Pre GE2025 Luhaga Mpina: Sitakaa kimya dhidi ya Ufisadi na Matumizi Mabaya ya Fedha za Umma

Pre GE2025 Luhaga Mpina: Sitakaa kimya dhidi ya Ufisadi na Matumizi Mabaya ya Fedha za Umma

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mbunge wa Jimbo la Kisesa, mkoani Simiyu, Luhaga Mpina, amesema hatakaa kimya wakati baadhi ya watu wakiendelea kuendeleza ufisadi na matumizi mabaya ya fedha za umma, hali inayorudisha nyuma maendeleo ya wananchi.

Soma Pia:
Mpina ameyasema hayo wakati akizungumza na mamia ya wananchi katika Jimbo la Mbogwe, ambako alikuwa mgeni mwalikwa wa Mbunge wa jimbo hilo, Nicodemas Maganga.

 
Mnafiki tu huyu, mbona kipindi CAG anazuiliwa kuwakagua TGFA na SGR huyu Mpina hakuinua mdomo?
 
Mama kama alivyo fanya Tanga kwa Januari alifikirie kwa Mpina siku akifanya ziara huko!
 
Mbunge wa Jimbo la Kisesa, mkoani Simiyu, Luhaga Mpina, amesema hatakaa kimya wakati baadhi ya watu wakiendelea kuendeleza ufisadi na matumizi mabaya ya fedha za umma, hali inayorudisha nyuma maendeleo ya wananchi.

Mpina ameyasema hayo wakati akizungumza na mamia ya wananchi katika Jimbo la Mbogwe, ambako alikuwa mgeni mwalikwa wa Mbunge wa jimbo hilo, Nicodemas Maganga. Alisema anampongeza Maganga kwa kusimama kidete dhidi ya wizi na ufisadi unaofanywa na watu wasiokuwa na mapenzi mema na nchi.

Kwa upande wake, Mbunge wa Mbogwe, Nicodemas Maganga, alisema wilaya hiyo imepiga hatua kubwa za kimaendeleo licha ya changamoto za upinzani kutoka kwa baadhi ya watu wanaopinga juhudi zake za kutekeleza ilani ya chama tawala.

 
Mbunge wa Jimbo la Kisesa, mkoani Simiyu, Luhaga Mpina, amesema hatakaa kimya wakati baadhi ya watu wakiendelea kuendeleza ufisadi na matumizi mabaya ya fedha za umma, hali inayorudisha nyuma maendeleo ya wananchi.

Soma Pia:
Mpina ameyasema hayo wakati akizungumza na mamia ya wananchi katika Jimbo la Mbogwe, ambako alikuwa mgeni mwalikwa wa Mbunge wa jimbo hilo, Nicodemas Maganga.

🔴CCM Ilikuwa na Dhamira Njema, Lakini Wana CCM Wameisaliti

CCM ilipozaliwa mwaka 1977, tuliikusanya kutoka kwa TANU na ASP, tukisema hiki ni chama cha wakulima na wafanyakazi! Hii haikuwa maneno matupu. Ilikuwa imani. Ilikuwa dhamira. Tuliweka msingi wa ujamaa na kujitegemea tukiamini kuwa taifa letu halitaachia rasilimali zake zichezewe na wachache. Tukasema kwamba serikali ya chama lazima ihakikishe uchumi unamnufaisha kila Mtanzania, si wachache wenye nguvu ya fedha!

Lakini leo, naona CCM inaishi kwa jina tu. Wanaosema ni chama cha wakulima na wafanyakazi ni wao kwa maneno, lakini kwa vitendo, chama kimekuwa cha wachache wenye fedha na ushawishi wa kisiasa. Wamekiuka misingi yao wenyewe.

🔴Katiba ya CCM Inasemaje, na CCM Inafanya Nini?

Katika Ibara ya 9 ya Katiba ya CCM, chama kiliahidi kusimamia ujamaa na kujitegemea, kuhakikisha kuwa rasilimali za nchi zinawanufaisha wananchi wote. Tukasema taifa hili lazima lijitegemee kwa kilimo chake, viwanda vyake, na kazi za wananchi wake.

Lakini leo, watu wale wale waliokabidhiwa chama wamekiuka ahadi zao wenyewe:

Madini yanachimbwa na wageni, wenyeji wanabaki watazamaji.

Mashamba yanaota magugu, wakulima hawana pembejeo, hawana masoko.

Mashirika ya umma yameuzwa kwa bei ya kutupwa, halafu serikali inarudi kuyakomboa kwa gharama kubwa!

Ajira kwa wafanyakazi imekuwa ndoto. Vijana wanahangaika huku nchi ikikumbatia wawekezaji wa kigeni badala ya kuwaendeleza wazawa!

Ndugu zangu, hii siyo CCM tuliyoianzisha. Hii ni CCM ya matumbo ya watu wachache!

