Lugha zetu za asili Tanzania na Herufi za kizungu.

Asante mkuu kwa marekebisho, na maelezo yako. Nia yangu nikujifunza hivyo napokea maelezo yako mkuu.
 
Mkuu nashukuru kwa maandiko yako nahisi kuna kitu unafahamu kuhusu hili. Umeongelea gestures za kimasai zinazotambulisha namba zoote, je zina maumbo ya herufi kuziwakilisha au bado nao kama makabila yetu licha ya wao kutokuwa wabantu?!. Kuna mtu kaniambia hata Waluo au wajaluo sio wabantu. Lakini ingawa kesi yangu ni lugha still bado sielewi vizuri kuhusu huu ubantu pia. Ubantu ni nini ni rangi nyeusi au ni umbo la sura au ni uafrika au nini?! huku juu uliongea kuhusu wabantu kutokuwa wavumbuzi na ni watu wa kutafuniwa. Mi mwanzo nilidhani ubantu ni uafrika. Lakini ulisema Waethiopia na Wa misri wa zamani wanamaandishi yao. Waethiopia nafahamu kuhusu kiaramic lakini hawa wa misri wa zamani lugha yao siifahamu na wala sijawahi kuona maandishi yao pia.
Nimetafutatafuta, na kuuliza watu mbalimbali sikupata lugha nyingine Afrika yenye herufi zake zaidi ya waethiopia.Umesema waethiopia sio wabantu, sijui ni watu gani lakini sipati picha hata makabila jirani yao hawakuwa na maandishi. Inawezekana zamani hata kuigilizia na kubadili kidogo haikuwa rahisi.
Sijawahi kufika amboni mapangoni, hiyo michoro iliyoko huko ni ya wanyama tu au kuna maandishi ya alama za kuwakilisha lugha pia?!. Nimetafuta mawasiliano ya anthropologist wakitanzania niwaulize huko kwenye fani hii kumewahi kuwa na tafiti ya herufi za lugha zetu za asili au la, bado nasubiri.
 
Mkuu Mkazamoyo nakubaliana nawe tena. Hawa watu weupe waliweza kutuandikia historia yetu. Sisi bado tupo na tuna tamaduni zetu za asili kikabila achana na kitaifa. Lakini nimeona siku hizi hata vile vitu tulivyoweza kwa muda mrefu sasa tumeviacha kwa sababu ya tekinologia, mfano vyungu vya kupiakia vyakula, mitungi ya kuhifadhia maji, maghala ya kiasili ya kuhifadhia chakula, mikeka na majamvi ya kukalia na kulalia, vitanda vya kamba(teremka tukaze), kawa za kufunikia vyakula, bakuli za kupakulia ugali na vingine vingi. Huko mbele tutalaumu wazungu pia lakini malighafi zipo soko lipo miongoni mwetu lakini tumeacha uasili wetu kwa kurahisishiwa na hizi tekinologia za wazungu.
Mimi namshukuru mungu lugha zetu bado tunazo na bado tunaziongea, ni muda sasa kurecord mazungumzo ya lugha zetu za asili na kuzihifadhi kitaalam ili huko baadaye zikipotea kumbukumbu iwepo. Leo hatuna herufi za matamshi ya lugha zetu tuna dai labda kumbukumbu zilipotezwa wakati wa vita na mkoloni au sisi wenyewe kwa wenyewe. lakini hizi lugha na matamshi yetu tungefanya juhudi ya kuyahifadhi. Sijui ni nani mwenye jukumu hili lakini kama taifa huo ndio utamaduni wetu uliobaki naweza kusema. Ngoma za asili hazina mvuto tena, midundo ya ngoma na uchezaji wetu hauna mvuto tena kwetu wenyewe, tunafurahi wazungu wakija wakaona na kutusifia lakini hatujali pekeyetu ikiwa mzungu hajapenda. Wizara ya utamaduni inaweza kuwa imeshalifanya hili au bado lakini nadhani huu ndio muda. Wazungu wana kusanya vinasaba/genes za kila watu, wanyama, hadi wadudu wa kubwa na tusiowaona wana Genes na DNA bank wanatanya tafiti wakiwa na data za kuanzia. Wanatafuta genes na DNA za Dinosaur ili wajaribu kuwarudisha wakiweza. Sisi kama taifa hatuna data base ya vitu vyetu nasi tuna copy wao wanafanya nini tunaiga. Tunapenda ku copy na kuiga reserach zao na kupaste kwetu na kujiita watafiti. kwanini tusifukunyue vyetu wao waige. Najua vyetu havitakuwa funded kwasababu reserch zetu zinategeme pesa zao pia. Nani athubutu hapa kwetu?! Wamarekani hata metric system za dunia wamekataa kuzifuata wanatumi zao. sisi hata mivchezo yetu ya asili tunataka tutumie sheria za wazungu. Niliona wazungu wameandika sheria za kucheza Bao, mchezo wetu wa asili. Sisi ni nani au nini mpaka tusiweze chochote?!
 
