Luhaga Mpina ataka Bunge lipitishe sheria ya kunyonga mafisadi na wezi wa fedha za umma

Nafikiri hata yeye pia ni kati ya watakao liwa kichwa!
Na yeye ni mmojawapo ila hapo anaongea tu ili kuwafurahisha wananchi wamuone mwema.
Kama yuko serious na ni mzalendo wa kweli apiganie mishahara ya wabunge ipunguzwe hela zipelekwe mahospitalini.
 
Yeye nwenyewe atanyongwa zile shamba ekari 1000 analipa kodi kweli.
 
Kwa hapa tulipofikia, hakuna namna, ni lazima hatua stahiki stahiki zianze kuchukuliwa dhidi ya ufisadi na mafisadi.

Imefikia kiwango hata ripoti za CAG na ya ile TAKUKURU hakuna anayezijali tena, ijapikua zinakabidhiwa kwa mbwembwe kwa watawala.

Ripoti hizi zinataja maeneo kadhaa yanayotiliwa shaka sana katika upigaji wa wazi, lakini si Bunge wala serikali vyenye kuonyesha shahuku ya kuwashighulikia wala rushwa na mafisadi wachache wakiogelea katika ukwasi mkubwa hapa nchini, huku wengi wa Watanzania wakitopea katika umaskini wa kurisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…