The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Tarehe 3 Machi 2025 Maimuna Pathan, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Lindi, amekabidhi bati 90 kuunga mkono juhudi za ujenzi wa nyumba ya mtumishi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Nachingwea. Bati hizi ni sehemu ya michango ya Pathan katika kuendeleza maendeleo ya Wilaya ya Nachingwea na Mkoa wa Lindi kwa ujumla.
Pia soma: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Pathan amesema kuwa ni furaha yake kuona wananchi wakishirikiana katika kujenga jamii bora, na alisisitiza kuwa ataendelea kuwa mstari wa mbele katika kuleta maendeleo kwa kutoa mchango kwa miradi muhimu, ikiwemo hiyo ya ujenzi wa nyumba za watumishi ndani ya Chama.
"Ujenzi wa nyumba hii ni muhimu sana kwa ustawi wa jamii na maendeleo ya Wilaya yetu. dhamira ya dhati ya Uwt Wilaya naiunga Mkono alisema Pathan.
Aidha Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Nachingwea, Salima Chilima, ametoa shukrani za dhati kwa Mhe. Pathan kwa mchango wake, akisema kuwa michango yake inatia nguvu na kuongeza ari ya kujitolea kwa viongozi wa UWT na jamii kwa ujumla.
"Pathan, tunakushukuru kwa moyo wako wa kujitolea na kujali maendeleo ya Wilaya yetu. Hii ni ishara ya wazi ya ushirikiano wa kweli kati ya viongozi na wananchi, na tunakuahidi kuwa tutadumisha juhudi zako katika kuleta maendeleo," alisema Chilima.
Mhe. Pathan ameendelea kuonyesha uongozi wa mfano katika Mkoa wa Lindi, akijitahidi kuwa kielelezo cha juhudi na kujitolea kwa maslahi ya umma, na sasa wananchi wa Nachingwea wana furaha ya kuwa na mtumishi wa umma anayejali na kuhamasisha maendeleo ya mkoa mzima.
Pia soma: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Pathan amesema kuwa ni furaha yake kuona wananchi wakishirikiana katika kujenga jamii bora, na alisisitiza kuwa ataendelea kuwa mstari wa mbele katika kuleta maendeleo kwa kutoa mchango kwa miradi muhimu, ikiwemo hiyo ya ujenzi wa nyumba za watumishi ndani ya Chama.
"Ujenzi wa nyumba hii ni muhimu sana kwa ustawi wa jamii na maendeleo ya Wilaya yetu. dhamira ya dhati ya Uwt Wilaya naiunga Mkono alisema Pathan.
Aidha Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Nachingwea, Salima Chilima, ametoa shukrani za dhati kwa Mhe. Pathan kwa mchango wake, akisema kuwa michango yake inatia nguvu na kuongeza ari ya kujitolea kwa viongozi wa UWT na jamii kwa ujumla.
"Pathan, tunakushukuru kwa moyo wako wa kujitolea na kujali maendeleo ya Wilaya yetu. Hii ni ishara ya wazi ya ushirikiano wa kweli kati ya viongozi na wananchi, na tunakuahidi kuwa tutadumisha juhudi zako katika kuleta maendeleo," alisema Chilima.
Mhe. Pathan ameendelea kuonyesha uongozi wa mfano katika Mkoa wa Lindi, akijitahidi kuwa kielelezo cha juhudi na kujitolea kwa maslahi ya umma, na sasa wananchi wa Nachingwea wana furaha ya kuwa na mtumishi wa umma anayejali na kuhamasisha maendeleo ya mkoa mzima.