Lugha zetu za asili Tanzania na Herufi za kizungu.

Lugha zetu za asili Tanzania na Herufi za kizungu.

Mafwi Munda

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2017
Posts
1,750
Reaction score
1,603
Habari zenu wana bodi.
Huwa najiuliza maswali lakini sipati majibu lakini leo naomba nanyi mnisaidie.
Tanzania tuna makabila mengi na haya makabila yanaongea lugha tofauti. Lakini pia tunaongea kiswahili. Swali langu ni hili ilikuwaje tuweze kuongea lugha tofauti lakini tukashindwa kuwa au kuweza kuandika hizi lugha zetu kwa HERUFI zetu?! Yani makabila yote tulijua kuongea lakini hakuna hata kabila moja liliweza kuwa na herufi za maandishi yake?! Angalia Ethiopia wana herufi zao,wahindi wana herufi zao,wachina wana herufi zao, warusi wana herufi zao,sweden wana herufi zao waingereza wana herufi zao. Sisi Tanzania tulishindwa au tulitegemea ugunduzi wa wazungu kutuwekea vitu vyetu kwenye kumbukumbu na kwakuwa hawakuziweka kumbukumbu inamaana hatukuwa na herufi zetu kweli?!
Je, tunaweza kutengeneza herufi zetu leo au ugunduzi uliishafungwa?! Ikiwa tunaweza kugundua leo, je kumeshawahi kufanyika utafiti wa kuanza kutengeneza herufi zetu au ugunduzi ni wa kiteknelogia tu lakini sio maandishi(herufi)?!. Kwa wataalam wa tafiti za lugha kumewahi au wamewahi kuona herufi zozote za kuwakilisha maandishi ya kabila lolote Tanzania?! Je kuna wataalam wale wanaoitwa ma anthropologist wa lugha?! Je wamewahi kutafiti herufi za kuwakilisha mawasiliano ya kimaandishi ya lugha yoyote ya makabila yetu Tanzania?!
Kwa BAKITA kiswahili tunaweza kukiundia herufi zetu mbali ya hizi A to Z?! Je kuna juhudi hizo au mnakuza lugha tu herufi zina mamlaka yake?!
Ni mjadala wa wote kwa yeyote anayejua chochote kuhusiana na hili. Karibuni kwa mjadala.
 
Swali fikirishi sana.

Hakuna lugha yenye asili ya kibantu iliwahi kugundua aina yake ya uandishi wa maneno.

Ni kweli kuanzia enzi kwa wagiriki, wayunani, warumi, waethiopia, Waarabu na hata baadhi ya nchi za ulaya kama ufaransa na ujerumani pia wana aina yao ya uandishi.

Kwa upande wa Kiswahili kuna zile IRABU (a, e, i, o, u) ila nahisi pia zina uhusiano na English Alphabets.

Kwa upande wa Wamasai wao wana baadhi ya matamshi ambayo hayaandikiki, mfano jinsi anavyotamkwa "Baba"

Lakini pia wao wana gestures za namba bila kutamka maneno.

Ngoja Waje wakina Chomsky watusaidie hapa.
 
Habari zenu wana bodi.
Huwa najiuliza maswali lakini sipati majibu lakini leo naomba nanyi mnisaidie.
Tanzania tuna makabila mengi na haya makabila yanaongea lugha tofauti. Lakini pia tunaongea kiswahili. Swali langu ni hili ilikuwaje tuweze kuongea lugha tofauti lakini tukashindwa kuwa au kuweza kuandika hizi lugha zetu kwa HERUFI zetu?! Yani makabila yote tulijua kuongea lakini hakuna hata kabila moja liliweza kuwa na herufi za maandishi yake?! Angalia Ethiopia wana herufi zao,wahindi wana herufi zao,wachina wana herufi zao, warusi wana herufi zao,sweden wana herufi zao waingereza wana herufi zao. Sisi Tanzania tulishindwa au tulitegemea ugunduzi wa wazungu kutuwekea vitu vyetu kwenye kumbukumbu na kwakuwa hawakuziweka kumbukumbu inamaana hatukuwa na herufi zetu kweli?!
Je, tunaweza kutengeneza herufi zetu leo au ugunduzi uliishafungwa?! Ikiwa tunaweza kugundua leo, je kumeshawahi kufanyika utafiti wa kuanza kutengeneza herufi zetu au ugunduzi ni wa kiteknelogia tu lakini sio maandishi(herufi)?!. Kwa wataalam wa tafiti za lugha kumewahi au wamewahi kuona herufi zozote za kuwakilisha maandishi ya kabila lolote Tanzania?! Je kuna wataalam wale wanaoitwa ma anthropologist wa lugha?! Je wamewahi kutafiti herufi za kuwakilisha mawasiliano ya kimaandishi ya lugha yoyote ya makabila yetu Tanzania?!
Kwa BAKITA kiswahili tunaweza kukiundia herufi zetu mbali ya hizi A to Z?! Je kuna juhudi hizo au mnakuza lugha tu herufi zina mamlaka yake?!
Ni mjadala wa wote kwa yeyote anayejua chochote kuhusiana na hili. Karibuni kwa mjadala.
Mkuu hujachelewa,dunia ndo kwanza inamiaka 2017 anza kutengeneza tu hizo herufi za kiswahili hadi kufikia mwaka 8017 itakua ishaeleweka
 
Ila pia kumbuka kuwa Watu weusi wenye asili ya kibantu (wenye pua kubwa na lips pana) ndio wanaoongoza kwa kusubiri kutafuniwa kiila kitu.