🔴Ubinadamu na Ubinafsi: CCM ya Leo Imeongozwa na Tamaa

Kuna tofauti kati ya ubinadamu na ubinafsi. Binadamu anatakiwa kujali wenzake, kuhakikisha kila mmoja anapata haki yake. Lakini ubinafsi ni sumu inayowafanya wachache wale, wengi wabaki na njaa. Leo CCM haiongozwi tena na utu. Inaongozwa na tamaa ya mali na madaraka.

Ujamaa haukuwa mzigo. Ujamaa ulikuwa njia ya kuhakikisha kila Mtanzania anafaidika na rasilimali za nchi yake. Lakini sasa, sera za uchumi zimegeuzwa kuwa biashara za wachache. Serikali inashindwa kusimamia rasilimali kwa sababu waliopo madarakani hawajali tena misingi ya chama. Wamekaa meza moja na wenye fedha, wamesahau maskini waliowapa uongozi.

🔴Wanachama wa CCM Wamegeuka Mashabiki Badala ya Wasimamizi

CCM ingekuwa na nguvu kama wanachama wake wangekuwa waangalizi wa nidhamu ya viongozi wao. Lakini leo, wanachama wa CCM siyo tena walinzi wa rasilimali, wamekuwa mashabiki wa viongozi wabovu!

Wanaimba majina ya viongozi badala ya kuwauliza wanatekeleza vipi misingi ya chama.

Wanapiga makofi kwa wale wanaovunja katiba yao wenyewe.

Wanapigia kura wale wanaouza nchi badala ya wale wanaoijenga.

Chama chenye wanachama wa aina hii hakina uhai. Kimebakia kama nembo tu, kama bendera inayopepea kwa upepo wa fedha na siyo upepo wa uzalendo.

🔴Je, CCM Bado ni Chama cha Wakulima na Wafanyakazi?

Leo, mtu akiniuliza je, CCM bado ni chama cha wakulima na wafanyakazi? Ningemuuliza:

Mkulima yuko wapi katika mipango ya CCM?

Mfanyakazi anafaidika vipi na rasilimali za taifa?

Kwa nini mikataba ya madini, gesi, na mafuta haijawahi kuwekwa wazi kwa wananchi?

Kwa nini serikali inalia kuhusu ajira lakini haina mpango wa kuhakikisha viwanda vya ndani vinaajiri watu?

CCM imekwepa maswali haya kwa sababu haina majibu.

🔴Hitimisho: CCM Lazima Iamke au Isambaratike

Nitasema kama Mwalimu: CCM inatakiwa kurejea kwenye misingi yake. Ikiwa wanachama wake hawataamka na kudai chama chao kirejee kwenye misingi ya ujamaa, basi chama kitakuwa hakina maana tena.

CCM siyo vibanda vya biashara vya wachache. CCM siyo jukwaa la matajiri wachache kujilimbikizia mali. CCM ni chama cha wananchi! Lakini kama hakiwezi tena kuwalinda wakulima na wafanyakazi, basi CCM itakuwa historia tu, kama majina ya vyama vilivyopotea duniani.

Wanachama wa CCM, amka sasa! Chagua viongozi waadilifu. Wawajibishe wale wanaouza nchi. Rudisheni chama kwenye misingi yake. Laiti ninyi mngekuwa walinzi wa rasilimali zenu, taifa hili lingekuwa mahali pa neema kwa wote.

Julius Kambarage Nyerere, akisema kwa sauti ya uzalendo kutoka moyoni!

🇹🇿Asante kwa kuwa sehemu ya safari hii ya tafakari na maarifa! Falsafa ni mwanga wa akili na dira ya maisha--Usiruhusu giza la kutokujua likuzuie kuona upeo mpana wa fikra. Endelea kufuatilia ukurasa huu, kwani kila wazo jipya ni hatua kuelekea hekima. Tafakari, hoji na usiache kufikiri.🇰🇪
 
Mnafiki tu huyu, mbona kipindi CAG anazuiliwa kuwakagua TGFA na SGR huyu Mpina hakuinua mdomo?
Mbona hukuja kutuambia kwamba Mpina kakaa kimya wakàti huo? Leo anaongea weee unahoji hayo ambayo hayajui? Ulimpa hii taarifa ya cag kuzuiliwa akakaa kimya?
 
Mbona hukuja kutuambia kwamba Mpina kakaa kimya wakàti huo? Leo anaongea weee unahoji hayo ambayo hayajui? Ulimpa hii taarifa ya cag kuzuiliwa akakaa kimya?
Naandikaje wakati nilijua ndio msimamo wa chama, nakumbuka hadi bunge likaazimia CAG akaguliwe pia bajeti ya CAG ikashushwa kutoka 80B mpaka 40B. Yaani serikali ya waadilifu inaogopa ukaguzi?

Fast forward leo eti Mpina ana rely kwenye CAG report kuibamiza serikali? Mambo ya unafiki sana.
 
Back
Top Bottom