Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Mpina, ameitaka Serikali kueleza kwa nini mikataba ya uwekezaji wa Bandari ya Dar es Salaam na kampuni ya DP World haijawasilishwa Bungeni ili wabunge waweze kujua maudhui yaliyokubaliwa kwenye mikataba hiyo.
Akiwasilisha hoja yake wakati wa kujadili Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2025/2026, Mpina ameeleza kuwa, kwa mujibu wa Sheria ya ‘Natural Resources, kifungu cha 12, mikataba ya aina hiyo inapaswa kuwasilishwa Bungeni.
Soma, Pia: Luhaga Mpina arejea Bungeni kwa mara ya kwanza baada ya kumaliza adhabu yake ya sakata la Sukari
Amelitaka Bunge kufahamu nani aliyekubali uwekezaji wa Shilingi bilioni 687 na makubaliano ya mgawo wa mapato ya asilimia 40 kwa 60 kati ya Tanzania na DP World.
Mpina amesema, "Nani aliyekubali kwamba sisi tunakubali uwekezaji wa Bilioni 687, nani aliyekubali kwamba sisi tumekubali rate ya kugawana mapato na DP World kwa ratio ya 40 kwa 60? Nani aliyekubali?"
Akiwasilisha hoja yake wakati wa kujadili Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2025/2026, Mpina ameeleza kuwa, kwa mujibu wa Sheria ya ‘Natural Resources, kifungu cha 12, mikataba ya aina hiyo inapaswa kuwasilishwa Bungeni.
Soma, Pia: Luhaga Mpina arejea Bungeni kwa mara ya kwanza baada ya kumaliza adhabu yake ya sakata la Sukari
Amelitaka Bunge kufahamu nani aliyekubali uwekezaji wa Shilingi bilioni 687 na makubaliano ya mgawo wa mapato ya asilimia 40 kwa 60 kati ya Tanzania na DP World.
Mpina amesema, "Nani aliyekubali kwamba sisi tunakubali uwekezaji wa Bilioni 687, nani aliyekubali kwamba sisi tumekubali rate ya kugawana mapato na DP World kwa ratio ya 40 kwa 60? Nani aliyekubali?"