Uchaguzi 2020 Lissu kuzungumzia tozo kwa wajawazito Sumbawanga, ni kweli zipo ndugu zangu CCM au anadanganya?

Hili la universal health au nhif/chf zinatakiwa zifanyiwe kazi ya kitaaluma kutokana na mfumo wetu kama nchi kuwa na watu wengi kwenye informal sector ambao hawajawa integrated kwenye hizo funds na kuona kiasi cha kuchangia na namna ya kuchangia
 
Sijakumbana na hizo tozo ndo maana nawataka muingie field zaidi na mfahamu kwa undani badala ya kulalamika

Hadi lini mtakua mnalalamika kwa masuala ya kuambiwa?
Mkuu kwanza hatujalalamika, tumekuja kuuliza ili tupate ufahamu, ,kama unatarifa sahihi juu yahizo tozo tunaomba utufahamishe, ili siku tukiwa nawenza wetu twende huku tukijua hizo tozo nizanini, au nasisi tuelimishe jamii juu yahizo tozo.
 
Mwaka jana mi nimekwenda Muhimbili mke alikua na changamoto kwenye uzazi wamemfanyia operesheni pale mtoto alikua ashafia tumboni, baada ya siku tatu napewa bill ya 2mil nikasema kama hapa ni National Hospital na mtu hana uwezo itakuaje. Ilibidi niparue akiba yangu niwalipe. Wanakwambia usipolipa leo kesho bill ya kulala inaongezeka.

Kitu kilinitatiza dressing ya kidonda walipompasua kwa siku niliona wameandika 50,000 nikasema yani eusol na Spirit na pamba na gloves wanatumia nyingi kiasi gani.

By the way serikali inatakiwa iangalie upya gharama za matibabu sio rafiki kivile kwa mtu asiye na bima.
 
Sijakumbana na hizo tozo ndo maana nawataka muingie field zaidi na mfahamu kwa undani badala ya kulalamika

Hadi lini mtakua mnalalamika kwa masuala ya kuambiwa?
Mimi mke wangu katozwa elfu 50 baada ya kujifungua mtoto wa kiume last 2 month na hakuna maelezo yanayoeleweka kutoka hospital.

So nalalamika kwa pesa niliyoitoa mfukoni mimi mwenyewe.

Numbisa wewe shukuru haujatozwa tozo husika ila haina haja ya kuwabeza wanaolalamika baada ya kutozwa.
 
Ulaya ya wapi hujifungui bure?
Mimi ninaishi Marekani na ninajua kuwa hakuna "free lunch" kwenye huduma za afya pamoja na kuwapo kwa Obamacare; bado utalipa copay na deductable ambazo ni takribani $500 na zaidi kwa kujifungua kwani wakati wa kujifungua chumbani kunakuwa na timu ya manesi kama watatu na madakati kama watatu pia ambao wako tayari kufanya operesheni wakati wowote iwapo kujifungua kwako kutaonekana kutokwenda vizuri. Ule muda wote wa uchungu utaulipia. Hawakuchaji kwa wewe kujifungua bali wanachaji kwa muda ule wa wewe kuwa leba hadi unajifungua.
 
Mkuu kwa huko nikwa Marekani, tunauliza kwa Tz nikwanini hio tozo ipo?. Na kwanini mzazi akijifungua Mtoto wakiume atozwe elfu 50, kwa mtoto wakike atozwe elfu 30?.
joka kuu TUJITEGEMEE
 
je alipoenda kujifungulia ndipo alipoandikiwa kwenye kadi yake ya clinic? Kama sio basi tozo inahusika na mngewauliza kwann 50000

Kingine ungepewa huduma mbovu ingefaa kulalamika sasa huduma nzuri,mwanao ana afya bado unalalamika

Vya bure gharama mkuu. Ona elimu ilivyoshuka kisa tulitaka elimu bure.
 
Mwenza wako atafundishwa na ndio maana kuna clinic kwa wajawazito
Mkuu kwanza hatujalalamika, tumekuja kuuliza ili tupate ufahamu, ,kama unatarifa sahihi juu yahizo tozo tunaomba utufahamishe, ili siku tukiwa nawenza wetu twende huku tukijua hizo tozo nizanini, au nasisi tuelimishe jamii juu yahizo tozo.
 
Mkuu elimu imeshuka vipi, huku tukiambiwa ufaulu umeongezeka?. Maana Serikali inapima kushuka/kupanda kwa elimu kwa kuangalia kigezo cha ufaulu.
 
Hakuna majibu ya maana tuliopewa.

Bure ni gharama ndiyo maana CDM wananadi sera ya Bima ya Afya kwa kila raiya, nadhani bima ya afya sio bure na ndiyomaana tunashangaa wanaoshabikia CCM wanasema wanawajali watZ wakati vijijini hali ngumu alafu wanatozwa kodi za mimba.

Mimi na wewe Numbisa kutoa elfu 50,000 sio issue ila vipi kuhusu shangazi yako huko Burigi anamudu hizo gaharama??
 
Kushuka na kupanda kwa elimu wananzengo tunapima kiswahili cha facebook siku hizi kuna tatizo la uandishi wa r,l etc
Mkuu elimu imeshuka vipi, huku tukiambiwa ufaulu umeongezeka?. Maana Serikali inapima kushuka/kupanda kwa elimu kwa kuangalia kigezo cha ufaulu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…