Ligi kuu Tanzania: Yanga SC kukabiliana na Coastal union uwanja wa Mkwakwani

Ligi kuu Tanzania: Yanga SC kukabiliana na Coastal union uwanja wa Mkwakwani

Shadida Salum

Journalist at JamiiForums
Joined
Sep 11, 2020
Posts
69
Reaction score
105
20210304_130313.jpg

Baada ushindi wa goli 3-0 wa Yanga SC dhidi ya klabu ya Coastal Union katika mchezo wao wa mwisho uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa Oktoba 30, 2020, leo vijana wa Jangwani watakipiga na Coastal Union katika uwanja wa Mkwakwani

Kuelekea mchezo huo takwimu zinaibeba Coastal union maarufu Wagosi wa Kaya kwasababu Yanga hajashinda Mkwakwani kwa takribani misimu mitatu. Na kwa upande wa Coastal haijawahi kupoteza Mkwakwani tangu ligi kuanza

Yanga itawakosa wachezaji wake watano kutokana na sababu mbalimbali wakiwemo Saido Ntibazonkiza Mapinduzi Balama na Ramadhan Kabwili, ambao ni majeruhi,

Huku Carlos Carlinhos akiwa anatumikia kadi nyekundu aliyopata katika mchezo uliopita wa FA dhidi ya Ken Gold, huku beki Dickson Job akiwa na ruhusa maalumu.

Hata hivyo, Kaze atakuwa akitabasamu baada ya kurejea kwa mshambuliaji wake, Yacouba Sogne aliyekuwa majeruhi na hadi sasa ameifungia timu hiyo mabao manne kwenye ligi.

Michezo mingine itakayopigwa hii leo ni kati ya Mtibwa Sugar dhidi ya Biashara United, Polisi Tanzania dhidi ya KMC huku Tanzania Prisons ikipimana ubavu na vijana wa nyumbani Mbeya City
 
Nataka niwape coast union bao moja tuuu mech nzima.
 
Maisha Bwana! Wakati mtu mwingine anatoka jasho kwenye kibarua cha kutwa ili walau apate buku tano, wakati huo huo kuna mwingine baada ya Kazi kaahidiwa mamilioni (200,000,000/=)!!! Utopolo wakilia wivu tuwaelewe!
 
Back
Top Bottom