Linapokuja suala la filamu, nauheshimu sana Mkoa wa Tanga

Linapokuja suala la filamu, nauheshimu sana Mkoa wa Tanga

Kidedea (chini ya mwanadada Peace), Mambo Hayo (Nyota Ensemble chini ya Bishanga na wenzake) na Kaole yalikuwa makundi matatu tofauti yaliyorusha michezo ITV. Kidedea ndo iliyowaibua akina Jengua, Tabia n.k...
Kuna madogo hawajawahi kuona hii michezo aisee daah enzi hizo michezo mitamu sana kuangalia Mzee Magari na msemo wake wa 'Mahinda Maidota'
Kaole hio
 
Kidedea (chini ya mwanadada Peace), Mambo Hayo (Nyota Ensemble chini ya Bishanga na wenzake) na Kaole yalikuwa makundi matatu tofauti yaliyorusha michezo ITV. Kidedea ndo iliyowaibua akina Jengua, Tabia n.k...
Nimemkumbuka Bishanga Bashaija 😂
 
Inaitwa AUGUA, filamu ya kwanza nchini iliyopata udhamini wa Mfuko wa Utamaduni, mtayarishaji si Said Bawji (mwasisi wa Sani) bali kaka yake, Amri Bawji, ambaye alikuja kuwa mhariri wa Sani baada ya kifo cha Said. Pia alianzisha jarida la AMBHA...

Mimi nina nakala ya filamu hii...
Tunaomba utuwekee nakala yake hapa na Sisi tuiangalie haujaipandisha YouTube utupe link?
 
Kidedea ni tamthiliya ilivyokuwa ikirushwa ITV na kundi la Mambo hayo au kama sikosei Kaole Sanaa group .

Nsyuka ni filamu ya kwanza ya kutisha iliyopata mapokezi makubwa ila kabla yake kulikuwa na filamu ya kibuyu ambayo haikutamba sana.

Shamba kubwa nayo ni ya zamani sana.
Kibuyu ilikua vizuri Sana marehem king majuto aliitendea haki .
 
Kampuni ya kutengeneza filamu ya Whatever Film Productions ya Tanga, ndiyo kampuni namba moja Tanzania nzima. Jamaa wanajitahidi sana
 
Kidedea (chini ya mwanadada Peace), Mambo Hayo (Nyota Ensemble chini ya Bishanga na wenzake) na Kaole yalikuwa makundi matatu tofauti yaliyorusha michezo ITV. Kidedea ndo iliyowaibua akina Jengua, Tabia n.k...
Hey nafahamu yote hayo.

Kuhusu kidedea achilia mbali nakumbuka kama kuliwahi kuwa na tamthiliya yenye jina hilo.

Kidedea kama sikosei alikuwa yupo Mzee Jengua.

Kaole wapo akina Swebe Santana, Nina, Muhogo mchungu, nyamayao, kibakuli, Kanumba,Johari, Nora,Ray Vincent kigosi nk


Mambo hayo bishanga ,Richie Richie ,Waridi nk.
 
Kidedea ni tamthiliya ilivyokuwa ikirushwa ITV na kundi la Mambo hayo au kama sikosei Kaole Sanaa group .

Nsyuka ni filamu ya kwanza ya kutisha iliyopata mapokezi makubwa ila kabla yake kulikuwa na filamu ya kibuyu ambayo haikutamba sana.

Shamba kubwa nayo ni ya zamani sana.
Mmm mimi mzee wa busara ndo niliona kali zaid kwa upande wa horror
 
Ila mbona miaka ya 2000s kulikuwa na michezo ya kidedea na Maisha?

Nsyuka ilikuwa mbele sana miaka ya 2003 hivi.

Sio mtaalamu kwenye maswala ya filamu. Napata wakati mgumu kuamini kuwa filamu zilianza Tanga 1995.

Nieleweshwe.

Pia nimepitia website ya bodi ya filamu Tanzania. Inaonyesha filamu zimeanza toka kipindi cha ukoloni

Isee enzi hizo hukosi hii michezo saa tatu usiku jumamosi yaani tv hapo antena za samaki chenga kwa mbali yaani mara inazingua.

Alafu tamthilia za zamani mnakaa familia zima mnaangalia
Nakumbuka michezo km maisha ndani kuna kibakuli na nyama yao, muhogo mchungu bi stara mchepuko hatari sana huko kuna dr. Cheni na sekeseke lake..
Mchezo mwingine ni kidedea unaamshaamsha balaa huyo jegua alikuwa moto fireee kila binti anapita nae mtaani na mwanae pasua kichwa.

Mwingine ni mabo hayo hapo kuna muhaya bishanga na waridi huu sikumbuki vizuri maan ndio nilikuwa naanza kujitambua ila kilikuwa kipindi fulani hivi cha raha sana.
 
Back
Top Bottom