Livingstone Lusinde(Mb): Muuza kahawa aliyemuoa house girl!

Livingstone Lusinde(Mb): Muuza kahawa aliyemuoa house girl!

Mbunge wa Mtera mh Lusinde ( Kibajaji ) amesema katika ujana wake alikuwa ni muuza kahawa maarufu pale Kawe ambapo alijulikana kama Stone. Lusinde amesema yeye elimu yake siyo rasmi na kwa hiyo hana cheti chochote cha taaluma ila anajivunia mafanikio makubwa aliyonayo kuwapita hata hao wenye PhD.

Amesisitiza kwamba akiwa muuza kahawa alibahatika kumuoa house girl na waliishi maisha ya kuunga unga lakini kwa sasa mke wake huyo anaendesha Prado VX, hivyo anamshukuru Mungu na kufafanua kuwa kiini cha mafamikio yake ni uaminifu, nidhamu na heshima ya hali ya juu aliyonayo.

Mh Lusinde ameyasema hayo yote katika semina ya fursa anzia sokoni iliyoandaliwa na Clouds Media na kurushwa luningani mubashara kupitia Clouds Tv jana mjini Dodoma.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, Nawasilisha!
Mnaropokaga hivi hivi,mkipewa vyeo vya hisani na kuambiwa mmekiuka maadili ya utumishi wa umma kwa kufanya kazi bila elimu,,,munaanza kulia makanisani.
 
Katiba ya kujua kusoma na kuandika kama sifa ya mbunge inaleta dharau kwa wasomi,yaani muuza kahawa anakuja sema ana maisha mazuri kuliko msomi kisa kupiga domo na kujipendekeza tu.
Eti ndio mtunga sheria,my foot.
 
Namfahamu alipokua Kawe amesema ukweli kuhusu elimu yake. Ana kipaji cha kusuka hoja tangu akiwa Chadema. Namkumbuka kwa Serengeti alizonipa pale Open Air Kawe. Angeongezea elimu ya vitabuni pamoja na kipaji chake angepaa
 
Ase alafu mtegemee Nchi ya Viwanda.
Yes! Amefanikiwa kimaisha-Je ni Kahawa ndiyo iliyomfikisha hapo au kuna Jingine????.
Mke wake anaendesha Prado Vx kwa biashara ipi to House Girl ????.
Anafaa ajikalie kimya ili asionyeshe mapungufu yake. Maana kihoja yuko Zero!
 
fb6a443bfd9cc650c1ebffe9b97afb49.jpg
a33a88fff053bb0ac289c0530e0ec044.jpg
 
Tejateja elimu ni kitu ambacho kipo na kinapatikana kiurahisi? Justify it homie.
 
Hii ndo tabia ya Watu waliofanikiwa, kila unaemsikiliza utasikia Mimi nilianza kwa kujaza wino kwenye speedo nakuuza..,
 
Mbunge wa Mtera mh Lusinde ( Kibajaji ) amesema katika ujana wake alikuwa ni muuza kahawa maarufu pale Kawe ambapo alijulikana kama Stone. Lusinde amesema yeye elimu yake siyo rasmi na kwa hiyo hana cheti chochote cha taaluma ila anajivunia mafanikio makubwa aliyonayo kuwapita hata hao wenye PhD.

Amesisitiza kwamba akiwa muuza kahawa alibahatika kumuoa house girl na waliishi maisha ya kuunga unga lakini kwa sasa mke wake huyo anaendesha Prado VX, hivyo anamshukuru Mungu na kufafanua kuwa kiini cha mafamikio yake ni uaminifu, nidhamu na heshima ya hali ya juu aliyonayo.

Mh Lusinde ameyasema hayo yote katika semina ya fursa anzia sokoni iliyoandaliwa na Clouds Media na kurushwa luningani mubashara kupitia Clouds Tv jana mjini Dodoma.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, Nawasilisha!
siku zote watu wanasema humu JF kwamba huyu jamaa Lusinde hana elimu siyo msomi,anakariri tu vitu,kumbe ni kweli nilikuwa si amini,kumbe ndo maana sheria nyingi za hovyo zinapitishwa na ccm mbungeni
 
siku zote watu wanasema humu JF kwamba huyu jamaa Lusinde hana elimu siyo msomi,anakariri tu vitu,kumbe ni kweli nilikuwa si amini,kumbe ndo maana sheria nyingi za hovyo zinapitishwa na ccm mbungeni
Mkuu kwani huko bungeni yuko Kibajaji peke yake?!!!
 
Katiba ya kujua kusoma na kuandika kama sifa ya mbunge inaleta dharau kwa wasomi,yaani muuza kahawa anakuja sema ana maisha mazuri kuliko msomi kisa kupiga domo na kujipendekeza tu.
Mie sina shida na mtu hata kama hajaingia darasani na ana milki mali kushinda maprofesa, tatizo langu lipo hapa wengi wao wana dharau sana kwa wasomi wetu na ukichunguza hata hao wanaojitokeza kwenye fursa utagundua wengi wao walijikatia tamaa na hata hayo mafanikio wanayoyazungumza kama sehemu ya kuhamamisha vijana unakuta yamekuja by chance na hapo ndo mwanzo wa dharau.

Tofauti na mtu aliekimbia shule akawa anakata mkaa mpaka akawa mfanyabiashara mkubwa (wengi wana nidhamu kwa watu wa tabaka zote)
 
Katiba ya kujua kusoma na kuandika kama sifa ya mbunge inaleta dharau kwa wasomi,yaani muuza kahawa anakuja sema ana maisha mazuri kuliko msomi kisa kupiga domo na kujipendekeza tu.
Kwani ubunge ni taaluma


Ni ajabu kumuona chumi kama lipumba ,na ma inginia wakiweka taaluma zao pembeni na kuendeshwa endeshwa kama gari bovu

Halafu hakuna sehemu kwenye katiba inasema msomi awe na maisha mazuri kuliko muuza kahawa au hujui kwamba Rais magufuli ni rais wa wanyonge
 
wanatoa Inspirational ideas kwa watu kama nyie ambao hamjafanikiwa!..au ulitaka mpaka bakhressa aje aseme ndo uone kutosoma sio kutofanikiwa?..
Wanatushushia hadhi ya bunge letu tukufu.
 
Hawa vilaza hawajitambui kwamba ni vilaza. Mtu akiwa na sent mbili tu tayari anajilinganisha na professor. Tumia hiyo sent basi leo ununue PhD ya orthopedic.
Kama mwenye hiyo phd ameshindwa kuibali kuwa fedha na kuishia kuajiriwa sasa uinunue ili iwaje
 
Ni sawa kama amepigania maisha anastahili pongezi.lakini aache kutukana anapokuwa jukwaani.hata kama hakusoma lakini ajue yeye ni mbunge ni kiongozi anatakiwa kuwa mfano.
 
Back
Top Bottom