Pre GE2025 Lissu na CHADEMA Plan B ni ipi ikiwa wananchi hawataingia barabarani kudai mabadiliko ya uchaguzi?

Pre GE2025 Lissu na CHADEMA Plan B ni ipi ikiwa wananchi hawataingia barabarani kudai mabadiliko ya uchaguzi?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

CHADEMA imeamsha matumaini ya Watanzania hasa baada ya Lissu kupiga krosi moja matata na kuwa Mwenyekiti Taifa. Watanzania walioonesha kuchoshwa na uchawa, ubadhilifu wa mali za umma na mazonge mengine yanayotokea nchini wameanza kupata matumaini huenda mambo yatabadilika for good.

Kuweka mambo sawa Lissu na CHADEMA ni muhimu kukata mzizi wa fitina kutoka kwenye katiba ili kutoka hapo msingi (uchaguzi) uwe imara kuweza kuhumili vishindo vya wanaokuja juu yake. Swali muhimu ni je, wananchi wapo tayari?

Ni jambo moja watu kushangilia na kuona wamepata mkombozi na ni jingine kubeba yale anayoyaamini na kuyafanyia kazi. Sio kumkatisha tamaa Lissu na CHADEMA lakini wanaona wanachofanya sasa inatosha kuwafanya watanzania wasimame kidete kuyataka mabadiliko hayo?

Mimi naona wengi hawapo tayari, siyo kwamba hawaelewi kile Lissu au CHADEMA wanahubiri, hapana, wanawaelewa vizuri lakini hawapo tayari kunyanyua mguu na kuanza kuchukua hatua. Na hili ni kwasababu bado wabongo hawajapigika vizuri, bado hawajaonja joto ya jiwe kufikia hatua ambayo hawana njia nyingine ya ku survive.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Wakigeuka hivi serikali/CCM inatoa kitu kidogo wanatulia, kelele zikikolea sana unaona ajira za walimu zinashushwa kundi moja linapiga kimya, wanabaki wachache inakuwa haina maana tena, hata sauti zao hazina athari yoyote. Baadhi watapigia kelele huduma mbaya za afya mara utaona kuna misaada ya uongo na kweli inapelekwa sehemu yanageuka mapambio tena, yaani fulani ana huruma kweli, na harakati zinaishia hapo.

Tunaona wasanii wetu hapa kila kukicha kuwa chawa na kutetea matumbo yao, tunawalia kooni weee alkini atakuja mwenye team yake atakwambia mi huniambii kitu kwa fulani, kama hamumpendi ni nyie.... mwishowe tunaendelea vile vile kwenye mzunguko wa kutumiwa, wanalipwa milions kupumbumbaza watu wakati fedha hizo zingekuwa zinatumika kuboresha huduma zinazozorota na kuchechemea.

Tunatoleana mifano ya Wakenya kila mara na jinsi walivyo wamoja kupigania haki... tunachokikosa kwetu ni hiko, hatujapigika kisawasawa kuelewa thamani yetu, kuelewa thamani ya kile tunachostahili, nguvu yetu na nini tunatakiwa kufanya kuhakikisha kila anayepata nafasi anawajali wananchi na kuhakikisha kuna huduma bora.

Mna mpango mwingine ikiwa wananchi hawatanyanyua miguu na kuchukua hatua ya kwanza?
 
Wakuu,

CHADEMA imeamsha matumaini ya Watanzania hasa baada ya Lissu kupiga krosi moja matata na kuwa Mwenyekiti Taifa. Watanzania walioonesha kuchoshwa na uchawa, ubadhilifu wa mali za umma na mazonge mengine yanayotokea nchini wameanza kupata matumaini huenda mambo yatabadilika for good.

Kuweka mambo sawa Lissu na CHADEMA ni muhimu kukata mzizi wa fitina kutoka kwenye katiba ili kutoka hapo msingi (uchaguzi) uwe imara kuweza kuhumili vishindo vya wanaokuja juu yake. Swali muhimu ni je, wananchi wapo tayari?

