Live Updates: SIMBA Sports Club vs TP Mazembe

Live Updates: SIMBA Sports Club vs TP Mazembe

wabongo tuna tatizo moja, tunadhani Simba alipofikia na kupapongzwa na kuandika vichwa vya habari eti "Simba yafa Kiume" huu ni upuuzi ambao tunao miaka nenda rudi, juzijuzi kuna mdau mmoja wa Simba (sijui kama ni mdau kweli wa wa kibiashara) anaitwa Azim Dewji alikua akilaani simba kukataliwa ombi lao la kuhairishiwa mechi na kagera sugar, akaenda mwali na kusema simba na yanga bila wao TFF haipo. Huyu mtu aliuza mechi ya fainali ya Stella na Simba baada ya kuona atatakiwa kutoa KIA kwa timu nzima, leo hii anajidai anamchungu na kuipenda club na sisi mashabiki tunamshadadia, hii sio sawa. Soka la bongo haliwezi kukuzwa na simba na yanga pekee, Dewji alipaswa na anapaswa kupuuzwa, soka letu linahitaji kuangaliwa kwa mapana yake...tutabakia na heading za kujipa matumaini but hamna kitu tunaangamia, toka enzi ya mwinyi tulikua kichwa cha mwenda wazimui na tutabaki kuwa hivyo mapaka pale tukakapo amua club haziwexi songa mbele kwa kutegemea friends of simba, Dewji, Gulamali (R.I.P), bakhresa, manji na wengineo. Soka inatakiwa kufikiriwa beyond that, tatizo letu tunaruhusu club zitawaliwe na wanachama ambao hawana maono ya wapi wanataka kwenda na ndo maana simba kumfunga yanga au yanga kumfunga simba ni Big deal, hatutafika hata kidogo, soka ni biashara na asiyejua aangalie mataifa ya watu, tutaishia kusema brain washed but the truth is there
unajua mechi ya AFC na Mtibwa ilipata kiasi gani kama walifikisha 200,000 nitashangaa...angalia mechi ya AFC na Simba walipata mil ngapi kama ni chini ya TZS 20,000,000 nitashangaa...hicho ndicho alicho kuwa anaimanisha Dewji..
 
Hivi hiyo Nguvu kubwa iliyowekwa ktk mechi moja tu dhidi ya TP Mazembe tena yenye ahadi za mamilioni ya pesa kwanini wasiwekeze kwenye kuiandaa timu????

Watanzania ni watu wa kupenda sana shortcut. Na kamwe hatutafanikiwa kwa hiyo njia
 
Jumamosi nilituma post hapa hapa, nikasema lazima mnyama angechinjwa na Kaluyituka...........ndivyo ilivyokuwa! Tatizo ni maandalizi! Sikuwa na nia mbaya ila jinsi magazeti na 'wadau' mbalimbali wa mpira walivyoi-under rate TP Mazembe badala kuhamasisha maandalizi, hata kama Simba ilicheza vizuri, mwisho wa siku mpira ni magoli na si porojo! Kama walivyosema wengine, nami naungana nao kuwapa pole watani zetu wa jadi! Msijali, mwakani si mtatuwakilisha tena kwenye michuano ya kimataifa! Anzeni maandalizi sasa, maana mnaweza kupangiwa tena mabingwa watetezi!
 
Hawa maembeee waliharibu kabisa wikiendi yangu....
Invizibo hebu watwange ban hawa wanaoendelea kuiharibu....
 
Lol............
 

Attachments

  • 200515_215270141821424_100000153207127_1005878_2719420_n.jpg
    200515_215270141821424_100000153207127_1005878_2719420_n.jpg
    15.2 KB · Views: 68
Huu sio uzalendo aisee....

Ni kweli si uzalendo...........hivi ni vijimambo tu vya utani wa jadi babu...........Usichukulie serious kiviiiile

Kwani TPM si kampakata Simba jana?
 
Ni kweli si uzalendo...........hivi ni vijimambo tu vya utani wa jadi babu...........Usichukulie serious kiviiiile

Kwani TPM si kampakata Simba jana?

Infakti naandaa muswada wa kuifungia ile pub....!
 
Ila na majina ya timu jamani yanatisha, mtu kabla ya kuingia uwanjani unahisi umeshafungwa. we timu inaitwa TOUT POUISANT MAZEMBE ENGLEBERT utatoka kweli?
 
lakini jamani si michezo tu sisi Wabongo tumezigi majigambo na maneno mengiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii vitendo 0.5% halafu mwisho wa siku tunatafuta mchawi au mamluki.
 
Hivi hiyo Nguvu kubwa iliyowekwa ktk mechi moja tu dhidi ya TP Mazembe tena yenye ahadi za mamilioni ya pesa kwanini wasiwekeze kwenye kuiandaa timu????

Watanzania ni watu wa kupenda sana shortcut. Na kamwe hatutafanikiwa kwa hiyo njia
Si kwamba Simba hatukujiandaa, tulijiandaa kadiri ya uwezo wetu na kwa aina ya timu na wachezaji tuliokuwa nao. Tunajua kuwa ni kazi ngumu kuitoa mashindanoni timu kama ile, lakini si vibaya kujaribu kama tulivyojaribu, hizi porojo za akina nanihii ni mambo yanayotawala vijiweni na kwa vile mpira wetu unaendeshwa kutokea vijiweni, porojo ni kitu cha kawaida sana.

Kwa hiyo ukiangalia hata wale anti-Simba wanavyotoa comments zao humu, ni muendelezo tu wa porojo zilizojaa katika mfumo wa uendeshaji wa timu zao. Mazembe wametusaidia kujijua tulipo na namna gani tutoke hapo na kusonga mbele, kwa watani wamewasaidia kujisahau na kuendeleza porojo, shangaa jinsi walivyonunua jezi ya mazembe kuliko hata wanavyonunua bidhaa za club yao,hiyo yote ni porojo tu kwa vile wangeweza kuishangilia Mazembe hata kwa kuvaa jezi yao na kuinunua kwa wingi.
 
Back
Top Bottom