Lissu: Mbowe aliitisha kikao nisitie nia ya kugombea uenyekiti, asema CHADEMA kimepoteza watu wa maana sababu ya 'kuatamia madaraka'

Lissu: Mbowe aliitisha kikao nisitie nia ya kugombea uenyekiti, asema CHADEMA kimepoteza watu wa maana sababu ya 'kuatamia madaraka'

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Mgombea uenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu amesema baada ya 'mastori ya town' kusambaa anataka kugombea uenyekiti aliitwa kwenye kikao na watu watatu wanaoheshimika kwenye jamii, anasema kwenye kikao hicho Mbowe alisema hatagombea uenyekiti lakini pia alimkatalia Lissu asigombee nafasi hiyo kitu ambacho Lissu alikikataa.

Lissu anasema mpasuko wake na Mbowe ulianzia mbali kabla ya kutangaza nia, mpasuko wao ulianzia baada ya kuhoji maridhiano yaliyoingiwa na Mbowe. Lissu amesema chama cha CHADEMA kimepoteza watu wengi wa maana kwa sababu ya 'watu kuatamia madaraka'.

Lissu amesema yeye binafsi anajiona anatosha kwenye nafasi ya uenyekiti na anavyojiona kunaenda kuthibitishwa na wanachama wa Chadema wenye sifa za kupiga kura January 21.

Clouds TV
 
Inaonekana Lissu hafai katika hiyo nafasi ila tatizo ni kwamba hakuna mbadala wa Mbowe mwenye kufaa kwenye hiyo nafasi hata ukimtoa huyo Lissu.
 
Back
Top Bottom