LISSU na Msimamo wa CHADEMA, Je ni Faida au Hasara?

LISSU na Msimamo wa CHADEMA, Je ni Faida au Hasara?

Abuka

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2013
Posts
248
Reaction score
242
IMG-20250212-WA0011.jpg
1. Je, CHADEMA wanaweza kususia uchaguzi, NDIO, wanaweza kama chama lakini kwa sasa wametangaza hawatasusia uchaguzi, kwasababu waliwahi kuona madhara yake. Ukisusa wenzako wala

2. Je, CHADEMA wanaweza kuzuia Uchaguzi? HAPANA hiyo sio kazi yao, mwenye mamlaka ya kutangaza na kuhairisha uchaguzi ni Tume huru ya Uchaguzi pekee.

3. Je, Uchaguzi usipokuwepo, nini kitatokea? Rais aliyepo Madarakani na Makamu wake wa Rais wataendelea kuongoza hadi pale uchaguzi utakapofanyika na viongozi wateule wakaapishwa. Hiyo bado ni hasara kubwa kwa CHADEMA

4. Je CHADEMA wanamaanisha nini kusema hakuna uchaguzi?, wamesema watatangaza Dunia nzima lakini pia watatumia nguvu zao zote kuzuia uchaguzi, maneno ambayo yana viashiria vya fujo, maandamano n.k

5. Je wakitangazia Dunia itafanya nini? Kwa sasa nchi kubwa kama Marekani na Umoja wa Ulaya wametangaza kupitia upya sera zao za mambo ya nje ili pesa ielekee tu kule inapoona kuna tija, hiyo uchaguzi huu tofauti na miaka mingine unaweza usiwe na macho mengi hasa kwa mataifa ambayo hayanufaiki na Tanzania.
 
..kwanini serikali haitaki kuunda Tume Huru ya Uchaguzi?

..kuna faida au hasara gani ikiwa uchaguzi wetu utakuwa huru, wa haki, na unaokubalika?
 
View attachment 32347131. Je, CHADEMA wanaweza kususia uchaguzi, NDIO, wanaweza kama chama lakini kwa sasa wametangaza hawatasusia uchaguzi, kwasababu waliwahi kuona madhara yake. Ukisusa wenzako wala

2. Je, CHADEMA wanaweza kuzuia Uchaguzi? HAPANA hiyo sio kazi yao, mwenye mamlaka ya kutangaza na kuhairisha uchaguzi ni Tume huru ya Uchaguzi pekee.

3. Je, Uchaguzi usipokuwepo, nini kitatokea? Rais aliyepo Madarakani na Makamu wake wa Rais wataendelea kuongoza hadi pale uchaguzi utakapofanyika na viongozi wateule wakaapishwa. Hiyo bado ni hasara kubwa kwa CHADEMA

4. Je CHADEMA wanamaanisha nini kusema hakuna uchaguzi?, wamesema watatangaza Dunia nzima lakini pia watatumia nguvu zao zote kuzuia uchaguzi, maneno ambayo yana viashiria vya fujo, maandamano n.k

5. Je wakitangazia Dunia itafanya nini? Kwa sasa nchi kubwa kama Marekani na Umoja wa Ulaya wametangaza kupitia upya sera zao za mambo ya nje ili pesa ielekee tu kule inapoona kuna tija, hiyo uchaguzi huu tofauti na miaka mingine unaweza usiwe na macho mengi hasa kwa mataifa ambayo hayanufaiki na Tanzania.
ni kupoteza muda na kujipoteza wenyewe bila kujihurumia kwa watakaomfuata huyo kibaraka wa mabwenyenye ya magharibi 🐒
 
Kujaribu kuzuia nchi kufanya uchaguzi ni kitendo cha kuvunja sheria, baada ya muda tutakuwa tunafungua nyuzi za kusema Lissu sio gaidi🐼
 
Back
Top Bottom