Hili la Fuvu la kwanaza siwezi kufahamu lilikuwa la mbantu au sio mbantu. Lakini niliwahi kusoma sehemu wakidai ni la mtu mweusi, sasa sijui inamaanisha nini ingawa kwa imani yangu eti mbantu ni mtu mweusi na kinyume chake , naweza kukosolewa lakini. Ingawa kama ilivyosemwa hata historia yetu imeandikwa na weupe ni ngumu kuamini au kujua ukweli ni nini au ni upi. Huwa naamini sisi binadamu wa leo hatuko pure kabisa nahisi tuna genes za asili tofauti tofauti bila kujali rangi zetu. Huwa siamini leo utakuta mzanaki pure yaani hajachanganyika na genes za mabalila ya jirani ingawa zote ni nyeusi zenye kufanana kwa karibu kila kitu lakini still naamini bado tumeshachanganyikana sana. Kuna mtu kuongea lugha ya asili fasaha lakini genetically anaweza asiwe pure.
Hivi tukiacha huu ubantu na uthoolite na uzungu. Leo hii kama tunavyoandika hapa, unadhani tunaweza pata maumbo ya sauti za matamshi ya lugha zetu za asili, kutoka kwa wataalam wetu ndani au wa nje?! Au kwa ufahamu wako umewahi kuona tafiti za maumbo ya herufi ya lugha yoyote duniani ukiacha marekebisho ya lugha zilizopo tayari?.
 
Wamasai katika mazungumzo ya lugha yao wanaambatanisha pia na gestures au alama inayotambulisha namba (nafikiri zote). Hizo namba nina uhakika ni ya kwao pekee waliobuni wao pekee tangu enzi na enzi.

Kwanini nimesema hivyo? Ni kwasababu sio Wazungu, Wahindi, Wachina ama Makabila yooote ya kibantu yanatumia hizo gestures zao.

Kwahiyo tayari wao wana asili yao ya Ubunifu wa ishara za mawasiliano zaidi ya sauti pekee ila si Kiuandishi.

Kuhusu lugha ya kimasai pia nikitrace origin yao sioni zikifanana saaana na kiaramaic ila najua zina asili moja kabisa, hivyo tayari sina ushahidi kuwa kimasai kimekopa maneno kokote kama kilivyo kiswahili na kiingereza.

Hiyo inanifanya nikubali na kuamini kuwa Wamasai tangu enzi na enzi walikuwa wakijisimamia na kuenzi asili yao katika:-

-Lugha
-Mavazi
-Chakula
-Organization / mfumo wa utawala wa kirika (Age-set)
- Style ya maisha kwa ujumla wake.


2) Wabantu ni akina nani?

Ni watu wa Afrika (zamani ikiitwa Ethiopia) ambao wana asili ya kutokea eneo la milima ya Cameroon kwa miaka mingi iliyopita.

Kimuonekano wanaelezewa kuwa weusi, wenye asili ya kunenepa, wenye uso mpana, pua na lips pana, tofauti na wakush, wanilotes etc.

Hawa wabantu walikuja kusambaa katika Afrika yote (kasoro sehemu zilizokaliwa tayari na waarabu, wanilotes, wakush etc.)

