Uchaguzi 2020 Lissu hutaweza kututoa wamachinga mitaani

Uchaguzi 2020 Lissu hutaweza kututoa wamachinga mitaani

Mathayo Fungo

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2018
Posts
319
Reaction score
511
Imeandaliwa na Umoja wa Wamachinga Iringa

Kauli ya mgombea urais wa CHADEMA, Tundu Lissu kuahidi kuwaondoa wafanyabiashara ndogo ndogo maarufu kama wamachinga kwenye mitaa mbalimbali ya miji na majiji tunaipinga vikali kwasababu inataka kutuingiza kwenye umasikini.

Katika kampeni zake, Lissu alisema kuwa wamachinga wamekuwa wakifanya biashara katika mitaa na kuzuia hadi maduka ya watu. Kwamba akiingia atawahamisha mitaani ili akawajengee nje ya mji.

Alipoingia madarakani Rais Magufuli aliamua kubuni mbinu ya kuwarasimisha wamachinga na wengine wakiwemo mama na babalishe ambao mitaji yao iko chini ya shilingi millioni nne ili wafanye biashara rasmi bila kubughudhiwa na mgambo wa miji na majiji lakini Lissu anasema atafuta vitambulisho hivyo na kuwaondoa wajasiriamali kutoka maeneo waliopo sasa.

Ahadi hii ya Lissu inadhihirisha jinsi gani asivyo mzalendo na nchi yake kwani alipaswa kufikiri kwa kuzungumza juu ya namna gani atafanya ili kuendeleza hatua nzuri alizotufikishia Rais Magufuli na sio kuja na maneno ya kuturudisha nyuma.

Katika Awamu ya Tano, wamachinga tumepata fursa nyingi ikiwemo mikopo, uhuru wa kufanya shughuli zao na hata bima za afya mambo ambayo hatukuwahi kufikiria kuyapata. Tunajisikia faraja kuwa sehemu ya kuchangia maendeleo ya nchi kutokana na kodi tunayolipa na kufarijika kuona huduma mbalimbali za kijamii zinaboreshwa kupitia hili.

Sisi tutaendelea kuunga juhudi za Rais Magufuli na Serikali ya CCM kwani imekuwa ikitusikiliza na kushirikiana nasi katika kutatua kero zetu. Tutailinda misingi ya uzalendo iliyootoshwa na Serikali kwetu wamachinga, katu Lissu hatoweza kuivunja kwani imeota mizizi.
 
Machinga huwafuata wateja waliko Lisu anataka kuwalazimisha wafungue maduka wasitembee kuwafuata wateja waliko wakae tu Kama gogo la mnazi kusubiri mteja !!!

Umachinga hauendi Kama Lisu anavyotaka hataweza hata angekuwa Raisi

Jibu rahisi tu machinga tarehe 28 Oktoba ni kumnyima kura yeye na chama chake
 
Wenye maduka karibu wote wamekuwa wamachinga. Kodi za pango hazilipiki watu wameamua bora wamwage bidhaa nje tuu.

Sasa kamanda kasema ataweka mazingira rafiki kwa hao wafanyabiashara ili warudi kwenye fremu zao kama mwanzo, kuna ubaya hapo?

Nadhani ww ni mmachinga hewa, huezi elewa situations waliyonayo.
Unforgetable
 
Wenye maduka karibu wote wamekuwa wamachinga. Kodi za pango hazilipiki watu wameamua bora wamwage bidhaa nje tuu.

Sasa kamanda kasema ataweka mazingira rafiki kwa hao wafanyabiashara ili warudi kwenye fremu zao kama mwanzo, kuna ubaya hapo?

Nadhani ww ni mmachinga hewa, huezi elewa situations waliyonayo.
Unforgetable
Kodi ikiwa ndogo, kodi rafiki kila mmoja huilipa lakini kodi za CCM ni kubwa mno ndizo zimepelekea ukwepaji kodi hasa kwa wanaccm ambao wengi si walipa kodi lakini CCM huutumia pesa ya walipa kodi watanzania wote ambao siyo CCM kudidimiza demokrasia.
 
Mnatakiwa kufanya biashara zenu kwenye maeneo maalum! Ni kweli huwa mnazingua sana. Mnakaaje mbele ya maduka ya watu wanaolipa kodi lukuki za serikali, huku nyinyi mkimlipa huyo magufuli elfu 20 tu kwa mwaka?

Halafu huo utaratibu wa kufunga barabara una tija gani? Barabara zimetengenezwa kwa ajili ya vyombo vya moto na pia wewe mwenyewe kupita na siyo sehemu/duka la kutandazia bidhaa zako.

