Mkuu leta basi hizo polls nyingine tulinganishe. Mimi nimegoogle poll 1 na link 1; sasa leta basi hata poll 1 na link zinazoonyesha Gerrard ni bora kuliko Scholes.
Asante Mkuu Malafyale. You always keep our thread a live. Much respect to you Bro!!
Nimekaribia kiongozi. Inafurahisha kuona jinsi wanalivepool walivyo wajuzi na ufahamu wa kina kuhusu timu yao na mchezo wa mpira kwa ujumla.
Jukwaa letu halichoshi
...Janjaweed, Tish-TOTO, Tee Bag, mak89, Kingmairo, MartinDavid, nyangelekene, TheMagnificent,Ed n Edd nEddy, Plesis, Kassid mtunzi, delako, Blac kid, nguvu, stormryder, Tores and the rest...heshima kwenu!!
Sababu ya SG kamfanya HENDO aende WC na the average Carrick abaki!Bila SG una amini Hendo angechaguliwa mbele ya akina Carrick kwenda WC?
Jamaa wewe bana!
Bao tu walizofunga team ya Taifa zinamdhalilisha Scholes
Games ambazo kaibeba Uingereza zinamdhalilisha Scholes
Mkuu ukiacha EPL titles HAMNA KINGINE chochote ambacho SCHOLES anamzidi SG!Hata O'shea ana EPL titles nyingi zaidi ya SG
Doh! Wewe kweli mkali....sasa unataka kumlinganisha huyo Henderson "who runs on from his knees, with a straight back" badala ya kukimbia from his hips, na Michael Carrick?!
Naamini unanogesha jukwaa...
Carrick alimiss WC kutokana na msimu mbovu wa United chini ya DM, Liverpool ikawa na msimu 1 mzuri chini ya Suarez na Stoolie...
Ila kama unaona Henderson alivyo sasa ndiyo kabadilishwa na SG, doh, basi kazi ipo!
Nauliza tena, mbona SG kashindwa kumfanya Henderson kuwa Alonso mpya kama SG ndiye 'aliyemtengeneza' Xabi Alonso?
Jamani kila lenye mwanzo lina mwisho,SG alipofikia sasa hivi anapaswa kuondoka maana msaada wake ni mdogo mno na zaidi anasaidia timu pinzani zitufunge!!!!
Kama msimu ulipita ndo mtu aliyetengeneza mazingira tukakosa ubingwa.....
SG JUST GO GO,,,,,,,,
Kopite????????
so 2010 alivyoitwa Kwenye kikos cha ENG kule South aligusa hata Nyasi za South Africa???
Dah! and i cant believe we're even discussing about Michael carrick Aisee..*Very Average player*
Ndo kama mimi nianze kuwapigia watu makelele kuhusu Lucas Leiva!!!!!
Ni ukweli usiopingika kuwa Gerad amekuwa mchezaji muhimu sana wa liverpool kipindi chote alichochezea.
Bado ni mchezaji muhimu lakini ambaye kwa sasa anatakiwa kuwa well managed ili kuhimili vishindo vya ligi ngumu kama epl na aendelee kuwa potential kwenye timu.Tumeona wachezaji wengi ambao baada ya kufika stage kama ya SG makocha wao aidha huwapunguzia mechi au kuwapunguzia majukumu au yote mawili kwa pamoja.Sijaona kama BR kumpunguzia mechi SG amefanya kitu cha ajabu sana.Hata wanajamvi humu baadhi walikiri kuwa timu imekuwa slow this season mara nyingi SG alipokuwepo
Kwahiyo kwakweli SG angekubaliana tu na situation kwa ajili ya timu yake.
Sikutegemea hiyo ndp iwe sababu kubwa ya yeye kuondoka liverpool.Ningemuunga mkono sana kama angeenda chelsea au man city ili ajihakikishie epl ndani ya misimu miwili,yaani kama sio huu basi ujao.
Kumpaisha SG kwa kumshusha Alonso au kumpaisha Alonso kwa kumshusha SG ni kitu nisichokubaliana nacho. Hiyo ligi kati ya SG na Scholes nani zaidi naendelea kuwasoma wachambuzi.
Nisamehe kwa kukurupa...
Nielimishe mkuu wangu kilichoisibu LFC mwaka 2009/10..
MESSi is Barcelona..
Mfano mdogo tu ni kwamba Iniesta na xavi wanaweza kuondoka na mapengo yao yakazibwa kirahisi na tusione tofauti sana!
Lakini MESSI akiondoka Barca, team lazima I-struggle sana, utamreplace MESSI na nan??
Kwenye soccer kuna team work, but kuna baadhi ya Clubs zinakuwa na mchezaj ambaye TEAM inamwangalia yeye kwa kila kitu..
Team Work ipo, lakin tunapozungumzia kizazi cha Barca hii Na mafanikio yake, Huwa tunamzungumzia MESSI zaid (his goals, passion, skills, his special talent) ndo vimeiweka barca ilipo sasa!
Team haibebwi na MTU mmoja, lakin tunaangalia MCHANGO na HESHIMA ambao mchezaji mmoja ameleta kwa club..Na KUTOKUWEPO kwake kunaiua vipi TEAM..
Sijajua umemaanisha nini! Naanza kupata wasiwasi wa uwezo wako wa kusoma mambo! Maana mwanzoni uliweka link ambayo hukuwa umeisoma. Sasa hujasoma na kuelewa post yangu!
Aisee, wewe kweli ni mkali...hivi ni nani aliyeanza kumwongelea pass master (kwenye passing Carrick is better than Gerrard, nasubiri mbishe) Michael Carrick?
Hivi wewe mtu unakumbuka hata post yako ya kwanza kuandika juu ya mjadala huu?
ni kweli mimi sijui soka na ni mshabiki maandazi....next time i will be calling u some names and take it as a man..respect is two way....now let me put u where u belong.
usidandie tu comments za watu bila kujua zimeanzia wapi....hujui carrick kaingiaje kwenye huu mjadala....aliemuingiza carrick kwenye huu mjadala ni Malafyale wakati anajibu post yangu niliyoandika "BR yuko right kumwambia SG hawezi kucheza muda wote coz he is 34" ndio Malafyale akasema mbona carrick is 33 na anaanza man utd?? nikamjibu silaha ya carrick ni brain na long passes lakini SG anatumia sana nguvu na ni box to box midfielder.....then malayale akasema huyo carrick timu ya taifa anasubiri kwa SG etc nikamwambia nikifikiri unalimganisha role na position zao uwanjani na mimi kama kawa nikampa dongo linalowauma nyinyi wote 'carrick has won epl title SG has never' thats a fact....kwahio usijifanye wewe mjuaje kuita watu majina ya dharau coz kila mtu hilo halimshindi...unaweza kuniona mimi shabiki maandazi na mimi nikakuona mpuuzi fulani tu.