Jack Daniel
JF-Expert Member
- Sep 23, 2021
- 2,912
- 12,904
Kila mtu huwa na Imani fulani kwenye haya maisha,lakini usiweke Imani kubwa kwenye battle ,yaani sehemu ambayo watu wawili ama watatu wanagombea.
Leo timu kubwa yenye mafanikio,mvuto na ya maana Duniani Real Madrid inacheza leo kwenye michuano ya ligi ya mabingwa ulaya.
Ikiwa imemzidi mpinzani wake Salzburg vitu vingi,rate ya mchezaji mmoja mmoja,na haya umaarufu.
Lakini bado hakuna anayekuwa na Imani ya kiasi kikubwa kuweka milioni 1 eti Madrid ashinde.
Lazima kuwe na akiba ya ubongo na maneno pia,hii kitu imemshinda Yeriko Nyerere,anadhani watanzania be wamelala,anadhani ukieneza propaganda unaweza kumshawishi mtu mwenye akili timamu
hata wajumbe walio wengi wamesoma ni nani anatakiwa na wananchi mwisho wa siku box limeamua.
Hongera TUNDU LISSU
Hongera FREEMAN MBOWE
Hongera CHADEMA.
Mmeonesha Demokrasia ya kweli,
Ila mwanakwetu Yeriko Nyerere punguza mdomo.
Umeshindwa kusoma alama za nyakati , umeshindwa kutumia ujasusi wako vizuri mdogo wangu.
Swela hela be myetu.
Pichani ni Yeriko Nyerere akiwa haelewi anavuta Oxygen au Carbon dioxide.