LIONEL RICHIE: Mwamba na mtawala wa muziki wa Funk, Soul, Rhythm, Blues and country music

LIONEL RICHIE: Mwamba na mtawala wa muziki wa Funk, Soul, Rhythm, Blues and country music

Akilihuru

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2022
Posts
1,512
Reaction score
2,980
lionel.jpg


Habari ya mchana huu wakuu, leo nimekuja na historia ya huyu mwamba na mtawala wa aina mbali mbali za miziki laini, yan ile inayogusa mioyo ya mamilioni ya wapenzi wa miziki hapa duniani.

Aina hizo za miziki ni funk, soul, rhythm, blues and country.

Anaitwa Lionel Brockman Richie Jr (born June 20, 1949) huko Alabama, USA.

Lionel Richie ni miongoni mwa wasanii walioanza kuimba wakiwa na umri mdogo kabisa, ambapo yey alianza kujishughulisha na mziki akiwa na umri wa miaka 12 tu, na ni miongoni mwa waimbaji wenye kipaji cha uimbaji na utungaji.

Lionel Richie ana sauti ya pekee ambayo inaweza kumgusa mtu yoyote moyoni hata kama kile anachoimba haukielewi.

Ni mmoja kati ya wasanii wachache waliofanikiwa kuteka akili, na kugusa mioyo ya mamilioni ya watu mbali mbali duniani kutokana na ubora wa nyimbo zake, umaridadi wake, sauti yake na pia aina ya uimbaji wake.

Mnamo miaka ya 1985s Lionel Richie ndio alimshauri Michael Jackson kutunga ule wimbo wa "We Are the World" ili fedha zitakazopatikana katika wimbo ule ziweze kusaidia watoto wenye matatizo mbali mbali duniani kama vile yatima, wagonjwa na wale wenye uhitaji wa msaada.

Baadhi ya vibao vyake kati ya vyote vilivyo bora ni 👇

1) Endless love ft Diana Ross.
2) Ballerina girl.
3) Stuck on you.
4) Say you, Say me.
5) All Night Long.
6) We Are the World & Michael Jackson na wengine.

Kwa wale wazee wa miziki laini, nafikiri mnamjua vizuri mwamba huyu kwa sauti na uimbaji wake.

Kazi yake kubwa ni muimbaji, muandikaji wa nyimbo mbali mbali na ni mtungaji mahiri sana.

Karibuni wakuu tujadili na mengine mnayoyajua kumhusu mwamba huyu wa soft songs.

images (3).jpeg
 
Hiyo namba 3 bonge moja ya wimbo, harafu kuna nyingine kaimba inaitwa hello kuna binti mle kama kipofu harafu jamaa anampenda, ni noma
Ya hata mimi hiyo hello naikubali sana. Kifupi mwamba nyimbo zake almost zote ni moto wa kuotea mbali. Haijalishi msikilizaji ni mzee au kijana yeyote atakaesikiliza wimbo wa huyu mwamba lazima utaipenda tu.
 
Baada ya Commodores ku-hit big time Lionel Richie alienda kwenya dealership ya Mercedes Benz ili amnunulie kila member gari yake.

Kufika pale na kujitambulisha muuza magari alikuwa anmshangaa anamuuliza umesema ni mwanamuziki wa band inaitwa 'commandos'?

Richie akamwambia chukua hii namba ya governor wa bank of america mwambie Lionel Ritchie anataka kununua Benz hapa anaweza kulipa?

Muuza magari kweli alipiga simu ila alibaki mdomo wazi baada ya governor kumwambia huyo ni nani!
 
Back
Top Bottom