Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,809
- 15,421
Jana bwana wadau wa JF Dar Wing tulipata ugeni kutoka Arusha wing, sasa ikabidi ni coordinate na baadhi ya wadau wenzangu kina Madam B, amu, Kipaji Halisi, Kaizer Paloma, Bujibuji, Asprin, Vin Diesel na mdau mmoja aliyevamia meza yetu na kujitambulisha kwa jina ambalo miongoni mwetu hakuna aliyewahi kukutana na jina hilo hapa JF.
Tuachane na hayo maana hata jina lenyewe nimeshalisahau. Bujibuji hebu nikumbushe, yule jamaa BONGE alisema anaitwa nani vile, maana nakumbuka alisema anajuana na yule Mbunge Mtata wa chama Tawala wa kule Singida….. Hebu ngoja nimpotezee kwanza nisije nikapoteza point ya kile nilichotaka kusema.
Sasa, pale Leo Tupo Hapa Pub, Bwana mkubwa MJEDA kafanya reshuffle kidogo, kaleta binti mmoja kutoka mji kasoro bahari ili kuchukua nafasi ya Binti mwingine aliyepangiwa kazi maalum.
Huyu Binti mpya, ambaye alitambulishwa kwetu na MJEDA kwamba anaitwa KAUNDIME, kwa kweli Mwenyenzi Mungu amemjaalia. Ni binti mfupi kidogo kama amu, rangi ya mwili wake uko kama chocolate, ana kijikalio cha kushuka na miguu iliyoshiba hasa. Macho yake madogo kama anasinzia na matiti ya kutuna kwa juu. Lakini pia amejaaliwa sauti nyororo na akizungumza ni kama vile hataki ana anahisi uvivu….
Sasa chalii yetu kutoka Arusha nikamuona macho kodo kodo, nikajua hapa lazima pataumana, ikabidi nitafute mwenyeji, ili nipate wasifu wa yule binti maana wakati huo Mjeda alishaondoka. Si nikampata kijana mmoja anayesaidia shughuli za pale Pub, akaniambia yule binti ni habari ingine, ukiingia kwenye himaya yake ufanye kazi ya ziada kuchomoka maana binti anayajua mahaba ya pwani kuliko.
Aliniambia kwamba ashavunja ndoa zaidi ya 6 huko Magomeni na baada ya kutangaziwa vita ndio akahamia Mwanyamala kwa Ali Manjunju.
Wakati namegewa habari za mrembo Kaundime, Upande wa pili naona mawasiliano kati ya Chalii yetu kutoka A Town na Kaundime yamepamba moto. Chalii hataki kuhudumiwa na mtu yeyote isipokuwa Kaundime. Nikajua hapa Ngondo Igwa. Lakini nikaona hapa lazima nimuokoe chalii yetu, Nikamshirikisha Bujibuji ili ampe somo, Bujibuji kamsomesha Chalii, lakini kwani aliewa. KONTENSA zishashuka kule kunako kichwa cha chini…. Chalii haelewi soma, ni yeye na Kaundime………….Kaundime na yeye.
Mie na Kaizer tukaondoka lakini nikaacha maagizo kwa Bujibuji ili aweke ulinzi shirikishi tusije mpoteza chalii halafu Mwenyekiti wa arusha Wing Arushaone atuletee noma.
Nilipofika Home Bujibuji akanipigia simu kunijuza kwamba Chalii kutoka Arusha katoweka katika mazingira ya kutatanisha. Swali langu la kwanza niliuliza iwapo Kaundime yupo, Bujibuji akaniambia kwamba na yeye haonekani katika eneo la tukio, nikajua chalii keshanasa katika mtego wa Kaundime.
Nilijaribu kupiga simu yake haipatikani, mpaka asubuhi hii simu yake haipatikani, nikajua hapa sasa wana JF wa Dar Wing tuna kesi ya kujibu. Ni hivi punde nimepokea simu kutoka wka chalii.....
" Aisee Mtambuzi, unajua nimeshangaa bado niko Mwananyamala hadi mida hii na simu yangu ilikuwa imezimwa lakini sikumbuki kama ni mimi nilizima maana naona bado iko na chaji……..…"
Nikamuuliza uko na nani..
"Ah, we acha tu tutaongea jioni…."
Sikukubali jibu jepesi nikambana mpaka akaamua kuniambia ukweli…..
"Mzee Mtambuzi acha, yaani acha kabisa, kumbe huku Dar mnafaidi jamaa yangu……………….. Kale kabinti si kalinichukua pale kakaniambia kananipeleka kunionyesha kwake, kisha katanirudisha, basi tulipofika hata sijui nguo nilivua mwenyewe au nilivuliwa, nilishangaa niko juu nazungushwa kama pangaboi la helikopta, yaani hakuna rangi sikuacha ona…… we acha kabisa kale katoto ni kadogo lakini kanajua mambo. Hata sijui nitawambia nini wenyeji wangu…….."
Nikamuuliza sasa nikufuate nikurudishe nyumbani…
"Mzee Mtambuzi hebu subiri kwanza……" aliposema hivyo simu ikakatwa, na nilipojaribu kupiga haipatikani kabisa…… Mpaka mida hii bado haipatikani kabisa.
Nahisi tutakuwa na kesi ya kujibu kwa wadau wa arusha Wing
Mh,Mbona Kaundime anataka kutuletea balaa aisee…..
Bujibuji msaada tafadhali