LGE2024 Ludewa, Mkoani Njombe, Majina ya Wagombea Kupitia CHADEMA hayamo Kwenye Karatasi za Kupigia Kura.

LGE2024 Ludewa, Mkoani Njombe, Majina ya Wagombea Kupitia CHADEMA hayamo Kwenye Karatasi za Kupigia Kura.

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Mkoani Njombe, na hasa wilayani Ludewa, uchaguzi umevurugika kwa kiwango cha kutisha.

Awali, katibu wa CHADEMA mkoani Njombe, alieleza kuwa wilaya ya Ludewa ilikuwa ya pili kitaifa kwa idadi kubwa kuenguliwa wagombea wa CHADEMA, ambapo kati ya wagombea 198 wa vitongoji, walienguliwa wote, kati ya wagombea 44 wa nafasi za wenyeviti wa vijiji, walienguliwa 42, na kati ya wagombea 450 wa nafasi za wajumbe, walienguliwa 440. Baada ya rufaa, majina karibia yote yalirudishwa, kasoro wagombea 6.

Kumbe urudishwaji huo wa majina, ambao unatajwa kupewa nguvu na mkuu wa mkoa bwana Mtaka, inaonekana ulikuwa na hila za mbeleni. Mkurugenzi kwa kupitia kamati yake ya rufaa, baada ya kuzikubalia rufaa na kuwatangazia kuwa wagombea wa CHADEMA wamerudishwa, hakuipeleka hiyo orodha kwa wazimamizi wasaidizi, kitendo kilichofanya baadhi ya maeneo kama vile kata ya Luilo, wagombea wa CHADEMA, kuzuiwa hata kufanya mikutano ya kampeni.

Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Ludewa, Bwana Mapunda, ameeleza kuwa, karibia maeneo yote ambayo CHADEMA ilikuwa ina uhakika wa kushinda kama vile Manda, Ngelenge, Lifua, Ludende na Luilo, majina ya wagombea wote wa CHADEMA, hayapo kwenye karatasi ya kupigia kura.

Kwenye maeneo ambayo wapiga kura wamekuwa wakali kama vile Ludende, msimamizi msaidizi wa uchaguzi amewatangazia wapiga kura kuwa amepewa maelekezo ya kuahirisha uchaguzi.

Kata ya Makonde, mwenyekiti huyo ameeleza kuwa, karatasi za kupigia kura zimeisha, walikuwa wanasuburi kuletewa nyingine, na tayari ilikuwa saa 9 alasiri.

Lifua wapiga kura baada ya kufanikiwa kuzuia uchaguzi kwa kutumia karatasi zenye wagomvea wa CCM pekee, wapiga kura wamegoma kuondoka vituoni kwa hofu kuwa wakiondoka CCM wanaweza kuingiza kura za wizi, wanasema watakuwepo vituoni mpaka saa 12 jioni, na asubuhi saa 12 tena watakuwepo kwenye vituo vya kupigia kura ili kuzuia uchafuzi wa uchaguzi.
 
Kuna watu watakuuliza " una ushahidi"?
Hawajui kwamba sasa tupp kwenye citizens journalism
Ccm wanafikiri Tanzania bado ipo kwenye kusikiliza RTD kumbe sasa kila ujinga wao unajulikana haraka kuliko wanavyotarajia .wao wamejifunika shuka
 
Mkoani Njombe, na hasa wilayani Ludewa, uchaguzi umevurugika kwa kiwango cha kutisha.

Awali, katibu wa CHADEMA mkoani Njombe, alieleza kuwa wilaya ya Ludewa ilikuwa ya pili kwa kuenguliwa wagombea wa CHADEMA, ambapo kati ya wagombea 198 wa vitongoji, walienguliwa wote, kati ya wagombea 44 wa nafasi za wenyeviti wa vijiji, walienguliwa 42, na kati ya wagombea 450 wa nafasi za wajumbe, waluenguliwa 440. Baada ya rufaa, majina karibia yote yalirudishwa, kasoro wagombea 6.

