Lini Watanzania tutaamka na kusema IMETOSHA?

Lini Watanzania tutaamka na kusema IMETOSHA?

Father of All

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
7,672
Reaction score
9,039
Ukiniuliza kama Tanzania ina kiongozi, nitajibu kuwa ina rais lakini si kiongozi. Ukiuliza kama Tanzania ina sera, nitakujibu kuwa ipo sera ya uchawa.

Ukiuliza, kiuchumi Tanzania inaongozwa na nini, nitakujibu kuwa sera yake ni ya shamba la bibi ambapo wezi huja na kugema watakavyo.

Ukiuliza kama Tanzania ni salama, nitakushauri ufanye utafiti na kuassess utekaji na kuporomoka kwa majengo.

Ukiuiza kama Tanzania ina future, nitakujibu kuwa hata past haina. Kama mwanafalsafa, nawaza tu.

Ukiuliza kama serikali inakusanya kodi na kuzitumia vizuri, nitakujibu kuwa inawakamua maskini na kuwapa matajiri wakwepa kodi na wapiga dili wanaoshirikiana na wanasiasa mafisi.

Ukiniuliza kama Tanzania ni kisiwa cha amani, nitakujibu kuwa ni kisiwa cha vurugu kinachongoja kulipuka.

Kwa wananchi wanavyoteseka huku watawala wakitanua, Tanzania inaweza kuzidiwa na hata Somalia.

Je, ni lini watanzania wataamka na kusema katu kuwa inatosha?
 
Viongozi ni kioo cha wananchi Mkuu.

Ukiona viongozi wa jamii Fulani ni wajinga, wezi, Wala rushwa au sifa zozote zile mbaya elewa jamii wanayotoka kwa sehemu kubwa ndio iko hivyo.

Jamii yenu akili haiwezi kuongozwa na kiongozi Mjinga
Jamii ya Watu waadilifu haiwezi kuongozwa na kiongozi asiye muadilifu

Tafakari
 
Viongozi ni kioo cha wananchi Mkuu.

Ukiona viongozi wa jamii Fulani ni wajinga, wezi, Wala rushwa au sifa zozote zile mbaya elewa jamii wanayotoka kwa sehemu kubwa ndio iko hivyo.

Jamii yenu akili haiwezi kuongozwa na kiongozi Mjinga
Jamii ya Watu waadilifu haiwezi kuongozwa na kiongozi asiye muadilifu

Tafakari

unamusema Trump nn kiaina?
 
Kwa wananchi wanavyoteseka huku watawala wakitanua, Tanzania inaweza kuzidiwa na hata Somalia. Je ni lini watanzania wataamka na kusema katu kuwa inatosha?
Hali ndiyo kama hivi mtu anajisimika halafu anajipalilia kwa kodi zako unategemea nini
 
Back
Top Bottom