Pre GE2025 Lissu amjibu Wasira. Asema Uchaguzi Mkuu usogezwe mbele kupata Katiba Mpya, vinginevyo watazuia uchaguzi kwa maandamano

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

..Wamewaza vizuri.

..Uchaguzi unaweza kusogezwa hadi 2026.

..Ndani ya muda huo tutakuwa tumepata Tume huru.

..Tunaweza pia kuamua awamu ijayo itakuwa ni miaka minne ili uchaguzi unaofuatia uwe 2030, au miaka 5 na uchaguzi uwe 2031.

..Kila upande utangulize maslahi ya taifa mbele.
 
Muda haupo,mwaka juzi na Jana kulitolewa mida wa kufanya marekebisho na Vyama vitoe mapendelezo Chadema walodharau.

Wengine walitoa na ndio maana inaitwa Tume huru ya Uchaguzi Kwa Sasa na hakuna kupita bila kupingwa.

..Wadau wengi, ikiwemo Chadema, walitoa mapendekezo kwa Kamati ya Bunge , lakini mwisho wa siku maoni hayo yalidharauliwa.

..Kamati ya Bunge ilitupilia mbali mpaka maoni ya viongozi wa Dini waliopendekeza watumishi wa serikali wasiwe wasimamizi wa uchaguzi, bali Tume iwe na watumishi wake yenyewe.

..Serikali ilitoa ahadi kwamba inao uwezo wa kuwasimamia na kuwadhibiti watumishi wake wasiharibu uchaguzi lakini jambo hilo limedhihirika kwamba haliwezekani kupitia uchaguzi wa serikali za mitaa.

..Serikali pia imekiuka sheria ya bunge inayoelekeza chaguzi zote kusimamiwa na Tume ya uchaguzi kwa kulazimisha uchaguzi wa serikali za mitaa usimamiwe na Ofisi ya Raisi Tamisemi.

..Mapendekezo ya Tundu Lissu yana mantiki na nia nzuri kama tutazingatia hali halisi, na maslahi ya taifa.
 
Maoni ya Katiba ya Chadema hakuna wa kuchukua ila maoni ya Katiba ya Wananchi.
 
Maoni ya Katiba ya Chadema hakuna wa kuchukua ila maoni ya Katiba ya Wananchi.

..Watanzania tuko milioni 60+ hivyo maoni yetu yatatoka kwa wawakilishi mbalimbali.

..Moja ya wawakilishi wa wananchi ambao maoni yao yalipuuzwa na Kamati ya Bunge ni VIONGOZI WA DINI.

..Viongozi wa Dini walipendekeza Tume Huru iwe na watumishi wake yenyewe, na isiwachukue wakurugenzi wa serikali kusimamia uchaguzi. Maoni hayo yalikataliwa na kamati ya Bunge.

..Tutangulize maslahi ya nchi mbele ktk suala hili.

..CCM bado ni chama kikubwa sana kulinganisha na vyama vya upinzani kwa hiyo hampaswi kuogopa Tume Huru ya uchaguzi.
 
Kwa hivyo twende na Samia hadi 2030 kwa mfano ikisha agombee kipindi chake cha pili?
Ccm hawatakibali, kama fomu ya kugombea kachukua kupitia mlango wa nyuma hawawezi kuvumilia mpaka mwaka huo, na sioni kitu chochote Cha kusabanisha uchaguzi uchelewe mpaka mwakani upande wa tume huru

Na upande wa mabadiliko ya katiba tulishamalizana ilikuwa ni suala la bunge kupitisha tu
 
Hata walioko Huwa wanaapa so hakuna Kisingizio .

Wakiwa tofauti na wakurugenzi kwani wanakuwa sio Watumishi wa Serikali na kulipwa na Serikali?
 
Bila KATIBA Mpya na Tume huru ya Uchaguzi, hapatafanyika uchaguzi wowote.
 
Yatakuwa yale yale kukosa wawakilishi ila uchaguzi utakuwepo
 
Rasimu ya Warioba irudi mezani, tufanye marekebisho na kuongeza baadhi ya mapendekezo Kisha tupate Tume huru ya Uchaguzi.

Nilisema,

2026 ni mwaka wa kukamilika na kuanza kutumika Katiba mpya, Judge Warioba akishuhudia Kwa macho yake.

Tusubiri.
 
Acha wazalendo wa kweli wenye akili kubwa waongoze mabadiliko ya kweli Tanzania.

Hata siku moja, mabadiliko ya kweli huwa hayaletwi na watu wajinga wajinga, punguani na wanafiki, kama ninyi.
Maandamano haya nitakuwepo🙏
 
Vyanzo vyangu vinaniambia, ujio wa Lissu umewapa panic kubwa,

Sasa wameanza mazoezi ya vyombo kukabiliana na mabadiliko.

Tutashinda💪
 
Lisu airudishe familia yake Tanzania ili tuungane nayo kupigania mabadiliko kwa maandamano, vinginevyo kelele zitakuwa hazina maana kwa Watanzania.

Tukishauana wanasiasa wanakaa chini na kugawana vyeo(nusu mkate) wanufaika kwanza ni hizo familia zao zilizoko Uberigiji, Marekani na Kanada. Wawarudishe nyumbani tuje kuvunja miguu wote.
 
Kama sheria hazikidhi uchaguzi kufanyika kwa nini usiahirishwe?
 
Umeandika ujinga tupu.
Hivi huko ccm huwa mnalishwa nini hicho kinachomaliza akili?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…