Lindi: Wananchi waua majambazi waliopora 1.2

Lindi: Wananchi waua majambazi waliopora 1.2

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
KITINKWI.jpg

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Mtatiro Kitinkwi


Majambazi wawili ambao majina yao hayajafahamika wameuawa na wananchi wilayani Kilwa Mkoani Lindi, baada ya kuvamia duka la mfanyabiashara mmoja na kupora fedha taslimu kiasi cha shilingi milioni 1.2.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Mtatiro Kitinkwi amesema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 5, 2022, majira ya saa 2:00 usiku katika Kijiji cha Kisongo Pande wilayani Kilwa mkoani humo.

"Watu hawa walikuwa wanne, wawili waliingia ndani na wawili walibaki nje na kupiga risasi juu ili kuwatisha wananchi na yule aliyevamiwa walioingia ndani walipora milioni 1.2, kutokana na Polisi Kata na ulinzi shirikishi wananchi waliweza kujikusanya na kuwadhibiti majambazi hao," amesema Kamanda Kitinkwi.
 
Kuweka picha ya polisi badala ya kuweka picha ya tukio ni upuuzi mtupu
 
Wananchi wa Lindi nitakuja kuoa dada yenu kama shukurani kwa tukio hili.
Hongereni sana.
 
Wa Dar mchana kweupe hakuna aliyerusha hata jiwe kwa hamza badala yake walikuwa wanampisha alenge askari wetu.
 
Back
Top Bottom