Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Hata vvd ana yake pale,. Je baada ya pale tulishinda mechi zilizobaki au sare,?
VVD ameingiaje hapa wakati tunaongelea golikipa kuacha goli na kwenda kushangaa katikati ya uwanja.

Zilizobaki za nini?
Tuanzie na hii ya Aseno
Kwanini aliachia?
 
Ameandika George Ambangile


TRENT ALEXANDER ARNOLD AS A CREATOR ( Mpishi )

✍🏻Trent Alexander Arnold kwa mashabiki wa kandanda huyu sio mgeni kwenu na aina ya soka lake lakini kwangu mimi kila siku anazidi kutanua upeo wangu wa kutazama soka tofauti .

✍🏻Kuna kipindi baadhi ya mashabiki na wengine pia kutoka Liverpool walikuwa wanatamani TAA kucheza eneo la kiungo kwasababu tu ya " Passing game " yake kiasi kwamba hata Southgate alijaribu mara moja

✍🏻Lakini uhatari wa TAA unatofautiana akiwa kwenye kiungo na akiwa beki wa kulia . Utofauti ni nini hapo ?

✍🏻Soma hapa : kuna tofauti kubwa sana baina ya " KUANZIA " eneo husika na " KUFIKA " eneo husika , yani :-

1: TAA akianzia eneo la kiungo moja kwa moja kuna sehemu unadunisha sana uhatari wake , maana kuna nyakati zipo atalazimika kupokea mpira goli kalipa mgongo , na pia hilo eneo mara chache huwa linakosa watu wengi ( kwahiyo space ni ndogo mno mara nyingi kuliko mara chache )

2: TAA akiwa anafika eneo la kiungo yani anatokea kulia halafu anazidi kusogea juu kwenye kiungo : iwe pembeni juu kulia , kwenye half space kulia , au hata katikati ya kiungo kabisa . Hapo anakuwa hatari zaidi , anauona uwanja vizuri mbele yake , na hata wapinzani wanakuwa mbali naye kwa distance fulani .

" Let TAA arrive there and not start in the midfield "
 
Kuna kipindi mkamdis sana humu
Eti Quansah mzuri kuliko Trent

Nani atafunga mabao katikati ya uwanja kama Trent?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…