Wabantu walioenda upande wa kusini ndio hawa ambao babu zao waliwaza kina Shaka wa Zulu etc

Wabantu wengine waliishi ktkt ya Africa ambao babu zao ndio walioianzisha Zimbabwe ya kina mugabe

Wabantu wengine walibaki cameroon, Ghana, Mali etc

Wengine walienda zaire / congo

Wabantu wengine wakaja mashariki ya Africa na ndio waliozaa makabila ya huku.

Ubantu ulikuja kusababisha aina nyingi sana za Makabila ya asili kama kihaya, kigogo, kipare n.k... ILA historia inakumbusha neno "NTU" kama ndio lugha ya kibantu ikimaanisha Mtu au Binadamu.

Wabantu wa mashariki ya Afrika walipokuja kuungana na Waarabu na Wareno kwasababu ya Dini, Ukoloni au Biashara walizalisha lugha nyingine inayoitwa KISWAHILI lakini uandishi wake si wa kiarabu ila ni wa wazungu waliokuja kufunza watu weusi namna ya kuandika.

● Hivyo kwa mtazamo wangu na uelewa wangu, UBANTU na MAKABILA YAKE haujawahi kugundua namna yake ya mawasiliano (ya kimaandishi au kiishara) zaidi ya SAUTI TU.

Aina za maandishi iliambatana na Formal Education ambayo wabantu waliletewa na Wageni (Wazungu) na aina nyingine ni kiarabu, na hata kirumi katika namba ambazo zinafundishwa katika shule za msingi.

Mfano baada ya kusoma One, two, three mpaka a thousands and Millions tukaambiwa tena ni vizuri tujue haya:

X ni 10
C ni 100
M ni 1000
V ni 5

Hahahaha [emoji23]

Kuna maneno nitakayoyaamini siku zote kuwa:

"Mtu akishaweza kutawala UTAMADUNI WAKO basi amekutawala kila kitu"

Hiki ndicho wakichokifanya watu weupe kwa Wabantu tangu enzi na enzi.


....x.....x......x.....x.....x......x......x.....
 
Samahani,mimi hoja yangu iko nje kidogo ya mada ila inahusu usahihi wa lugha hiihii ya kiswahili.Kwa muda mrefu sasa kiasi cha kuwa mazoea na kuonekana ni sahihi kwa baadhi ya maneno ya kiswahili yanaoongelewa tofauti na usahihi wake (labda kama mimi ndo nitakuwa siko sahihi,nafaso ya kunirekebisha iko wazi na nitashukuru)
1.Kwanini watu husema "Ng'ombe hizi au ng'ombe nyingi BADALA ya "Ng'ombe hawa au ng'ombe wengi?

2.kama pia ilivyo kwa "samaki/dagaa hizi" BADALA ya samaki/dagaa hawa?
 
Ni kutokana na kutofahamu tu namna ya kutamka maneno fasaha ya lugha ya kiswahili ama kukusudia au wengine ni mazoea tu.
 
Ni kutokana na kutofahamu tu namna ya kutamka maneno fasaha ya lugha ya kiswahili ama kukusudia au wengine ni mazoea tu.
Azarel nakubaliana na wewe,kiukweli mazungumzo mengi ya kiswahili huwa yanakosewa kiasi cha kuudhi kabisa,nilichefukwa kumsikia waziri mmoja kwenye chombo cha habari akisema "tumezikamata ng'ombe kutoka kenya".Kiukweli hii sio sawa basi tu inakosewa kwa makusudi au kutojua
 
Nchi ambazo hazikutawaliwa mf ethiopia, ndizo nchi ambazo zina maandishi (heruhi ) zao zenyewe. Zoye zilizotawaliwa na kupata uhuru baadae ziliendeleza mifumo ile ile ya elimu ya aliyekuwa bwana wake. Mfano nchi nyingi za jangwa la sahara wanatumia kiarabu nk. Ethiopia wanatumia amharic na wana herufi zao
 
Bwana una mawazo ya ajabu! Mabantu walikuwa hodari sana katika ugundizi maana walitoka kiasili sehemu ya Kamerun wakagundua Tanganyika hadi Afrika Kusini, baada ya kufaulu kuvuka beseni ya Kongo penye mazingira magumu sana. Ukiwa na wasiwasi kuhusu uvamizi (ingawa sioni sifa za uvamizi maana ni mauaji na kupora) basi ujiulize hao wa Songea walifika namna gani?

