KPI za wabunge ni kuhudhuria vikao au kuongea? ama vyote? Mana Lowassa kahudhuria karibu vikao vyote lakini hajaongea. na Mbunge anapoongea maana yake anawakilisha mawazo ya wapiga kura wake. Lowassa hakuongea bungeni, lakini tulimwona akiwa bega kwa bega na wapiga kura wake kwa shughuli za maendeleo, hata kama ni mara chache.
Hakuhitaji kampeni za kuzima moto kama tutakazoona kwa baadhi ya waheshimiwa baada ya kuvunjwa kwa bunge hili. Wengi ndo watakumbuka kwenda katika majimbo wao wakijaribu kuvuta shuka asubuhi.
But all in all, the big question about his involvement in Richmond PLC is still uncovered. ...to add salts onto the wounds, the matter has been laid to rest. Ni kama vile ndoa iliyofungwa kanisani na kubarikiwa na Padre haitakiwi kuonyeshwa vidole tena.
Watanzania machozi yetu yamekuwa kama ya kilio cha samaki...yamekwenda na maji. Wabunge wametusaliti! Justice delayed, justice denied!!!!