wachache wasiojitambua ndio wanaosababisha haya mambo ya vurugu.!
 
Dah mabomu ya machozi balaa, Pale pale nilipokaa Ndio limetua mguuni kwangu, balaa tu
Pole mkuu. Pale askari nao walifanya kosa kuanza kurusha mabomu wakati wangeweza kutuliza zile vurugu bila kufanya vile. Kule jukwaani kulikuwa Na watoto Na walemavu ambao hata hawakufanya fujo ila huenda waliathirika Na hayo mabomu. Kungeweza kutokea vifo kwa watu kukanyagana
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji115] [emoji115] [emoji106] [emoji106] [emoji106] [emoji102] [emoji102] [emoji102]
Mda wote ulijificha ukasubiri matokeo kwanza.

Refa hakuwa upande wa Simba ila nashukuru imekuwa droo kuliko kufungwa na hawa Ndala aka vyura fc
 
Mchezo ulikosa ladha baada ya Yanga kushinda na ile kadi nyekundu. Hata baadhi yetu ambao ni mashabiki damu wa Yanga tuliliona kwamba refa hakuwa fair. Mechi kubwa kama hizi refa hatakiwi kutoa kadi nyingi mpk na nyekundu ila alitakiwa kuubalansi mchezo.

Mashabiki inabidi wabadilike hata wakionewa au wakifungwa sababu refa nae ni binadamu na kwenye mpira mistakes zipo. Kuvunja viti si jambo zuri kwa mashabiki iwe ni kwa club au taifa stars tukifungwa.
 
Kulialia haijawahi kusaidia chochote.

Kila MTU anajua maamuzi ya refa huwa hayabadiliki wewe unaenda kumsukuma ili iweje?

Safi sana refa
 
Hao ndo mkodisho FC hawafungi ila mipango tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…