ni kweli umechakachua mno. Tuanze na hivi
1. lowasa- hana sifa za kuwa raisi wa tanzania ni mchafu kuliko unavyo fikiria
2. huseni mwinyi- sijaona mchango wake katika nchi hii kwanza alitakiwa awe amekwisha jiuzuru kutokana na mabomu ya mbagala na gongo la mboto, c muwajibikaji, au umemuweka kisa mtoto wa raisi msataafu? Basi unge muweka na ridhiwani pamoja na makongolo nyerere
3. sumaye , huyu ni fisadi sana kipindi ubinafishaji umeshika kasi enzi za mkapa alijibinasifishia mali nyingi sana za uma, unge kuwa arusha ungeelewa zaidi story zake
4. nchimbi- hana uwezo wa hata kuwa waziri mkuu, sijui umelenga nini katika kuwa teua hao watu, tupe mchango wake katika taifa hili, ameifanyia nini tanzania?
5. lipumba- huyu ameisha choka sana na ukizingatia cuf wako kwenye ndoa na ccm huyu haamniniki tena ni ndumila kutatu. Ccm b
6.migiro- huyu nae kuwa naibu katibu mkuu wa un c kwamba ni cheo kikubwa sana, na hata cheo cha katibu mkuu wa umoja wa mataifa huwezi linganisha na cheo cha uwaziri mkuu, sifa ya migiro kuteuliwa ilikuwa moja tu, alikuwa waziri wa mambo ya nje pekee mwanamke katika nchi masikini, kama sikosei walikuwa wawili pamoja na wa south africa but bank mun akaona amchukue migiro, na hata hivyo kule un yeye hana say yoyote, ulisha wahi kumsikia hata cnn akitoa tamko? Yeye ni kama alivyo uingereza malikia na waziri mkuu.
7. dr slaa- hapa sina coment kabisa na sina uwezo wa kukoment hapa.