Ni jambo moja watu kushangilia na kuona wamepata mkombozi na ni jingine kubeba yale anayoyaamini na kuyafanyia kazi. Sio kumkatisha tamaa Lissu na CHADEMA lakini wanaona wanachofanya sasa inatosha kuwafanya watanzania wasimame kidete kuyataka mabadiliko hayo?

Mimi naona wengi hawapo tayari, siyo kwamba hawaelewi kile Lissu au CHADEMA wanahubiri, hapana, wanawaelewa vizuri lakini hawapo tayari kunyanyua mguu na kuanza kuchukua hatua. Na hili ni kwasababu bado wabongo hawajapigika vizuri, bado hawajaonja joto ya jiwe kufikia hatua ambayo hawana njia nyingine ya ku survive.

Wakigeuka hivi serikali/CCM inatoa kitu kidogo wanatulia, kelele zikikolea sana unaona ajira za walimu zinashushwa kundi moja linapiga kimya, wanabaki wachache inakuwa haina maana tena, hata sauti zao hazina athari yoyote. Baadhi watapigia kelele huduma mbaya za afya mara utaona kuna misaada ya uongo na kweli inapelekwa sehemu yanageuka mapambio tena, yaani fulani ana huruma kweli, na harakati zinaishia hapo.

Tunaona wasanii wetu hapa kila kukicha kuwa chawa na kutetea matumbo yao, tunawalia kooni weee alkini atakuja mwenye team yake atakwambia mi huniambii kitu kwa fulani, kama hamumpendi ni nyie.... mwishowe tunaendelea vile vile kwenye mzunguko wa kutumiwa, wanalipwa milions kupumbumbaza watu wakati fedha hizo zingekuwa zinatumika kuboresha huduma zinazozorota na kuchechemea.

Tunatoleana mifano ya Wakenya kila mara na jinsi walivyo wamoja kupigania haki... tunachokikosa kwetu ni hiko, hatujapigika kisawasawa kuelewa thamani yetu, kuelewa thamani ya kile tunachostahili, nguvu yetu na nini tunatakiwa kufanya kuhakikisha kila anayepata nafasi anawajali wananchi na kuhakikisha kuna huduma bora.

Mna mpango mwingine ikiwa wananchi hawatanyanyua miguu na kuchukua hatua ya kwanza?
Suala la kudai na kupigania Haki siyo suala linalomhusu Tundu Lisu peke yake, kila Mwananchi mpenda Haki na mpenda mabadiliko anao wajibu wa msingi kabisa wa kudai na kupigania Haki. It's an individual duty.

Remember: "When injustice becomes law resistance becomes duty."
By Thomas Jefferson.

Hivyo basi, Wananchi wote tunao wajibu wa kutoa ushirikiano wote kwa Watu wengine Wapenda Haki ambao wanaonyesha wazi kabisa dhamira zao za dhati katika kudai na kupigania HAKI zilizoporwa.
 
Suala la kudai na kupigania Haki siyo suala linalomhusu Tundu Lisu peke yake, kila Mwananchi mpenda Haki na mpenda mabadiliko anao wajibu wa msingi kabisa wa kudai na kupigania Haki. It's an individual duty.

Remember: "When injustice becomes law resistance becomes duty."
By Thomas Jefferson.

Hivyo basi, Wananchi wote tunao wajibu wa kutoa ushirikiano wote kwa Watu wengine Wapenda Haki ambao wanaonyesha wazi kabisa dhamira zao za dhati katika kudai na kupigania HAKI zilizoporwa.
Ndio nimeuliza hapo Mkuu, unadhani watanzania wako tayari kunyanyua mguu? If not kuna mpango gani? Lazima uangalie pande zote... na kwa nature ya watanzania mizani inadondokea pabaya
 
Kwanza kabisa mimi napinga namna yoyote ya maandamano kwa sababu hata mimi mwaka 2009/2010 nilikuwepo huko NMC Arusha wakati Dokta Slaa ni moto kweli, na nimeshuhudia mwenyewe vyombo vya ulinzi vikitawanya watu kwa mabomu ya machozi na hata kuna vifo vilitokea(hivyo sikushuhudia).

