Love kwa wale wote ambao hamchoki kuwapa tafu waliokwama kimaisha

Love kwa wale wote ambao hamchoki kuwapa tafu waliokwama kimaisha

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Niwe mkweli kabisa saa sita hii usiku nimekuwa inspired na uzi wa Robidinyo ambaye ameeleza changamoto ya kutokuwa na kazi au biashara jinsi maisha yanavyokuwa magumu.

Nikajikuta nataka kuwapa respect wale wote ambao hamchoki kutoa msaada kwa ndugu na jamaa zenu waliopata changamoto za hapa na pale,Mungu awape maisha marefu sana

Kwa kawaida mtu akikuomba msaada kwa kipindi kirefu sana huwa tuna kawaida ya kumchoka,na hapo tutaacha kupokea simu zake wala kujibu meseji zake na tunamuona msumbufu

Heshima za dhati kwako wewe ambaye pamoja na kuombwa msaada na mtu wako au jamaa yako wa karibu mara kwa mara lakini hujachoka kusaidia wala hujaacha kupokea simu za watu wako wenye shida wala kujibu meseji.

Wewe ni mtu wa maana sana unastahili medali ya dhahabu,niwaambie kitu?

Hakuna mtu ambaye anapenda kuwa omba omba tena mwenye familia ila ni shida tu imemkuta,ndio maana anajidhalilisha na kuomba msaada.

Hivyo ukimuona mtu anapenda mara kwa mara kukucheki ujue anajisikia comfortable kutaka msaada kwako,anaamini wewe ni mtu pekee ambaye unaweza kumstiri na kuficha aibu yake,basi nawe mstiri hakika hutujui kesho yetu

Binafsi nishawahi pitia hayo maisha najua yanatesa sana,una watoto halafu hujui kesho utakula nini,na ukila mchana hujui jioni utakula nini?

Nakumbuka kuna siku kumekucha mpaka mida ya saa nne asubuhi haikujulikana breakfast itapatikana wapi, Nina watoto wawili hapo,baby girl wangu analia njaa,,ukimtazama mama watoto analia hajui cha kufanya,,mara hapa na pale unamcheki mwamba unamuelezea changamoto yako mara paap muamala huu hapa,analeta tabasamu nyumbani.

Ninachotaka kusema baadhi yetu tumewahi kupitia katika changamoto na wengine wanapitia kipindi hiki,,kikubwa usikate tamaa God is always good,,ipo siku utakuja kusahau na kuwa historia

Wadau tafadhali msichoke kuwasaidia wenye shida tena wenye familia wanapitia kipindi kigumu sana,,usichoke haijalishi mara ngapi atakucheki kama unacho msaidie,hutamsaidia milele ipo siku Mwenyezi Mungu atamuinua,na hatosahau msaada wako katika maisha yake

Wakati mwingine Mungu anakutumia wewe kumstiri mja wake na atazidi kukuinua zaidi

Usichoke na usisite kutoa msaada kwa wahitaji kwani wanakuhitaji sana,,much respect kwenu enyi wenye mioyo ya utu na ubinadamu

Gracias

Ni hayo tu!
 
Wengine u omba omba unatokana na uvivu,kujiona anastahili kusaidiwa na kujilegeza anyway u omba omba sio mzuri tujifunze kutafuta vyetu ili tuheshimike.
 
Sikatai kuna wale wa uvivu lkn hakuna mtu mwenye majukumu akataka kuwa omba omba nitakuwa mtu wa mwisho kukubali hilo

Utamsaidia elfu kumi,hapo hajala bado,hajalipa bills ,hajapata sabuni na mambo mengine,,kiukweli hawezi ridhika na hayo maisha kwakuwa huo msaada haukidhi mahitaji bali walau unapunguza kiasi flani cha changamoto

Je mtu kama huyu unadhani atabweteka tu kutegemea buku kumi au tano?
 
