Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Screenshot_20240826_191527.jpg



YNWA
 
Klopp na ka cult club kake ka miujiza huku henderson
Huku milner huku trent humwambii mtu yule babu.
Klopp bwana klopp 😂😂 klopp alkua mhuni sana yule mzee anakupump unaamini wewe duniani hamna kama wewe
Ref to Gini haya akahama 😂😂
Na mwingine mnamjua nyie

Klopp alikua ana believe kwenye miracles funny football... fantasies

Na it was funny watching klopp era mimi alifanya ni believe everything ni possible

Huyu slot tumpe muda

Asiporudi kwenye mambo ya cult ya klopp tutaona 😂😂
Binafsi niliona baada ya kutua Klopp tulikua bora kileleni kwa kulinganisha ta ulipokua especially enzi ya Fergie yupo moto fire yaaani kwa Klopp kutua na tukawa hatuchezi mbali na ubingwa aa the feeling was good at least... Ishu tu FSG hawakujua how lucky kua na yule Kocha klabuni kwani Klopp ni Mwalimu ni brand pia yupo muliti talented..
Hawa ma cult heroes wa Klopp ilikua wanatembelea nyota ya wengine.. Ukihitaji kutaja wachezaji wenye bahati duniani lazima Henderson awe wa kwanza.

YNWA
 
Slotball.

Brentford walijaribu sana kutushambulia but we were combact enough hawakuwa na madhara sana.

Ubora wa Alisson, Ibou, Vvd, Gravern, pass makini za Trent, Runs za Szobo, ziliwafungua Brent, vizuri tu. Magoli mazuri, la kwanza counter, la pili flowing move, good timing, good decisions kwenye magoli yote.

Mimi ni muumini wa double pivot, sana kwa sababu inasadia kutunza energy ya kiungo wako no. 6 na kuwa na watu wawili katikati.

Bado wachezaji wanahangaika na system ya Slot ila pole pole inawaingia.

Vvd na Ibou waliwin aerial duels nyingi sana, 2nd balls tuliziwin nyingi sana. Ikarahisisha maisha ya timu kwa ujumla wake.

Mtu naona tunahitaji mbadala wake ni Robertons ule upande wake upo very weak ukianza na yeye mwenyewe, ana struggle sana. Robbo alishamaliza mpira ma LFC since 2022/2023, injuries ya za last season zimemmaliza. He is not the same.

Uzuri sasa hivi kila mtu anatekeleza wajibu wake, hakuna mtu kuhangaika na jukumu la mtu.

Slot naona anavyomtumia Trent huenda tukamfaidia sana offensively na defensively kwa sababu hamtumii kuingia ndani zaidi anamuacha akae pembeni, zaidi which is good hata mkishambuliwa space inakuwa ndogo.

Slot sio attack attack coach kuna muda anacotrol mchezo with less intensity ili ku save energy ya wachezaji wake na kupunguza Spaces, kupunguza makosa yatokanayo na counter za opponents. Which is good thing, kuna muda ni bora kulinda moja ulilopata kuliko kuhangaikia mengine ambayo pengine unaweza kukosa.

Kuna njia nyingi za ku defense na moja wapo ni possession with low intensity, less counter, stay focused kwenye patterns, na combination plays.

Combination play ni mchanganyiko wa patterns na namna ya kucheza kuna muda inakuwa diamond, triangle, rectangular, passing through players, individual dribbling n.k hii inasaidia kumchanganya mpizani wako asijua unatumia nini.

Kuna muda Salah alikuwa anagonga 1.2 anaondoka, kuna muda Trent aliingia katikati, na 1,2 yeye na Szobo, kuna muda through dribbling, kuna muda tulikuwa, 4–2-4 kwenye kukaba, kuna muda 4-4-2 kwenye kuzuia. Baada ya goli la pilia tukapiga Slot ball with flowing movements waohh, just waooh..!!!

It’s a second match, binafsi gari la Slot nilishapanda muda tu, mengine mambo ya pira.

Gravern kwenye no. 6 anaicheza vizuri mno, mno, weakness yake ni tackling kama ile aliyoifanya jana unaona he is not expert kwenye mambo hayo akaishia kupata njano. Bradley, Konate hawa ndio wataalamu wa Tackling pale LFC, timing yao nzuri sana. View attachment 3079796
Namba nzuri kwa mtu ambaye sio natural 6.

View attachment 3079805
Tukio lililoshika hatamu mechi ya jana. Nilipenda Slot alivyomfuata jana Trent baada ya kuonesha kutoridhishwa na kufanyiwa sub dk zile, Na hata alivyolijibu swali hilo kuhusu tukio lile.


