Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Ajali ya barabarani iliyohusisha gari mbili za abiria, Saibaba iliyokuwa inatoka Nachingwea kwenda Dar na Baharia iliyokuuwa inaelekea Nachingwea. Ajali hii imetokea jana mchana tarehe 05.10.2023 katika eneo la Kiwawa, Mkoani Lindi.
Tunasubiri Taarifa rasmi kutoka kwa mamlaka
=====
Watu saba wamekufa na wengine 22 wamejeruhiwa kufuatia ajali iliyotokea katika Kijiji cha Kiwawa kilichopo Wilaya ya Kilwa mkoani Lindi, ikihusisha basi aina ya Scania mali ya kampuni ya Saibaba na basi aina ya Tata, mali ya kampuni ya Baharia.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi, ACP Pili Mande amesema ajali hiyo imetokea jana jioni, ambapo miongoni mwa waliofariki dunia ni pamoja na dereva aliyekuwa akiendesha basi la kampuni ya Saibaba, Lucas John (59) ambaye ni mkazi wa Arusha pamoja na dereva wa basi la kampuni ya Baharia, Omari Alli Abdalah (49) mkazi wa Dare s salaam.
Amesema miili ya marehemu watano bado haijatambuliwa majina yao mpaka sasa.
Tunasubiri Taarifa rasmi kutoka kwa mamlaka
=====
Watu saba wamekufa na wengine 22 wamejeruhiwa kufuatia ajali iliyotokea katika Kijiji cha Kiwawa kilichopo Wilaya ya Kilwa mkoani Lindi, ikihusisha basi aina ya Scania mali ya kampuni ya Saibaba na basi aina ya Tata, mali ya kampuni ya Baharia.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi, ACP Pili Mande amesema ajali hiyo imetokea jana jioni, ambapo miongoni mwa waliofariki dunia ni pamoja na dereva aliyekuwa akiendesha basi la kampuni ya Saibaba, Lucas John (59) ambaye ni mkazi wa Arusha pamoja na dereva wa basi la kampuni ya Baharia, Omari Alli Abdalah (49) mkazi wa Dare s salaam.
Amesema miili ya marehemu watano bado haijatambuliwa majina yao mpaka sasa.