Kumbe urudishwaji huo wa majina, ambao unatajwa kupewa nguvu na mkuu wa mkoa bwana Mtaka, ulikuwa una hila za mbeleni. Mkurugenzi kwa kupitia kamati yake ya rufaa, baada ya kuzikubalia rufaa na kuwatangazia kuwa wagomvea wa CHADEMA wamerudishwa, hakuipeleka hiyo orodha kwa wazimamizi wasaidizi, kitendo kilichofanya baadha ya maeneo kama vile kata ya Luilo, wagombea wa CHADEMA, kuzuia kufanya kampeni.

Mwenyekiti huyo ameeleza kuwa, karibia maeneo yote amvayo CHADEMA ilikuwa ina uhakika wa kushinda kama vile Manda, Ngelenge, Lifua, Ludende na Luilo, majina ya wagombea wote wa CHADEMA, hayapo.

Kwenye maeneo ambayo wapiga kura wamekuwa wakali kama vile Ludende, msimamizi msaidizi wa uchaguzi amewatangazia wapiga kura kuwa amepewa maelekezo ya kuahirisha uchaguzi.

Kata ya Makonde, mwenyekiti huyo ameeleza kuwa, karatasi za kupigia kura zimeisha, walikuwa wanasuburi kuletewa nyingine, na tayari ilikuwa saa 9 alasiri.

Lifua wapiga kura walikuwa wamegoma kuondoka vituoni kwa hofu kuwa wakiondoka CCM wanaweza kuingiza kura za wizi, wanasema watakuwepo vituoni mpaka saa 12 jioni, na asubuhi saa 12 tena watakywepo kwente vituo vya kupigia kura ili kuzuia uchafuzi wa uchaguzi.
Wanachama wa CHADEMA wamechukua hatua gani?
 
Wanachama wa CHADEMA wamechukua hatua gani?
Wanasema wamewasiliana na mkurugenzi wa Wilaya, naye amejibu kuwa wanachapisha karatasi nyingine. Manda na Ngelenge wamepelekewa karatasi zenye wagombea wa CHADEMA saa 8 mchana, wakati tayari watu wamepiga kura kwa kutumia karatasi zenye wagombea pekee wa CCM. Wapiga kura ambao walikuwa bado wapo vituoni, na hawajapiga kura, ndiyo wamepewa hizo karatasi zenye majina ya wagombea wa vyama vyote. Lakini hujo Luilo, Lifuma, Ludende, mpaka saa 9 mchana hawakuwa wamepelekewa karatasi hizo za marekebisho.

Lifua wamekomaa na kufanikiwa kuzuia mtu yeyote kupiga kura mpaka fomu zenye majina ya wagombea wote zitakapofika.
 
Wanasema wamewasiliana na mkurugenzi wa Wilaya, naye amejibu kuwa wanachapisha karatasi nyingine. Manda na Ngelenge wamepelekewa karatasi zenye wagombea wa CHADEMA saa 8 mchana, wakati tayari watu wamepiga kura kwa kutumia karatasi zenye wagombea pekee wa CCM. Wapiga kura ambao walikuwa bado wapo vituoni, na hawajapiga kura, ndiyo wamepewa hizo karatasi zenye majina ya wagombea wa vyama vyote. Lakini hujo Luilo, Lifuma, Ludende, mpaka saa 9 mchana hawakuwa wamepelekewa karatasi hizo za marekebisho.

Lifua wamekomaa na kufanikiwa kuzuia mtu yeyote kupiga kura mpaka fomu zenye majina ya wagombea wote zitakapofika.
Nchi inafukarishwa kwa aina ya viongozi na watendaji wa aina hiyo. Hao CCM utulivu wa nchi wamefanya kuwa ni hisani yao kwa watanzania.
Viongozi wa CHADEMA walikuwa sahihi walipowaagiza wananchi kuchukua hatua zinazofaa, inagawa nina uhakika wananchi kutokuwa na uwezobwa kutoa fundisho
 
Back
Top Bottom