Trent he is a world class player, kikubwa akubaliane na hali, na aendelee kupiga kazi, Anfield inamkubali sana na LFC inamtegemea kwenye ubora wake, (quality passes, long and shot passes, long and short ranges). Kipimo kizuri ni next match vs Utd at OT.

Its too early ila tuna enjoy every moment we have under Slotball. He might be our Bob Paisley

Best luck to us
Up reds
YNWA
Lastborn wa Klopp
Bebe wangu Trent
Anune apasuke
slot shikilia hapohapo
Hakuna kubembeleza mtu 😂😂😂😂
Yaani kavuruge halafu kasitolewe

Slot baba kipara
We wakizingua
Weka bench
Hakuna mwenye hatimiliki ya namba

Pale lastborn wanaenda kuwa watoto wa kambo😂
 
Watu wanamlaumu Slot kwamba yupo harsh. Ila kutumia akili yake ya kawaida kuona kama ni kweli au la ni ngumu.

Slot alisema “Quansah hakuwa vizuri kipindi cha kwanza, alikosa aerial duels nyingi” je ni kweli au uongo?? Jibu ni kweli.
Wengi wamekaa na Klopp muda mrefu hawajawahi kuona Klopp akisema hivyo, ndio maana wanaona jamaa yupo harsh.

Ilikuwa rahisi Klopp kukaa ni kina Henderson, Milner, Keita, Thiago, Ox, Matip licha ya kuwa na viwango visivyoridhisha na wengine kuwa majeruhi wa kudumu. Mchezaji akikosea Klopp alizidi kumpa game time ili ajirekebishe kitu ambacho ukiwa kama Manager sio kizuri.

Slot ana namna yake ya kufundisha na kuhudumia wachezaji, yes anahitaji mchezaji awe attention muda wote wa mchezo, asipoteze umakini, which is somethimg good.
Slot kanyaga twende😂😂😂😂
 
Slot Stat.... No wonder ma Yankees wanatulia tuli.

Liverpool vs Brentford tulikamlisha pasi asilimia 92 ikiwa na rekodi mpya kwetu. Mara ya mwisho kukamilisha pasi kama vile ilikua msimu wa 2003/04.

Liverpool vs Ipswich vijana wa Slot wameweka rekodi kwa 'kugusa' mpira mara 50 ndani ya box ya Ipswich ikiwa na rekodi kwa kocha mpya gemu ya kwanza EPL.

Mashabiki 60,107 walihudhuria gemu ya Liverpool vs Brentford ikiwa ni rekodi mpya kwa uwanja wa Anfield gemu ya league.

YNWA
 
Ninaamini tuna Scouting Department bora zaidi barani Ulaya kwa sababu.

1.Huwezi kuwa na scouting team mbovu ukasajili wachezaji 10 na katika yao 9 wakawa successful.

2.Huwezi kuwa na scouting mbovu ukasajili wachezaji ambao bei zao ni almost nusu ya bei za soko na wakakupa kiwango zaidi ya wale walionunuliwa kwa bei kubwa.

Tuna scouting team bora sana Ulaya ndo maana tumekuwa very successful sokoni kwa zaidi ya 90%.

Tujiulize 🤔

1.Scouts waliomuona Robo unasemaje wabovu??

2.Scouts waliomuona Salah wanakuwaje hawajui

3.Scouts waliomuona Sobo au Macca wanakuwaje wabovu??

4.Scouts waliomsajili Tsimikas wanamuwaje wabovu?

5.Scouts waliomuona Slot over all big name coaches wanakuwaje hawajui kazi??

6.Scouts waliomwambia Klopp asubiri deal la VVD na si beki mwingine, wanakuwaje wabovu??

7.Nani alimjua Jota tunayemsifia kama aiyo hao scouts ambao hawajui??

8.Scouts hawa waliomuona Konate over all big names defenders??

9.Scouts hawa waliochungulia kipaji cha Bajcetic kule Spain akiwa ni beki wa kati akaja kubadilishwa kuwa kiungo, hawa waliomuona Elliot pale Fulham, leo ni mmoja wa wachezaji bora vijana Uingereza.

Scouts ambao so far wanaifanya Liverpool kupata quality ya kushindana kwenye ligi na timu tajiri zikiwa zimenunua kwa bei ghali lkn tumekuwa kwenye ushindani kwa miaka 10 mfululizo.
 
Wana Liverpool wenzangu
Mimi nakubaliana na sera za timu yetu kwenye usajili, lakini ninachopingana nacho kwenye kuchelewa kumaliza deals. Wana nyatia sana na kubembeleza sana bei.

Wishes za mashabiki ni kuona timu inasajili sana, lakini tunaona watu wanavyofeli sokoni kwa sajili za kukurupuka. (Manchester utd, Chelsea) Hiyo ni mifano.
 
Back
Top Bottom