Louisiana: Serikali yaamuru amri kumi za Mungu kubandikwa madarasani Marekani

Louisiana: Serikali yaamuru amri kumi za Mungu kubandikwa madarasani Marekani

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2020
Posts
7,899
Reaction score
10,415
Louisiana imekuwa jimbo la kwanza nchini Marekani kutaka kila darasa la shule za serikali, kuanzia msingi hadi chuo kikuu kubandika Amri Kumi za Mungu ukutani.

Hatua hiyo iliyochochewa na chama cha Republican na kutiwa saini kuwa sheria na Gavana wa jimbo hilo Jeff Landry (pichani) siku ya Jumatano, inaelezea amri hizo kuwa ni “nyaraka za msingi wa taifa letu na serikali”.

Hata hivyo sheria hiyo inatarajiwa kupingwa mahakamani na makundi ya wanaharakati wa haki za kiraia, ambao wanasema inakinzana na kifungu cha kwanza cha katiba ya Marekani cha kutenganisha baina ya kanisa na mamlaka.

Shirika la Utangazaji la BBC limesema amri hizo lazima ziwe zimebandikwa kwenye madarasa ya shule zote zinazopewa fedha za umma ifikapo mwaka 2025.

Sheria kama hizo zimependekezwa hivi karibuni katika majimbo ambayo ni ngome za chama cha Republican kama vile Texas, Okhlahoma na Utah. Kumekuwa na mpambano mkali wa kisheria kuhusiana na suala la kubandika Amri Kumi kwenye ofisi za serikali kama vile shule, mahakama na vituo vya polisi. Mwaka 1980, Mahakama Kuu ilitupilia mbali sheria kama hiyo katika jimbo la Kentucky lililotaka amri hizo kubandikwa katika shule za elimu ya kati.

1718931595472.jpeg

Pia soma:Kuna amri 10 za Mungu. Je,ikatokea fursa ya kupendekeza Amri ya 11. Wewe ungependekeza Amri ipi mpya?
 
Hiyo hiyo Marekani inaandaa mswada wa kupinga mahubiri ya imani ya kirokole "anti sematism". Sasa kipi ni kipi?
Siasa za Marekani zinachanganya sana. Hao conservatives wa Louisiana wanajidaia wanalinda religious freedom lakini ukiawaambia waweke misahafu ya kiislamu mashuleni utawasikia waking'aka,
 
Si ni dini? ukishasema uhuru wd kuabudu, huwezi kutenga uislamu

Pamoja na kwamba ni dini lakini uislamu si imani ya kwanza, wala ya pili, wala ya tatu kwa wazungu wa kimarekani...

Unaishi/umeishi huko, hili unalijua...
 
Siasa za Marekani zinachanganya sana. Hao conservatives wa Louisiana wanajidaia wanalinda religious freedom lakini ukiawaambia waweke misahafu ya kiislamu mashuleni utawasikia waking'aka,
Huko afigani kuna hata kanisa?
 
Hiyo hiyo Marekani inaandaa mswada wa kupinga mahubiri ya imani ya kirokole "antisemitism". Sasa kipi ni kipi?
As for me walokole huwa hawahubiri neno la Mungu wanachofanya wao ni kuwashambulia wasiokuwa wenzao.

Kusimama mbele ya hadhira ya watu wenye imani tofauti tofauti na kuanza kuwatukania imani zao ambazo wewe hujawahi kuzisoma kwa undani huku ya kwako hawajawahi kuigusa siyo jambo jema.
 
As for me walokole huwa hawahubiri neno la Mungu wanachofanya wao ni kuwashambulia wasiokuwa wenzao.

Kusimama mbele ya hadhira ya watu wenye imani tofauti tofauti na kuanza kuwatukania imani zao ambazo wewe hujawahi kuzisoma kwa undani huku ya kwako hawajawahi kuigusa siyo jambo jema.
Unazijua principal za kuhubiri?
 
Unazijua principal za kuhubiri?
Siyo muhubiri mimi so sizijui hizo kanuni lakini kikawaida tu kanuni ya kwanza ya kusema chochote kwenye hadhira iliyojaa watu msiofungamana itikadi ni kuheshimu vile ulivyowakuta navyo eg mawazo imani mitazamo .

Na hiki kitu kwa wahubiri wengi wa kilokole hawana.
 
Back
Top Bottom