Kuhusu ubunifu Wabantu walibuni mengi, pamoja na kilimo na teknolojia ya chuma. hawakuwa watu wa pekee waliobuni teknolojia hizi lakini walijitegemea katika hatua hizi.

Menginevyo wazee hao waliishi katika jamii ndogo sana, kabla ya ukoloni Tanzania ilikuwa na watu wachache. kama jamii ni ndogo hakuna haja ya kuanza mbinu za kuandika. Uchumi wao katika mazingira jinsi ilivyokuwa haukuhitaji kumbukumbu ya kimaandishi. Hapo naona sababu ya kutotumia mwandiko.
 

Habari zako mkuu !
Mié sio mweledi sana wa tasnia hii Ila tujue tu kuwa nchi za Ulaya za magharibi , ukitoa Ugiriki, wanatumia herufi za kilatini, wakifanya marekebisho kidogo kuendana na sauti zao ( mfano ; ç kwa Kifaransa na kikatalani, ß ambayo ni sawa n'a ss kwa Kijerumani, ukienda kule skandinavia wao pia wana ø na herufi nyengine Kama hizo).

Afrika kwa asilimia kubwa hatuna herufi zetu ukitoa makabila/ jamii chache zenye nazo.

Mfano ni Geez za Uhabeshi(Ethiopia) na Eritrea. Ukienda kule Afrika kaskazini zipo herufi za tifinag za jamii za Berber n'a Tuareg. Sina ujuzi wa herufi zaidi ya hizo.

Ukienda nje ya Afrika, Amerika kabla ya kufika wakolini, pia hawakua na herufi zao.

Labda hii ilitokana na jamii kutohitaji maandishi kwa maana Hao walioona uhitaji huo wakaanzisha herufi zao.

Mchango wangu Mdogo tu ni huo.

Wasalam.
 
Mada hii imekosa wachangiaji kabisa?!

Hii Mada ni nzuri sana. Tatizo ninavyoona ni kwamba ama hatuna wataalamu wa mambo ya kale waliojikita kwenye Lugha zetu hasa upande huo wa maandishi na herufi, Au wapo ila si unajua vitabu walivyosoma na wanavyosoma ni vya wageni.

Labda niulize kaswali kadogo Chuo chetu Kikuu na Kikongwe hakina Kitivo cha mambo ya Kale ?
 
Nilichojifunza kwa hawa wataalam wa mambo ya kale wamegawanyika sana Kuna Anthropologist wa lugha, wapo wa biologia na mambo mengine. Lakini kujibu swali lako Sina uhakika kama UDSM au chuo kingine Tanzania tunao hawa watu. Na labda tunao na wameshalifanyia kazi lakini tutajuaje ikiwa hatufahamu wamepublish wapi hizo taarifa. labda kama wewe mwenzangu unataarifa za Journal wanayo publish paper za tafiti zao. Lakini pia kama ulivyosema, tunasoma vitabu vilivyoandikwa na wazungu ili ku qualify kielimu kwa level za juu hasa, hivyo sidhani kama kuna vitabu vyetu vyenye maandishi yetu kwa herufi zetu, maana hazipo au hatuzifahamu.
 
Mkuu Nanye GO, siku nikienda Dar es salaam nitajaribu kupita pale Kijiji chetu cha Makumbusho labda naweza kuambulia mawili matatu ya utangulizi.
 
Mkuu Nanye GO, siku nikienda Dar es salaam nitajaribu kupita pale Kijiji chetu cha Makumbusho labda naweza kuambulia mawili matatu ya utangulizi.
Niwazo zuri jaribu tuone kama wanakumbukumbu za herufi zilizotumiwa na watangulizi wetu kuwasiliana, maana huo unaweza kuwa mwanzo wa kutafuta herufi za makabila mengine. Wachina wameleta program za kichina vyuo vyetu,tunajifunza na tunashangilia kufahamu kichina. Lakini unaweza kukuta mtu awezi au hafahamu kuongea lugha ya asili ya/za wazazi wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…