Maandamano yanayosemwa hapo yako karibu sana na vita.

Na ni kwanini tuingie katika vita katika nchi hii aliyotupa Mungu?

Kwa faida gani? CCM ina matatizo lakini nikuhakikishie Hakuna muujiza wa CHADEMA au chama gani sijui.

Hivi kwa mfano Lissu aliposimama na kusema kuwa tutashitakiwa MIGA, kisa ya Hayati Magufuli alikuwa akifanya dhidi ya wawekezaji, na ni kweli wawekezaji walikuwa wanakosea!

Je, nini tafsiri ya hiyo kauli ya Lissu?
Hivi wewe unaweza kumtetea mgeni anayevunja sheria dhidi ya ndugu yako ambaye anataka kumweka katika mstari mgeni anayevunja sheria?

Mbinu zooote za maandamano zimeshatumika, na hazikusaidia, atleast akili ya maridhiano ingeweza kuleta matokeo mazuri.


Kuandamana huko anakodai Lissu ni nini basi?
"kuandamana ni sawa na kuiharibu nyumba uliyoijenga kwa mikono yako ukidhani hasara ni ya Serikali"
 
Kwanza kabisa mimi napinga namna yoyote ya maandamano kwa sababu hata mimi mwaka 2009/2010 nilikuwepo huko NMC Arusha wakati Dokta Slaa ni moto kweli, na nimeshuhudia mwenyewe vyombo vya ulinzi vikitawanya watu kwa mabomu ya machozi na hata kuna vifo vilitokea(hivyo sikushuhudia).

Maandamano yanayosemwa hapo yako karibu sana na vita.

Na ni kwanini tuingie katika vita katika nchi hii aliyotupa Mungu?

Kwa faida gani? CCM ina matatizo lakini nikuhakikishie Hakuna muujiza wa CHADEMA au chama gani sijui.

Hivi kwa mfano Lissu aliposimama na kusema kuwa tutashitakiwa MIGA, kisa ya Hayati Magufuli alikuwa akifanya dhidi ya wawekezaji, na ni kweli wawekezaji walikuwa wanakosea!

Je, nini tafsiri ya hiyo kauli ya Lissu?
Hivi wewe unaweza kumtetea mgeni anayevunja sheria dhidi ya ndugu yako ambaye anataka kumweka katika mstari mgeni anayevunja sheria?

Mbinu zooote za maandamano zimeshatumika, na hazikusaidia, atleast akili ya maridhiano ingeweza kuleta matokeo mazuri.


Kuandamana huko anakodai Lissu ni nini basi?
"kuandamana ni sawa na kuiharibu nyumba uliyoijenga kwa mikono yako ukidhani hasara ni ya Serikali"
"The right cannot be given as a gift by the oppressor, it must be demanded by the oppressed."

Martin Luther King Jr
 
Lisu ameonyesha njia,kimaisha yupo daraja la juu kabisa.
Kama raia wataamua kupiga kimya basi itakuwa ni kwa faida yao,TAL atahitajika kukung'uta miguu na kuendelea na mambo yake...

Kenge hasikii hadi avujishwe damu...
 
Kwanza kabisa mimi napinga namna yoyote ya maandamano kwa sababu hata mimi mwaka 2009/2010 nilikuwepo huko NMC Arusha wakati Dokta Slaa ni moto kweli, na nimeshuhudia mwenyewe vyombo vya ulinzi vikitawanya watu kwa mabomu ya machozi na hata kuna vifo vilitokea(hivyo sikushuhudia).

Maandamano yanayosemwa hapo yako karibu sana na vita.

Na ni kwanini tuingie katika vita katika nchi hii aliyotupa Mungu?

Kwa faida gani? CCM ina matatizo lakini nikuhakikishie Hakuna muujiza wa CHADEMA au chama gani sijui.