Hawana asili ya Ubunifu (Innovation), Ugunduzi (Discovery) wala Uvamizi kwa nia ya utawala / ushikaji dola (Conguering).

Ni kama watu hawa waliumbwa ili kutawaliwa na kuwatumikia Wazungu, Waarabu, Wahindi na hata Wachina...na mpaka leo ni Watumwa kwa races hizo na ushahidi upo wazi.
 
Mada yako ina confuse sana, au sijui mimi ndio sijakuelewa (plz utanielekeza)
unaposema tubadili herufi lakini papo hapo tunatumia maneno kama
Mama,
Baba,
Chakula,
Dawa,
Kichwa,
Goti,
Zawadi,
n.k

Haya maneno yanatokana na herufi za A,B,C,D......
Sasa unaposema tubadili herufi na tuunde za kwetu kama India, Urusi na China ina maana tubadili lugha ya kiswahili kwa kuleta lugha nyingine yenye herufi zingine au ulikusudia nini hapo kwenye 'herufi za kizungu na zetu'???
 
Sawa bana, hizi lugha kweli "tusi kwangu kwako jina" haya mkuu ila umenielewa,

Ngoja wajuvi waje washuke kwenye mada yetu au yako hapo kwa hoja bila uwoga.
Lakini still sio tusi, labda tafsiri tu.
 
Mada yako ina confuse sana, au sijui mimi ndio sijakuelewa (plz utanielekeza)
unaposema tubadili herufi lakini papo hapo tunatumia maneno kama
Mama,
Baba,
Chakula,
Dawa,
Kichwa,
Goti,
Zawadi,
n.k

Haya maneno yanatokana na herufi za A,B,C,D......
Sasa unaposema tubadili herufi na tuunde za kwetu kama India, Urusi na China ina maana tubadili lugha ya kiswahili kwa kuleta lugha nyingine yenye herufi zingine au ulikusudia nini hapo kwenye 'herufi za kizungu na zetu'???
Kwa nilivyomwelewa, anazungumzia kuwa na herufi rasmi za lugha yetu.

Mfano hilo neno Mama au Dawa ina herufi zile zile zilizopo katika consonanti za kizungu A, B, C, D... kuendelea.

Wajerumani wana S`, waethiopia wana kiaramaic, Warumi wana kirumi hata katika namba. Mfano i , V, X, C, M, Waarabu wana maneno yao yaandikwayo kutoka kulia kwenda kushoto etc.

Wabantu je wana herufi zipi za kwao?
 
Mkuu hujachelewa,dunia ndo kwanza inamiaka 2017 anza kutengeneza tu hizo herufi za kiswahili hadi kufikia mwaka 8017 itakua ishaeleweka
Nashukuru kwa ushauri wako mkuu. Ningeweza kuanza hiyo kazi lakini nasikitika mimi sio mtaalam wa lugha, ila niliingiwa na mawazo kila nikiona lugha zingine wana herufi zao nikaona niulize nisije nikafanya kazi ambayo wajuzi wameshaifanya au wanaifanya.Na ikiwa bado still inaweza kuleta mshawasha kwa wataalam kufikiria namna ya kuanza. Mimi sitokuwa mtu sahihi kufanya utafiti huo labda niwe mbeba mabox ya mtafiti, au kusaidia kuandika questionnaire. Ila najua wapo wataalam wa mambo haya watatusaidia au iko siku wakiandika thesis zao jamii forum tutakua quoted.
 
Kwa nilivyomwelewa, anazungumzia kuwa na herufi rasmu za lugha yetu.

Mfano hilo neno Mama au Dawa ina herufi zile zile zilizopo katika consonanti za kizungu A, B, C, D... kuendelea.

Wajerumani wana S`, waethiopia wana kiaramaic, Warumi wana kirumi hata katika namba. Mfano i , V, X, C, M, Waarabu wana maneno yao yaandikwayo kutoka kulia kwenda kushoto etc.

Wabantu je wana herufi zipi za kwao?

Wabantu
Lakini still wana herufi zao kutokana na lugha yao, mfano kabla hakijaja kiswahili lugha za kibantu wao walikua na herufi gani za lugha zao??
 
Kwa nilivyomwelewa, anazungumzia kuwa na herufi rasmu za lugha yetu.

Mfano hilo neno Mama au Dawa ina herufi zile zile zilizopo katika consonanti za kizungu A, B, C, D... kuendelea.

Wajerumani wana S`, waethiopia wana kiaramaic, Warumi wana kirumi hata katika namba. Mfano i , V, X, C, M, Waarabu wana maneno yao yaandikwayo kutoka kulia kwenda kushoto etc.

Wabantu je wana herufi zipi za kwao?

Wabantu
Asante kwa ufafanuzi mkuu.
 
Mada yako ina confuse sana, au sijui mimi ndio sijakuelewa (plz utanielekeza)
unaposema tubadili herufi lakini papo hapo tunatumia maneno kama
Mama,
Baba,
Chakula,
Dawa,
Kichwa,
Goti,
Zawadi,
n.k

Haya maneno yanatokana na herufi za A,B,C,D......
Sasa unaposema tubadili herufi na tuunde za kwetu kama India, Urusi na China ina maana tubadili lugha ya kiswahili kwa kuleta lugha nyingine yenye herufi zingine au ulikusudia nini hapo kwenye 'herufi za kizungu na zetu'???
Kuna mdau katoa jibu zito la maswali yako. Kuna tofauti ya kuongea/matamshi na kuandika. Haya maumbo ya herufi ndio nataka kufahamu sisi hatukuwa na yetu?! Je tunaweza kuyatengeneza leo?! N.k
 
Back
Top Bottom