Liverpool 4-0 Man United, Gary Neville asema "Sijawahi kuiona Man United mbovu kama hii ya sasa"

Liverpool 4-0 Man United, Gary Neville asema "Sijawahi kuiona Man United mbovu kama hii ya sasa"

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
FQuv9uvXIAI30GC.jpg

FQuv9XtXoAQ8y_F.jpg
Mabao ya Luis Diaz katika dakika ya 5, Mohamed Salah (22 na 86) na Sadio Mane (68) yameipa ushindi #Liverpool dhidi ya Manchester United katika Premier League kwenye Uwanja wa Anfield.

Nahodha wa zamani wa United, Gary Neville wakati mchezo ukiendelea alinukuliwa akisema: “Nimeiangalia United kwa miaka 42, sijawahi kuona timu mbovu kama hii ya sasa.”

Katika mchezo huo ilipofika dakika ya 7, mashabiki wa #ManUnited na Liverpool waliungana na kusimama kwa dakika moja kutuma salamu za rambirambi kwa Cristiano #Ronaldo wa Man United aliyefiwa na mtoto wake wa kiume wakati mpenzi wake akijifungua.

Kwa matokeo hayo sasa Liverpool anashika usukani wa Premier League akiwa na pointi 76 katika michezo 32, Man City ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 74 ikiwa na michezo 31.


Picha: Premier League
 
Wachue wachezaji wa timu B wamalizie michezo iliyobaki ili kupunguza aibu
 
tatizo wachezaji waliopo wengine hawastahili kuwa pale hii nd sababu kubwa ya kukosa matokeo ni sawa na baba haujui umuhimu wake ndani ya nyumba kila siku mtakuwa mnalala giza
 
Kocha wa makocha anageuzwa geuzwa na wanafunzi wake bila kujitetea,hii timu ivunjwe,mechi zilizobaki wamalizie timu B,kupigania nafasi ya nne ....ili Tenhag akija acheze uefa
 
Back
Top Bottom