Hivi kwa mfano Lissu aliposimama na kusema kuwa tutashitakiwa MIGA, kisa ya Hayati Magufuli alikuwa akifanya dhidi ya wawekezaji, na ni kweli wawekezaji walikuwa wanakosea!

Je, nini tafsiri ya hiyo kauli ya Lissu?
Hivi wewe unaweza kumtetea mgeni anayevunja sheria dhidi ya ndugu yako ambaye anataka kumweka katika mstari mgeni anayevunja sheria?

Mbinu zooote za maandamano zimeshatumika, na hazikusaidia, atleast akili ya maridhiano ingeweza kuleta matokeo mazuri.


Kuandamana huko anakodai Lissu ni nini basi?
"kuandamana ni sawa na kuiharibu nyumba uliyoijenga kwa mikono yako ukidhani hasara ni ya Serikali"
Mkuu jaribu kufuatilia. TZ tumelipishwa pesa nyingi sana kwa sababu ya sera za mwendazake. Maybe mengine huyajui au huyafuatilii. Unakumbuka ndege zetu zilivyozuiliwa huko South na Ulaya? au hujui? TAL was right. Ila kama alivyoandika mkuu Lord denning sasa hivi tumekuwa na kizazi cha hovyo sana. vijana hawapendi kujishughulisha au kusoma habari zenye mashiko. watu wanataka twitter na insta.

Mkuu kama alivyosema John Wickzer Mulholland, jukumu la mapambano ni la kila mtu. Ukishiba leo, kumbuka kuna kesho.
 
Wakuu,

CHADEMA imeamsha matumaini ya Watanzania hasa baada ya Lissu kupiga krosi moja matata na kuwa Mwenyekiti Taifa. Watanzania walioonesha kuchoshwa na uchawa, ubadhilifu wa mali za umma na mazonge mengine yanayotokea nchini wameanza kupata matumaini huenda mambo yatabadilika for good.

Kuweka mambo sawa Lissu na CHADEMA ni muhimu kukata mzizi wa fitina kutoka kwenye katiba ili kutoka hapo msingi (uchaguzi) uwe imara kuweza kuhumili vishindo vya wanaokuja juu yake. Swali muhimu ni je, wananchi wapo tayari?

Ni jambo moja watu kushangilia na kuona wamepata mkombozi na ni jingine kubeba yale anayoyaamini na kuyafanyia kazi. Sio kumkatisha tamaa Lissu na CHADEMA lakini wanaona wanachofanya sasa inatosha kuwafanya watanzania wasimame kidete kuyataka mabadiliko hayo?

Mimi naona wengi hawapo tayari, siyo kwamba hawaelewi kile Lissu au CHADEMA wanahubiri, hapana, wanawaelewa vizuri lakini hawapo tayari kunyanyua mguu na kuanza kuchukua hatua. Na hili ni kwasababu bado wabongo hawajapigika vizuri, bado hawajaonja joto ya jiwe kufikia hatua ambayo hawana njia nyingine ya ku survive.

Wakigeuka hivi serikali/CCM inatoa kitu kidogo wanatulia, kelele zikikolea sana unaona ajira za walimu zinashushwa kundi moja linapiga kimya, wanabaki wachache inakuwa haina maana tena, hata sauti zao hazina athari yoyote. Baadhi watapigia kelele huduma mbaya za afya mara utaona kuna misaada ya uongo na kweli inapelekwa sehemu yanageuka mapambio tena, yaani fulani ana huruma kweli, na harakati zinaishia hapo.

Tunaona wasanii wetu hapa kila kukicha kuwa chawa na kutetea matumbo yao, tunawalia kooni weee alkini atakuja mwenye team yake atakwambia mi huniambii kitu kwa fulani, kama hamumpendi ni nyie.... mwishowe tunaendelea vile vile kwenye mzunguko wa kutumiwa, wanalipwa milions kupumbumbaza watu wakati fedha hizo zingekuwa zinatumika kuboresha huduma zinazozorota na kuchechemea.

