Ludewa, Njombe: RC asema wasiolima mazao ya biashara kuwekwa rumande

Ludewa, Njombe: RC asema wasiolima mazao ya biashara kuwekwa rumande

Soko ndio huwa linaamua kuwa wananchi walime au wasilime.Alishawahi ona wananchi wa Uwemba Matola wanalazimishwa kulima viazi?
 
Napenda kilimo lakini siwezi kulima zao ambalo litanifanya niwe mtumwa wa serikali. Kuna watu mwakajana waliwekwa ndani maeneo ya kusini mwa Tanzania, na wengine kuporwa korosho zao kwa kukutwa wakisafirisha kupeleka kwenye masoko waliyoyataka.

Kwa nini uteseke wewe, ugharamie kila kitu wewe, wakati wote, ila wakati wa mauzo, ulichokihangaikia huna uhuru nacho? Kati ya mazao ambao inabidi ufikirie sana kabla ya kuyapanda ni korosho. Mkulima wa korosho awamu amekuwa kama kichwa cha mlevi ambachi hata mwendawazimu hujifunzia kunyoa

Zao la biashara ni zao lolote unaloweza kuuza. Hata mhogo, kama unauuza na unakupa pesa, ni zao la biashara. Sasa huyu DC sijui kama anajua tafsiri hasa ya zao la biashara. Huwezi kumlazimisha mtu alime kahawa wakati humpi shamba, humpi mbegu, hugharimii utunzaji na wala humpi soko.

Mwananchi anaweza kushauriwa mazao ya kulima lakini siyo kulazimishwa. Mkulima anatakiwa kuangalia gharama za uzalishaji, uwepo wa soko na bei ya soko. Kisha anaamua alime zao gani.
 
Mkuu wa wilaya ya Ludewa mkoani Njombe Andrea Tsere ametangaza kumuweka lumande “Lock up” mwananchi yeyote atakayeshidwa kuwa na zao la biashara kutokana na uhamasishaji mkubwa unaoendelea wilayani humo ili kukuza uchumi wa wilaya na wananchi wa wilaya hiyo.

Mkuu wa wilaya hiyo amesema uamuzi huo katika kikao cha hamasa cha wadau/wanaLudewa wanaoishi nje ya wilaya kilichofanyika mjini Njombe, na kutokana na sheria ndogo walizojiwekea ili kuhakikisha kila mtu anakuwa na zao la biashara kwa kuwa wilaya hiyo imekuwa ikikubali mazao mbali mbali ya kibiashara ikiwemo zao la korosho,chai na kahawa hivyo sheria kali zitachukuliwa kwa mwananchi ambaye hataweza kushiriki katika mazao hayo.

“Akiwa Lock up tutakuwa tunamuelimisha umuhimu wa kupanda korosho,akielewa akiahidi kwamba atapanda tutamuachia aende kupanda korosho,lakini kwasababu tumetunga sheria kama ataendelea kuwa mkaidi tutampeleka mahakama ya mwanzo kwasababu kuto kupanda zao la biashara ni ukiukwaji kwa mujibu wa sheria ndogo ya halmashauri na kama watakuwa wengi tutawachukuwa kwa viwango”anasema Andrea Tsere

Amesema mkuu wa wilaya amepewa mamlaka na Rais kwa mujibu wa sheria ya kumuweka mtu yeyote masaa 24 hakutakuwa na swali lolote ni lazima mkaidi apelekwe Lumande kwakuwa ajenda iliyopo kwa sasa ni kujenga uchumi huku mazao hayo yakiwa ni mali yao wananchi
Hakuna njia mbadala ya kuhamasisha wananchi zaidi ya kuwaweka rumande
Hiyo sisi waalimu tunaita kichocheo hasi na chanya
 
Back
Top Bottom