kuna vitu vya kuzingatia kabla hujaanza hiyo safari yenyewe...
kama piki piki sio mpya.
✓jiandae kuongeza mafuta full tank mara 3 hadi mwisho wa safari yako.
✓hakikisha una weka break mpya zote 2.
✓kagua waya ya break pamoja na cable ya clutch.
✓kaza vizuri nuts zote.
✓weka oil mpya best recommend Mogas ukiweza ongeza mls200 za oil kwa kawaida chupa ya oil huwa na ujazo wa lita 1. hivyo utaongeza kidogo mils 200.
✓jitahidi upate gloves [emoji3451]....
✓tafuta mzura au koti lenye kofia ambayo itasaidia kuibana helmet.
✓vaa suluali 2 au 3.
✓ukiweza kupata mabuti marefu yatakayo kuwezesha kuibana suluali miguuni itakuwa poua sana maana njiani kuna upepo wenye baridi kari mno. hali ya hewa huanza kubadilika ukifika Chalinze.
✓usibebe begi kama ukilazimika kulibeba hakikisha unalifunga nyuma.
✓beba oil ya akiba. kama ni mziefu wa kuendesha piki piki utakuwa unajua mlio wa pikipiki endapo oil itakuwa imeisha nguvu. japo kitaalam km1700 Hizo unaweza kwenda bila kuchange oil.
✓hakikisha unatembea na spana za muhimu kama hiyo ya Oil pamoja na za kuajustia break.
✓mipira ya pikipiki isiwe imetumika sana ikiwa mipya itapendeza zaidi maana njia unayoenda kupita ina viwaya vilivyoachwa na matairi ya magari makubwa hivyo kama tairi likiwa limeisha ni rahisi kupata pancha.
✓usisahau kubeba lita wau 2 au ukiweza 5 za petrol za emergency. hizi zitakusaidia endapo utaishiwa mafuta sehemu ambayo haina Petrol stations. hakikisha unafika nayo mwisho wa safari.
✓changamoto utakayo kutana nayo kubwa ni madereva wanaoenda mwendo wa haraka hawawathamini waendesha pikipiki hivyo ni bora ukawasha taa muda wote uwapo safarini.
✓usiendeshe mwendo mkari kupita kiasi barabara zetu zina mashimo. na mashimo mengine ni makubwa kiasi cha kufanya tairi izame hivyo ukiwa kwenye speed kali utashindwa kulikwepa hilo shimo. best recommend speed 70 kushuka chini...! usivuke 80 barabara zetu haziruhusu.
nakutakia safari njema
najua nimechelewa ila kwa faida ya wengine na watakaohitaji elimu,
kwa safari za masafa marefu, vitu muhimu ni pamoja na
✓aongeze plug spana na plug ya ziada, akiwa ni mpiga ruti za usiku pia akumbuke bulb na angalau screw driver.
✓uwe na sclaf au kitambaa cha kufunga koti na shingo maana kuna upepo mkali ukivuka speed 100
✓tumia side mirrors usigeuze shingo, ni rahisi kupoteza barabara ukajikuta mtaroni hususani ukiwa mwendo mkubwa, zingatia. cheki nyuma kabla hujakipita chombo chochote
✓usiingie ligi na gari au pikipiki nyenzako. zingatia uwezo wa injini na uzoefu wa dereva unatofautiana sanjari na kuijua barabara
✓usijiamini kwa kuzingatia sheria za barabarani (mf. kutompisha wa semi/basi eti kisa tu uko kwenye right lane-upande sahihi/waswahili tumezoa mkono wako. akikupiga taa ta tahadhari, usiwe mbishi, punguza mwendo tenga pembeni apite maanq kuna kuachiwa mkia/treila ikakumaliza ama upepo tu unatosha kukuhamisha
✓ukichoka ukaanza kuhisi usingizi, pumzika, oga au push-ups na kichurachura, nawa uso na jimwagie maji kichwani dk 10 endelea na safari. hali ikizidi lala kabisa uisubiri siku inayofuata.
*uzoefu wa miaka 20 kwa pikipiki