Tunatoleana mifano ya Wakenya kila mara na jinsi walivyo wamoja kupigania haki... tunachokikosa kwetu ni hiko, hatujapigika kisawasawa kuelewa thamani yetu, kuelewa thamani ya kile tunachostahili, nguvu yetu na nini tunatakiwa kufanya kuhakikisha kila anayepata nafasi anawajali wananchi na kuhakikisha kuna huduma bora.

Mna mpango mwingine ikiwa wananchi hawatanyanyua miguu na kuchukua hatua ya kwanza?
Mpaka tutakapoacha kuliangalia swala la kudai haki kama ni swala la TAL au Chadema.

Ila sasa nadhani sasa hivi mambo yatakuwa magumu zaidi. Unajua wafadhili (USAID?) wamekuwa wanatekeleza majukumu ya serikali (afya, elimu nk) na serikali inachukua credit. Sasa hivi, itabidi gova ipambane. Na ikiona inashindwa, itaamua kuinvest kwa vijana wa Wambura kudeal na wanaoinua sauti dhidi ya watawala.
 
Mkuu jaribu kufuatilia. TZ tumelipishwa pesa nyingi sana kwa sababu ya sera za mwendazake. Maybe mengine huyajui au huyafuatilii. Unakumbuka ndege zetu zilivyozuiliwa huko South na Ulaya? au hujui? TAL was right. Ila kama alivyoandika mkuu Lord denning sasa hivi tumekuwa na kizazi cha hovyo sana. vijana hawapendi kujishughulisha au kusoma habari zenye mashiko. watu wanataka twitter na insta.

Mkuu kama alivyosema John Wickzer Mulholland, jukumu la mapambano ni la kila mtu. Ukishiba leo, kumbuka kuna kesho.
Mkuu kama nakumbuka hizo ndege zilikamatwa kutokana na madeni na sio suala la wawekezaji.

Pia Lissu atasemaje tutashtakiwa yeye hapo si alikuwa akiside na wawekezaji?

Kwa mtu anayeipenda nchi yake atasema hawa wawekezaji wamekosea ila njia hii haifai hii ndio iko sahihi.

Ni sawa na mimi nishadadie maandamano saivi wakati najua mwisho wa maandamano ni uharibifu, sababu nimeshayashuhudia!

Na huko marekani kwa Luther King Jr, watu weusi wamefanikiwa wapi?

Wewe kwenye hata makampuni makubwa huko marekani unawaona watu weusi?
 
Tupige kura tuone nani ataenda na nani hataenda majibu utakaopatikana wayatumie kama roadmap

Nashauri pia njia hiyo waitumie katika mitandao mingine ili kura ziwaongoze kuamua njia wanayoitaka kuitumia

Tulipiga kura humu kuwa atashinda na akashinda kweli social media is real
 
Kwanza kabisa mimi napinga namna yoyote ya maandamano kwa sababu hata mimi mwaka 2009/2010 nilikuwepo huko NMC Arusha wakati Dokta Slaa ni moto kweli, na nimeshuhudia mwenyewe vyombo vya ulinzi vikitawanya watu kwa mabomu ya machozi na hata kuna vifo vilitokea(hivyo sikushuhudia).

Maandamano yanayosemwa hapo yako karibu sana na vita.

Na ni kwanini tuingie katika vita katika nchi hii aliyotupa Mungu?

Kwa faida gani? CCM ina matatizo lakini nikuhakikishie Hakuna muujiza wa CHADEMA au chama gani sijui.

Hivi kwa mfano Lissu aliposimama na kusema kuwa tutashitakiwa MIGA, kisa ya Hayati Magufuli alikuwa akifanya dhidi ya wawekezaji, na ni kweli wawekezaji walikuwa wanakosea!

Je, nini tafsiri ya hiyo kauli ya Lissu?
Hivi wewe unaweza kumtetea mgeni anayevunja sheria dhidi ya ndugu yako ambaye anataka kumweka katika mstari mgeni anayevunja sheria?

Mbinu zooote za maandamano zimeshatumika, na hazikusaidia, atleast akili ya maridhiano ingeweza kuleta matokeo mazuri.


