Pre GE2025 Lissu: Kama wanakamata viongozi wa upinzani wakati wa kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa uchaguzi Mkuu 2025 itakuwaje?

Pre GE2025 Lissu: Kama wanakamata viongozi wa upinzani wakati wa kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa uchaguzi Mkuu 2025 itakuwaje?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Lissu asema kitendo cha kiongozi wa upinzani kukamatwa kwa nchi inayojiita ya kidemokrasia ni aibu, akaongeza kama wanafanya hivi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa kwenye uchaguzi mkuu 2025 itakuwaje? Lissu ameongeza kuwa kukamatwa kwa Mbowe iwe fundisho wasije kurudia tena kudanganywa na amewataka polisi wamuachie Mbowe.

Kupata taarifa na matukio yote kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

ameongeza kuwa kitendo hiki (cha viongozi wa CHADEMA kukamatwa) kinamaanisha kwanza hakuna uchaguzi, na pia chama na serikali hiyo inayosababisha hayo kimekwisha, ni mfu na kinachobebwa bebwa. Lissu akaongeza kuwa CCM ya sasa ni ya wakurugenzi, usalama wa taifa na polisi, sababu bila ya polisi hawawezi hata kufanya mkutano.

Lissu ametoa kauli hiyo wakati akiwanadi wagombea wa Serikali za Mitaa katika wilaya za Nyamagana na Ilemela.


 
Lissu ameteleza ulimi.
Lissu ndiye mwenye kazi ya kumtoa Freeman mahabusu.
Afanye kazi ya kumtoa,aache kujadili 2025.
 
Back
Top Bottom