LIssu alikuwa kiongozi wa Chama cha Wanasheria wa Mazingira (LEAT), kimekufa baada ya Lissu na Nshala kufanya ubadhirifu, ndio apewe CHADEMA?

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
LEAT ilikuwa ni moja kati ya taasisi kubwa sana, ikipokea mabilioni kutoka kwa wafadhili, kiasi kwamba ikawa na ofisi mikoani, pale Mwanza walikuwa na ofisi jengo la Nyanza ghorofa ya juu,.

LEAT haikudumu. Lissu na Nshalla na mwenzao mmoja sasa marehemu walifyeka hela zote na kuingiza mifukoni mwao kiasi kwamba taasisi ikafa. Utawala wa hovyo ulitamalaki, mpaka leo wameacha madeni ya mishahara ya wafanyakazi.

Huyu ndio mumkabidhi chadema? Like serious? Lile jumba lake pamoja na la Nshalla yalijengwa wakati wizi umetamalaki LEAT.

Chadema sio taasisi ya majaribio!
 
Hii pia imebuma, vp mmeshampitisha au ndio mnakusanyika kijani kibichi kupiga vigelegele
 

Hapa ndo huwa nawaheshimu sana nyie Wanawake. Hii hali yako hata Mke wangu alipokuwa na Mimba yangu alikuwa kama wewe. Alinisema vibaya, alihangaika na mimi kunisema kwa watu. Alinichukia sana. Utadhani nlikuwa nimebaka. Alipojifungua yote yakaisha. So nakuelewa kinembe utakuwa vizuri tu kwa sasa vumilia.
 
Mwaka 2020 mlimteua agombee urais wa Tanzania hamkujua kama ni mbadhirifu? Chadema ni kubwa kuliko Tanzania?!!
Hizi siasa za kipumbavu ndizo zimesababisha wananchi wawe wanasusia chaguzi
 
Lete katiba ya LEAT hapa tuijadili angalau hata business plan, hakuna taasisi inayo anzishwa bila malengo, kwa maana unaijua kwa undani
 
Hata haiji ,
 
Wacha weee! Mmekosa hoja kiasi hicho? Chafuaneni kadiri muwezavyo lakini mjue kuwa This time MBOWE must go!
 
Mnazidi kujidhalilisha tu wajumbe wameshafanya maamuzi sahihi kuiokoa Chadema kutoka mikononi mwa Sultan Mbowe.
 
Mkuu wakati anapewa nafasi ya kugombea urais hilo hawakuliona??

Wakati anachaguliwa urais wa TLS hilo hawakuliona??

Mkuu punguza uongo!!
 
Bado hamjasema hadi mseme.
 
Kwa huyu Lissu, mwaka huu maji mtaita mma
 
Wenyewe mnasema kuwa kumbe Lisu ni fisadi alafu kipindi Cha uchaguzi mtataka watanzania wampigie kura

Sio Lisu tu CHADEMA yote imejaa mafisadi
 
Mbowe ameshachokwa.
Mnapoteza muda tu kwa hivi viroja vyenu.
 
Wenyewe mnasema kuwa kumbe Lisu ni fisadi alafu kipindi Cha uchaguzi mtataka watanzania wampigie kura

Sio Lisu tu CHADEMA yote imejaa mafisadi
Mnaweseseka sana, tulieni muive vizuri kwani hata maharage hurukaruka sana ili yaive.
Lisu ndiye mwenyekiti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…