Hata ningekua mimi ndiyo Rais, ningewafurumusha na kuwahamishia sehemu sahihi ambayo mngeuza bidhaa zenu kitaalamu na kwa mafanikio makubwa zaidi.

Na ningewatoza pia kodi mnayostahili. Haiwezekani mlipe elfu 20 tu kwa mwaka huku wafanyakazi wakilipishwa maelfu na malaki ya kodi (PAYEE) kila mwezi. Nyinyi ni wahujumu uchumi wakubwa na hatushangai mnapo mng'ang'ania huyo mhujumu uchumi mwenzenu.
 
Wanaccm si walipa kodi lakini ni mabingwa wa kuitafuna kodi inayolipwa na wapinzani pamoja na watanzania wasio na vyama
 
Machinga wamekuwa kero Magufuli amejifanya mfuata sheria lakini kwa hili la kila mtanzania kuwa Machinga hakika ni hatari


Serikali inapoteza mapato mengi Sana ya Kodi kwa kuruhusu kila mtanzania kuwa Machinga.
CCM wanajua kutafuna kodi tu lakini wao hawalipi kodi
 
Umoja hauna hata Uongozi?

MATAGA wa Lumumba kaamua kujiita 'umoja wa Wamachinga-Iringa' [emoji2][emoji2][emoji2]
 
Machinga huwafuata wateja waliko Lisu anataka kuwalazimisha wafungue maduka wasitembee kuwafuata wateja waliko wakae tu Kama gogo la mnazi kusubiri mteja !!!

Umachinga hauendi Kama Lisu anavyotaka hataweza hata angekuwa Raisi

Jibu rahisi tu machinga tarehe 28 October ni kumnyima kura yeye na chama chake
Tundu na chama chake hawawajui watanzania wala hawajui watanzania wanataka nini....
Nautamani usiku wa October 28, 2020 mnoooo
 
Kwa hii pointi ya Lissu amejidanganya sana. Siyo kwamba machinga hawavioni nyumba vya kuweka biashara zao bali wanatembea maksudi ili wawakute wateje kokote waliko. Hivyo kuwambia wasiwafuate wateja hiyo Lissu kajidanganya
Sio wale wa kutembeza amboa hasa ndiko neno machinga limeanzia. Ni wale wanaopanga vitu chini mbele ya maduka.
Wanatembeza mitaani wataendelea kama kawaida. Hao hawakwepeki na hajawataja hao.
 
Wenye maduka karibu wote wamekuwa wamachinga. Kodi za pango hazilipiki watu wameamua bora wamwage bidhaa nje tuu.

Sasa kamanda kasema ataweka mazingira rafiki kwa hao wafanyabiashara ili warudi kwenye fremu zao kama mwanzo, kuna ubaya hapo?

Nadhani ww ni mmachinga hewa, huezi elewa situations waliyonayo.
Unforgetable
Acha kutulaghai ndg. Atawaambia wenye frem washushe bei mpaka 20000 kwa mwezi.
Mtaji laki moja frem kwa mwaka 700000. Hata aksamehe kodi bado ni ngumu.
 
Sio wale wa kutembeza amboa hasa ndiko neno machinga limeanzia. Ni wale wanaopanga vitu chini mbele ya maduka.
Wanatembeza mitaani wataendelea kama kawaida. Hao hawakwepeki na hajawataja hao.

Sent from my Nokia 6.1 using JamiiForums mobile app
Hao wapanga vitu chini ni machinga wa kutembea vile vile hupanga wateja wapita njia walipo wao shida Yao sio kuwa na frame hata ungewapa bure Leo hawataki hizo frem wao wanaenda sehemu za watembea miguu wengi wanaweka chini bidhaa zao yaweza kuwa barabarani kabisa ,stendi ,misikitini.makanisani au popote

Huwezi badili staili Yao hawahitaji shida Yao sio vifremu vya viduka nenda hata unawaulize

Lisu anachoongea kwa hao machinga hakikubaliki October 28 yeye na chama chake tukikitae
 
Acha kutulaghai ndg. Atawaambia wenye frem washushe bei mpaka 20000 kwa mwezi.
Akiwasaidia kujenga? Kea hiyo atarudishe tume ya Bei kumpangia mfanyabiashara Bei za fremu zake? Kwa hiyo atafuta soko huria kupanga Bei Bei za fremu zitakuwa zinapangwa Ikulu?

Lisu kwenye issue za uchumi Ni mweupe kichwani

Wafanyabiashara Chadema hao wanakuja na tume ya Bei hizo Bei a fremu zenu Bei itapangwa Ikulu!!!!
 
Back
Top Bottom