Liverpool FC (The Reds) | Special Thread



Mkuu BR hawezi kujifunza, game na swans tulipotea kabisa kipindi cha kwanza na alitakiwa aangalie game ya manure na spurs . man walitakata sana kati na Moreno alupotea mapema sana alitakiwa atolewe kabla half time
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli mkuu, lakini BR alitakiwa aelewe kwa nini tulipotezwa na swans kipindi cha kwanza Ali abadilike lakini yeye akaja na approach ile ile ya kijinga

Moreno anapaswa apewe mapumziko ametumika sana Jana imeonesha.

At least Mkuu umeona source ya weakness kuliko waliamua kumlaumu Stevie, hakuna anayeweza kuhakikisha kuwa kama SG angemaliza ile game ya jana basi mngeshinda.
Magoli yote ya United yalitokea upande wa kushoto wa defense yenu, kwa Moreno na Sakho lakini sidhani kama individual players wanastahili sana lawama kuliko Kocha na mfumo aliotumia
Pamoja na kuwa hiyo formation imempa matokeo mazuri mwaka huu, lakini haina maana kwamba hawezi kubadili mfumo na baadhi ya position uwanjani kutokana na mpinzani, kwanini Emre Can hampi chance ya kucheza kwenye kiungo? Kwa nini kwa match ya jana asichezesha say 4-3-3 au 4-2-3-1 ilimradi tu achezeshe 4 at the back?
Rodgers was naive na ndiye aliyeiweka rehani nafasi yenu ya kumaliza ndani ya top 4, lakini bado games nyingi tu mpaka ligi ikamilike ile spirit ya kops huu ndio muda wake
 

Siwezi kumlaumu BR kwa lolote hapa. It's mediocrity ya wachezaji and their inability to handle pressure at a big stage. Nimeangalia highlights za game ya jana - it's all shambolic display from all the players across the pitch hata kama BR ange-flip-flop wachezaji kwa namna gani. He's a very smart tactician whilst on the touchline.

Since Dedember, the same players and the same formation imetumika and has won us plenty of plaudits hadi tukawa tagged "the in-form EPL team of 2015".

Ile mechi na Swansea ilikuwa tupoteze - but thanks to the profligacy ya washambuliaji wa Swansea tukatoka na ushindi wa bahati.

Tunaye coach mzuri technically but hatuna kikosi cha "champions" pale. Under BR's tutelage , am sure mchezaji kama Di Maria angeng'ara kama alivyokuwa Suarez.

FSG need to cough up some colossal dough and get us marquee signings in the summer, or else...... (hapa nina tusi baya sana, so wacha nikae nalo mwenyewe!!)
 
Mkuu BR hawezi kujifunza, game na swans tulipotea kabisa kipindi cha kwanza na alitakiwa aangalie game ya manure na spurs . man walitakata sana kati na Moreno alupotea mapema sana alitakiwa atolewe kabla half time

Moreno is totally out of form jana tangu game inaanza Sakho alijitahidi kum-cover ila ilikuwa ngumu

Sina la kulaumu sana ila deeply tunahitaji some players ambao wata-compete real on pitch we have a young player only
 


Mkuu nashangaa kuona bado mna matumaini na top four... niliwambia hapo nyuma kua baada ya huu mchezo sasa tunaweza tukaongea....nyie top four hamtoingia ata iweje...mna michezo miwili mikubwa alafu ugenini amabayo lazima mfungwe....Wa chelsea na wa Arsenal na tayari ManU wako juu yenu points 5 kitu amabcho hatoweza kumshusha ata sijui itokee nini....BR anapaswa kulaumiwa sn ktk hii michezo mikubwa maana amekua anafungwa tu, hawezi kuwaanda vijana wake kukabiliana na hizi timu kubwa....atakua anawabahatisha Man City na Arseanl lkn sio ManU au Chelsea na siku kale kazee Wenger kakiamka vibaya katalichinja jogoo hapohapo kwenu....

Jipangeni msimu ujao wakuu nawapeni pole sn kwa hilo...
 
Last edited by a moderator:

Mkuu!!Usihofu kabisa, ktk mechi nane zilizobakia kuna point 24 za kutafutwa, Siishangai sana. Man U wali deserve ushindi jana kwa mbinu zetu kushindwa, but anayesema ligi imeisha anaukosea mpira adabu kabisa
 


Mkuu umesomeka vema mkuu....nitashangaa kuona mtu anamtetea BR ktk hili......
 

Ok ata km hamkupotezwa muda wote lkn mlizidiwa ndio maana mkafungwa...

Km ukicheza faulo ndani box lako unategemea usiadhibiwe.....?

PSG walikua nusu uwanjani na wakatutoa nje ya CL, huoni km kua watu kumi hiyo sio sababu ya kujitetea kupoteza mchezo?

Di maria alipodaka mpira mwamuzi hakumuacha tu...alipuliza kipenga na akawapa nyie mpira au mlitaka awape Penalty ata km ilikua nje ya box la ManU?

Jones alipewa kadi ya njano...mwamuzi hakumuacha tu...na kitu kingine ambacho mwamuzi aliwashitukia ni wachezaji wenu kujifanyisha wamechezewa madhambi ili mwamuzi atoe kadi nyekundu kwa ManU pia... hili lilionekana kwa kipa wenu dhidi ya Rooney na hilo tukio la Jones...janja yenu refa alikwisha igundua....
 
