Live Updates: MO Bejaia FC vs Yanga SC at Unite Maghrebine Stadium!

Live Updates: MO Bejaia FC vs Yanga SC at Unite Maghrebine Stadium!

Wakija taifa hawa maboya ni bora game ipigwe saa8 mchana.
Itawasaidia wao maana kule joto kali kuliko hapa
View attachment 358130 View attachment 358014 View attachment 358015

Wadau wote tukutane hapa kupeana udambwi dambwi wa mechi ya leo usiku.
Kwanza tutangulize dua zetu kwa wawakirishi hawa wa Africa Mashariki.
Mungu Ibariki Yanga, Mungu Ibariki Tanzania......
=================================

FT: MO Bejaia 1-0 Yanga SC

=========

KIKOSI CHA YANGA LEO.
KIKOSI:
1: Deo Dida
2: Mbuyu Twite
3: Oscar Joshua
4: Kelvin Yondani
5: Vicent Bossou
6: Thabani Kamusoko
7: Simon Msuva
8: Harouna Niyonzima
9: Donald Ngoma
10: Hamic Tambwe
11: Deus Kaseke
BENCHI:
- Ally Bathez
- Mwinyi Ngwali
- Pato Ngonyani
- Antony Matheo
- Juma Makapu
- Godfrey Mwashiu

========
Dakika 90 za mchezo wa kwanza kwa Yanga hatua ya makundi ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika zimemalizika.

MO Bejaia 1 - 0 Yanga SC

90+1′ Mwinyi Haji anaoneshwa kadi nyekundu baada ya kumchezea vibaya mchezaji wa MO Bejaia

Zimeongezwa dakika 4 za nyongeza baada ya dakika 90 kumalizika

86′ Yanga wanafanya mabadiliko, anatoka Amis Tambwe nafasi yake inachukuliwa na Matheo Anthony

> wakati huohuo MO Bejaia wanafanya mabadiliko pia

78′ MO Bejaia wanafanya mabadiliko kwa mara nyingine tena

76′ Geofrey Mwashiuya anapoteza nafasi ya wazi kuisawazishia Yanga

72′ MO Bejaia wanafanya mabadiliko, anatoka mfungaji wa goli Yassin Salh

69′ Kipindi cha pili kinaendelea MO Bejaia bado wanaongoza kwa bao 1-0 (MO Bejaia 1-0 Yanga)

62′ Yanga sasa wanashambulia kwa nguvu…Wanajenga vizuri mashambulizi yao na timu inaonekana ina muunganiko mzuri. . Kona ya pili mfululizo Yanga wanapata inapigwa kona ile lakini walinzi wa Mo Bejaia wanaokoa. Ngoma, Ngoma anatokea mlinzi wa Bejaia anaosha mpira unarudishwa tena langoni mwa Bejaia Msuva. Msuva anawekwa chini na Hadhiri mpira ni faulo mlinzi wa Bejaia analimwa kadi ya njano. Faulo inapigwa na Mwinyi mpira unatoka nje.

Bejaia 1 – Yanga 0.

Kipindi cha pili kimeanza. Bado MO Bejaia wanaongoza, Bejaia 1 – Yanga 0.

Mpira ni mapumziko mechi ya hatua ya makundi kati ya MO Bejaia dhidi ya Yanga, MO Bejaia 1-0 yanga

45′ Zinaongezwa dakika mbili kabla ya kipindi cha kwanza kumalizika na timu kwenda mapumziko, MO Bejaia 1-0 Yanga

42′ MO Bejaia wanapata mpira wa adhabu, unaopigwa na Sufian lakini unaokolewa na mabeki wa Yanga

41′ Yanga wanapata kona fupi…Niyonzima anamuanzaia Msuva

Msuva anatumbukiza krosi kwenye lango la MO Bejaia lakini Ngoma yuko kwenye eneo la kuotea

32′ Haji Mwinyi anaingia kuchukua nafasi ya Oscar Joshua ambaye ameumia na kushindwa kuendelea na mchezo

Bejaia 1-0 Yanga

Goli la Mo Bejaia Yassin limefungwa na Yassin Salh

20′ Yassin anaiandikia MO Bejaia goli la kwanza baada ya walinzi wa Yanga kuchelewa kuondoa mpira uliokuwa unazagaa langoni mwao. MO Bejaia 1 – 0 Young Africans

14′ Deo Munishi ‘Dida’ anafanya kazi ya ziada nyingine baada ya kuokoa mchomo mkali…MO Bejaia wameanza mchezo huu kwa kasi kubwa kujaribu kupata goli la mapema! Yanga wanajibu mashambulizi kwa mahesabu zaidi ili kumiliki presha hii. MO Bejaia 0 – Yanga Afrika 0

