Pre GE2025 Luhaga Mpina: Baadhi ya Viongozi wa Serikali wanahusika kutorosha fedha

Pre GE2025 Luhaga Mpina: Baadhi ya Viongozi wa Serikali wanahusika kutorosha fedha

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Kivumbi tu! Kutoka kwa Mpina, anaendelea kutapika nyongo haswa

Ila huyu jamaa ni tofauti sana na wanaCCM wengine yani aogopi kupiga panapo stahili
================
Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Mpina, amesema Tanzania inakabiliwa na changamoto kubwa ya utakatishaji wa fedha haramu, hali inayoiweka nchi kwenye hatari ya kuingizwa katika orodha ya uangalizi maalum wa Kikosi Kazi cha Kimataifa cha Kudhibiti Utakatishaji wa Fedha (FATF).

Akizungumza na wanahabari kuhusu maoni yake kwa Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi, Mpina amebainisha kuwa Tanzania inapoteza takriban dola bilioni 1.5 za Kimarekani (sawa na shilingi trilioni 3.3) kwa mwaka kutokana na utoroshaji wa fedha kwenda nje ya nchi.

Soma Pia: Luhaga Mpina: Wanaomsifia Rais Samia ndio hao wanaoongoza kwa kumhujumu na kufanya uovu

Ameeleza kuwa hivi karibuni kumekuwa na madai ya utoroshaji mkubwa wa fedha unaofanywa na baadhi ya viongozi na watendaji wa serikali, akisisitiza umuhimu wa kuchukua hatua madhubuti ili kudhibiti tatizo hilo na kulinda uchumi wa taifa.

 
Machawa ñi wazi mnaongozwa na matumbo ,kichwani mkiwa weupe pee pee !!.

Lai yangu kwenu, Kila Eneo aloligusa MPINA , mkalifatilie ,mchimbe Kwa undani ,mjipe maarifa kwanza .

Mkishindwa kufanya hivo, Basi kaaeni tu Kimya, mlichukie Hilo kama Darasa.
 
Nilipost humu namna pesa hutoroshwa nje, Wasanii/watu wa ovyo wote wanaosafiri na viongozi(Pengine na Rais) wanakuwa wanatumika kusafirisha pesa.

Mfano Safari za Dubai, kuna ile Safari rais alisafiri na wasanii kwenda Korea
 
Machawa ñi wazi mnaongozwa na matumbo ,kichwani mkiwa weupe pee pee !!.

Lai yangu kwenu, Kila Eneo aloligusa MPINA , mkalifatilie ,mchimbe Kwa undani ,mjipe maarifa kwanza .

Mkishindwa kufanya hivo, Basi kaaeni tu Kimya, mlichukie Hilo kama Darasa.
Lucas Mwashambwa njoo ububujikwe na machozi jumla na rejareja, mama yako hatakiwi LUMUMBA
 
Back
Top Bottom