Umenena vyema sana nimeanzisha kikundi cha cha kutoa msaada kwa watoto wasio jiweza kwenye kijiji chetu toka mwaka juzi na na kwahilo dogo
tu najivunia mno🙏
 
Umenena vyema sana nimeanzisha kikundi cha cha kutoa msaada kwa watoto wasio jiweza kwenye kijiji chetu toka mwaka juzi na na kwahilo dogo
tu najivunia mno🙏
Mungu akubariki sana chief kwa kushow love,,unajiwekea hazina ya baadae ,hakika karma haitokutupa
 
Japo sio muumini sana wa hyo dhana ya Mungu ila napenda kufanya vile nilivyo.
Unajua tumeumbwa kujua baya na zuri,,kwhiyo hata kama humuamini Mungu lkn ile natural instict inatuongoza kuyaendea mambo mema
 
Niwe mkweli kabisa saa sita hii usiku nimekuwa inspired na uzi wa Robidinyo ambaye ameeleza changamoto ya kutokuwa na kazi au biashara jinsi maisha yanavyokuwa magumu.

Nikajikuta nataka kuwapa respect wale wote ambao hamchoki kutoa msaada kwa ndugu na jamaa zenu waliopata changamoto za hapa na pale,Mungu awape maisha marefu sana

Kwa kawaida mtu akikuomba msaada kwa kipindi kirefu sana huwa tuna kawaida ya kumchoka,na hapo tutaacha kupokea simu zake wala kujibu meseji zake na tunamuona msumbufu

Heshima za dhati kwako wewe ambaye pamoja na kuombwa msaada na mtu wako au jamaa yako wa karibu mara kwa mara lakini hujachoka kusaidia wala hujaacha kupokea simu za watu wako wenye shida wala kujibu meseji.

Wewe ni mtu wa maana sana unastahili medali ya dhahabu,niwaambie kitu?

Hakuna mtu ambaye anapenda kuwa omba omba tena mwenye familia ila ni shida tu imemkuta,ndio maana anajidhalilisha na kuomba msaada.

Hivyo ukimuona mtu anapenda mara kwa mara kukucheki ujue anajisikia comfortable kutaka msaada kwako,anaamini wewe ni mtu pekee ambaye unaweza kumstiri na kuficha aibu yake,basi nawe mstiri hakika hutujui kesho yetu

Binafsi nishawahi pitia hayo maisha najua yanatesa sana,una watoto halafu hujui kesho utakula nini,na ukila mchana hujui jioni utakula nini?

Nakumbuka kuna siku kumekucha mpaka mida ya saa nne asubuhi haikujulikana breakfast itapatikana wapi, Nina watoto wawili hapo,baby girl wangu analia njaa,,ukimtazama mama watoto analia hajui cha kufanya,,mara hapa na pale unamcheki mwamba unamuelezea changamoto yako mara paap muamala huu hapa,analeta tabasamu nyumbani.

Ninachotaka kusema baadhi yetu tumewahi kupitia katika changamoto na wengine wanapitia kipindi hiki,,kikubwa usikate tamaa God is always good,,ipo siku utakuja kusahau na kuwa historia

Wadau tafadhali msichoke kuwasaidia wenye shida tena wenye familia wanapitia kipindi kigumu sana,,usichoke haijalishi mara ngapi atakucheki kama unacho msaidie,hutamsaidia milele ipo siku Mwenyezi Mungu atamuinua,na hatosahau msaada wako katika maisha yake

Wakati mwingine Mungu anakutumia wewe kumstiri mja wake na atazidi kukuinua zaidi

Usichoke na usisite kutoa msaada kwa wahitaji kwani wanakuhitaji sana,,much respect kwenu enyi wenye mioyo ya utu na ubinadamu

Gracias

Ni hayo tu!
Endeleeni tu kutumika kama dumping sites kisa mnataka sifa za kuonekana ni watu wema. Saidia mtu genuinely kwa moyo kama unaona he/she deserves comforts. Sio wote wanastahili msaada wako, wema uwe na kiasi.
 
Endeleeni tu kutumika kama dumping sites kisa mnataka sifa za kuonekana ni watu wema. Saidia mtu genuinely kwa moyo kama unaona he/she deserves comforts. Sio wote wanastahili msaada wako, wema uwe na kiasi.
Hakuna kitu kigumu kama kutoa pesa kumsaidia mtu,na ukimuona mtu anatoa pesa kumsaidia mtu mpe heshima yake,kwasababu hakuna asiyependa pesa.

Hata katika upande wa imani ukimuona mtu anatoa hela yake basi ujue huyo ana imani ya kweli

My point hakuna mwenye kutoa kwa dhati akataka sifa bali ana moyo wa dhahabu
 
Back
Top Bottom