Reactions: Nzi

Ngoja ubingwa upepeee ndio ujue mpira hauna adabu...ha ha ha ha, usitutoe LFC top 4, tuko nyuma only 5pnts wakati bado kuna point 24 za kushindaniwa, United did well, wamejiweka pazuri but ligi still haijamalizika
 
Mkuu!!Usihofu kabisa, ktk mechi nane zilizobakia kuna point 24 za kutafutwa, Siishangai sana. Man U wali deserve ushindi jana kwa mbinu zetu kushindwa, but anayesema ligi imeisha anaukosea mpira adabu kabisa

Nimefurahishwa na sentesi yako ya mwisho ulimalizia....

Ngoja ubingwa upepeee ndio ujue mpira hauna adabu...ha ha ha ha, usitutoe LFC top 4, tuko nyuma only 5pnts wakati bado kuna point 24 za kushindaniwa, United did well, wamejiweka pazuri but ligi still haijamalizika

Mkuu km BR hatobadilika hasa anapokutana na timu kubwa, top four hiyo msahau kabisa....

Mna michezo miwili mikubwa ambayo lazima mtapoteza wakati huo ManU wanaweza kupoteza mchezo mmoja tu mkubwa dhidi ya chelsea pale darajani na sasa wako juu yenu kwa points 5.....huoni km hamuwezi kufika top 4?
 

Mkuu with all due respect, Rodgers is yet to be called a smart tactician, technically he is one of the best in the EPL but tactically, hamgusi hata Tony Pulis.
Msimu jana kuna tactical errors alizifanya Rodgers ambazo ziliicost team ubingwa wa EPL particularly games at home Vs Chelsea & away to C.Palace. Hakua na haja ya kwenda all guns blazing against Chelsea siku ambayo alihitaji droo tu, akaenda C.Palace akacheza the same, matokeo yake wote tunajua.
A smart tactician asingeruhusu team yake kushuka kiwango namna Liverpool ilivyoshuka mwanzoni mwa msimu huu kwa sababu tu mchezaji mmoja aliondoka klabuni, asingenunua mamluki ya wachezaji asiojua kama watafit kwenye mfumo wake, asingefanya makosa ya kitoto kabisa kwenye ile game ya Bernabeu against Madrid.
Mwaka huu (2015) mmekua kwenye kiwango safi kuliko team yeyote, na hicho kiwango ndio kimempa kiburi Rodgers kuapproach each game in the same manner bila kujali anacheza na nani na anahitaji nini from a particular game, ndio maana nikasema Rodgers is naive
SG alichwa bench, RS amedrop sana pamoja na matatizo yake nje ya uwanja, AL hovyo kabisa, kwenye kiungo yenu JA na JH walichemsha sana jana kuna time Can alikua anaingia kati kuwapa tafu, kwanini Rodgers hakuliona na kurekebisha hilo? Kwanini baada ya red card ya SG hakumpeleka Can pale katikati at least atafute droo ili kukeep distance na Manure kwenye nafasi ya nne?
Pamoja na mfumo kufanya vizuri toka mwaka ugeuke, hivi kweli kocha makini hawezi kuhisi kwamba labla team yake inaweza kuwa too predictable against the great tacticians like Van Gaal, kwa hiyo anahitaji kubadilisha team kidogo? So far pamoja na hii form ya 2015 Rodgers ameshindwa kufurukuta mbele ya real tacticians, MOU and Van Gaal wote wamemchapa.
Hawahawa wachezaji unaowaponda ndio wamefanya vizuri kwa mwaka huu mpaka jana walipokwaa kisiki, kama wangekua viazi kivilee kama unavyosema wasingeweza kuwacontain Manure baada ya ile red card, tungeiona team inafall into pieces.
 
Mourinho umemaliza. watu wasipoelewa haya uliosema yote basi ujue kuna shida.....

Alafu bado eti wanakua na matumaini ya kuingia top 4 eti kisa kisa bado kuna michezo 8 wakati huo wanasahau bado hawajukatana na gwiji la mbinu Jose Mou na Mzee Wenger......BR ndio wa kulaumiwa ktk yote haya.
 
Last edited by a moderator:

Red, Hapo ndipo mahali ambapo napishana na fans wengi yani ukasisitiza kabisa "LAZIMA"?????????ha ha haha uwa unatazama kwanza kwenye kibuyu nini?. Basi sawa now najua hata Chelsea dhidi ya Bradford may be ulisema LAZIMA Bradford afe Stamford Bridge kisha ukatoka. Mkuu yani umeni quote niliposema tunaukosea mpira adabu, alafu bado UMEENDELEA KUUKOSEA ADABU kwa kulazimisha Kifanyike Upendacho ama Uwazacho
 

Mkuu, Vizuri umepaona. Hapo ndipo kulipofanya tupoteze jana.
 


Hahaahahahaa mbona nyie mnakomaa kua mtaingia top 4 wakati dalili zote za kuingia top 4 hakuna? Hamuukosei mpira adabu kweli?
 
Hahaahahahaa mbona nyie mnakomaa kua mtaingia top 4 wakati dalili zote za kuingia top 4 hakuna? Hamuukosei mpira adabu kweli?

Ha ha ha ha nimesema uko juu, ligi bado mechi 8 ambazo ni sawa na 24pnts, anyone can make it. Tunatofautiana mazingira tu.
 
Ha ha ha ha nimesema uko juu, ligi bado mechi 8 ambazo ni sawa na 24pnts, anyone can make it. Tunatofautiana mazingira tu.

Anyone can make it but not Liverpool....Tukubaliane hapo kwanza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…