9′ Donald Ngoma anafanyiwa madhambi na Mlinzi wa MO Bejaia. Mpira ni faulo anaenda kupiga Haruna Niyonzima. . Anarudi nyuma moja mbili taaaaatu anapiga kula lakini mpira unawababatiza safu ya ulinzi ya Bejaia. MO Bejaia 0 – 0 Yanga

Dk 5. MO Bejaia 0 – 0 Young Africans. Mpira ni goal kick unapigwa kuelekea lango la Mo Bejaia
 
Yanga mmepigwa.. Msitafute mchawi.. Mbwembwe za mazoezini zilkuwa nyingi kuliko maandaliz halisi.
Life is not a rehearsal but a real performance and good outcome.....US Baby[emoji482]

Magazeti yenu yalisema WAARABU WANATETEMEKA kwa mazoezi ya Yanga.
Nasubiri leo yatasemaje.....[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Yanga mmevuruga hedhi ya FaizaFoxy
Nimeona gazeti moja lina kichwa cha habari "Yanga kampa kampa tena Mwarabu"
 
Leo mji umetulia sana. Kunani?

Nasikia kuna mtu anasema Mwarabu na Yanga ni sawa na mme na mke.... kwani kimetokea nini mkuu??
ukiolewa shariti ulale uchi yanga kaolewa hataki kulala uchi hiyo inawezekana wapi...kapigwa kimoja subiri TP mazembr
 
Waendelee kukaa ulaya tena halafu wakirudi wapigwe tena
 
Pia watani zangu wawe makini hizi ni mechi za makundi kwa maana kinachoangaliwa ni point na sio wingi wa magoli......kwa matokeo hayo waliyopata huko uarabuni hawana budi kushinda mechi ijayo dhidi ya TP MAZEMBE hapa nyumbani....na yote inawezekana kama watautaka ushindi kwa kujituma na kutumia nafasi chache zitakazo patikana ndio msingi wa ushindi....
Nina amini kama watani zangu watajianda vizuri kwa ajili ya mchezo ujao hapa nyumban wanaweza wakashinda bao nyingi na kujihakikishia kuendelea kuwepo mashindanoni......

Lazima watanzania tuipe sapoti Yanga kwani yeye ndio muakilishi pekee wa taifa letu huko kimataifa....analitangaza jina la Tanzania.....hata mtangazaji utamsikia Yanga from Tanzania hawezi kusema from Jangwani.....kwa maana waliopo ni zaidi ya wana Jangwani......

NB;
UZALENDO KWANZA....kuichukia Yanga na kuiombea mabaya Yanga hakutusaidii chochote sisi wanamsimbazi zaidi ya kudharaulika mbele ya wageni na kuupoteza muda ambao pengine tungeutumia kuangalia madhaifu ya timu na kuyafanyia kazi ili kufanya vizuri kwenye ligi na mashindano mbali mbali msimu ujao.....
 
Pia watani zangu wawe makini hizi ni mechi za makundi kwa maana kinachoangaliwa ni point na sio wingi wa magoli......kwa matokeo hayo waliyopata huko uarabuni hawana budi kushinda mechi ijayo dhidi ya TP MAZEMBE hapa nyumbani....na yote inawezekana kama watautaka ushindi kwa kujituma na kutumia nafasi chache zitakazo patikana ndio msingi wa ushindi....
Nina amini kama watani zangu watajianda vizuri kwa ajili ya mchezo ujao hapa nyumban wanaweza wakashinda bao nyingi na kujihakikishia kuendelea kuwepo mashindanoni......

Lazima watanzania tuipe sapoti Yanga kwani yeye ndio muakilishi pekee wa taifa letu huko kimataifa....analitangaza jina la Tanzania.....hata mtangazaji utamsikia Yanga from Tanzania hawezi kusema from Jangwani.....kwa maana waliopo ni zaidi ya wana Jangwani......

NB;
UZALENDO KWANZA....kuichukia Yanga na kuiombea mabaya Yanga hakutusaidii chochote sisi wanamsimbazi zaidi ya kudharaulika mbele ya wageni na kuupoteza muda ambao pengine tungeutumia kuangalia madhaifu ya timu na kuyafanyia kazi ili kufanya vizuri kwenye ligi na mashindano mbali mbali msimu ujao.....
Uzalendo aliondoka nao Mwl. Nyerere wengine wasanii tu...
 
Bora wamefungwa ,,hakuna na kambi ya uturuk wala ugiriki,,na bado TP MAZEMBE wanakuja kujichukulia point,,hahhhha eti ndo wakimataifa yaan mnachoambuliaga sanasana kupanda ndege tuu na kushiriki mashindano na co kushindana...
 
Back
Top Bottom