Kuandamana huko anakodai Lissu ni nini basi?
"kuandamana ni sawa na kuiharibu nyumba uliyoijenga kwa mikono yako ukidhani hasara ni ya Serikali"
Ni vyema ukisema kitu ukielezee kikamilifu au kama hukuelewa uachane nacho.

Lissu aliposema tutafikishwa ICSID kwa kuvunja mikataba kinyume na masharti yake kwa vile tumesaini makubaliano ya kimataifa ya MIGA ulimuelewa? Unaelewa MIGA ni nini?

Pia alishauri cha kufanya ili tusipate adha hiyo tena tukitaka kuvunja mikataba hiyo. Ulielewa?

Unajua kinachoendelea hadi leo kuhusu hiyo mikataba iliyovunjwa?
 
Mabadiliko ni mchakato na matumizi ya mbinu mbalimbali mfano elimu ya uraia kwa watu wote, kuhamasishaTaasisi za dini, Taasisi zisizo za kiserikali, sekta binafsi, Taasisi za umma ili kupata uungwaji mkono. Jambo kubwa ni kujenga ushawishi kuhusu mambo hayo ili kudai mabadiliko ya kweli na inaweza ukawa mchakato endelevu na wa muda mrefu na mikakati yenye mantiki. Siyo tukio la siku moja tu. Matokeo yanaweza kuwa ya siku moja lakini ndani ya mchakato mrefu.
 
Ndio nimeuliza hapo Mkuu, unadhani watanzania wako tayari kunyanyua mguu? If not kuna mpango gani? Lazima uangalie pande zote... na kwa nature ya watanzania mizani inadondokea pabaya
Kama wenye bunduki wanaambiwa kuleni za brashi unafikiri wataweka silaha chini? Haiwezekani
 
Ni vyema ukisema kitu ukielezee kikamilifu au kama hukuelewa uachane nacho.

Lissu aliposema tutafikishwa ICSID kwa kuvunja mikataba kinyume na masharti yake kwa vile tumesaini makubaliano ya kimataifa ya MIGA ulimuelewa? Unaelewa MIGA ni nini?

Pia alishauri cha kufanya ili tusipate adha hiyo tena tukitaka kuvunja mikataba hiyo. Ulielewa?

Unajua kinachoendelea hadi leo kuhusu hiyo mikataba iliyovunjwa?
Kinachoendelea sijui, ila nachojua ni kitu ambacho hata wewe pengine hukijui, ni kuwa hicho unachosikia kinaitwa Makinikia, watanzania walikuwa wanaambiwa jazeni katika makontena huu mchanga tunaenda kutengenezea gololi, kama una experience na migodi utaelewa gololi ni nini?

Je, wao hawakujua kuwa ni makosa kuiba?

Na hakuna mashiko yoyote ya kukingia wawekezaji kifua kwa kusema tutashtakiwa, alitakiwa aanze nao kwanza...
 
Kinachoendelea sijui, ila nachojua ni kitu ambacho hata wewe pengine hukijui, ni kuwa hicho unachosikia kinaitwa Makinikia, watanzania walikuwa wanaambiwa jazeni katika makontena huu mchanga tunaenda kutengenezea gololi, kama una experience na migodi utaelewa gololi ni nini?

Je, wao hawakujua kuwa ni makosa kuiba?

Na hakuna mashiko yoyote ya kukingia wawekezaji kifua kwa kusema tutashtakiwa, alitakiwa aanze nao kwanza...
Aisee.
 
Nashangaa sana hapa huu uzi watu wanatetea maandamano ya Lissu, na wanapinga Magufuli alipoandamana kulinda mali zetu...
 
Ndio nimeuliza hapo Mkuu, unadhani watanzania wako tayari kunyanyua mguu? If not kuna mpango gani? Lazima uangalie pande zote... na kwa nature ya watanzania mizani inadondokea pabaya
Mkuu Lissu sio ideal
Should protests be an only way of demanding right?

Protest is a statement or action expressing disapproval of or objection to something.
And there many ways of protests.
 
Back
Top Bottom