SI KWELI Lionel Messi halisi akiwa anapiga gitaa

SI KWELI Lionel Messi halisi akiwa anapiga gitaa

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1


1729114802961.png
 
Tunachokijua
Lionel Messi ni mchezaji wa mpira wa miguu kutoka Argentina, anayetambulika kama mmoja wa wachezaji bora zaidi katika historia ya mchezo huo. Alizaliwa Juni 24, 1987, na amechezea klabu ya FC Barcelona kwa muda mrefu kabla ya kuhamia Paris Saint-Germain (PSG) mnamo 2021. Mwaka 2023, alijiunga na klabu ya Inter Miami nchini Marekani. Messi ameshinda tuzo nyingi, ikiwemo Ballon d'Or mara kadhaa, na alikuwa sehemu muhimu ya timu ya taifa ya Argentina iliyoshinda Kombe la Dunia 2022

Ufuatiliaji wa awali wa JamiiCheck umebaini video hii ya Messi akipiga gitaa iliwekwa Oktoba 7, 2024 kwenye ukurasa wa Instagram wa FutbolAlreves (tazama hapa).

UCHAMBUZI WA PICHA
Ufuatiliaji wa JamiiCheck umebaini kuwa Video hii imetengenezwa kwa Akili Mnemba kutokana na sababu zifuatazo

1. Vidole vya Lionel Messi havina umbo la kawaida, vinaonekana kama vimevimba.

2. Mijongeo na watu wanaopita nyuma ya Messi Wana Kasi kubwa isiyo ya kawaida.

Je, wewe umeona nini kingine?
Ni uongo,

1. Ukiangalia watu waliopo background, wanakimbia kwa kutetemeka alafu ni wadogo sana kwa size..

2. Angalia mkono wa kushoto vidole vyake ni vikubwa sana pia kama vina vetiligo, tofauti na vidole vya mkono wa kulia
 
Back
Top Bottom