Lukuvi kutumika kama alivyotumika Musukuma?

Lukuvi kutumika kama alivyotumika Musukuma?

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Hili ni swali. Naungana na bwana Pascal Mayala kuwa swaki siyo statement.

Ukitaka kummaliza adui yako ni vizuri umpate kibaraka wa kupandikiza kwa adui yako.

Unasikia huko Ukraine, makamanda kadhaa wa kirusi wa ngazi za juu walivyouawa kwa makombora ya Ukraine. Hatujawahi kusikia makamanda wakubwa wa Ukraine wakitunguliwa kwa makombora. Swali la kujiuliza, hao wapigaji wa makombora wa Ukraine wanajuaje kwamba leo kuna kamanda mkubwa wa majeshi ya Ukraine anatembelea komandi fulani? Jibu ni rahisi. Ni lazima Ukraine imepenyeza watu wake ndani ya jeshi la Russia.

DP walipojua kuwa mkataba wao ja Tanzania ni mbaya, na hakuna mwenye akili anaweza kuukubali, ilitumia mbinu ya kuwapenyeza watu wake ndani ya vyombo vya maamuzi vya Tanzania na vyombo vya habari. Ndiyo maana watanzania wakilalamika dhidi ya maamuzi hayo ya hovyo, tayari kuna watu wa mwarabu waliopandikizwa kwenye jamii yetu, watapiga kelele kutetea na kutoa sifa juu ya DP, sifa ambazo hata DP wenyewe wanazisikia kwa mara ya kwanza.

Ni ukweli kuwa kelele za hao makywadi wa mwarabu hazijaweza kubadili msimamo wa watanzania wengi wenye akili, uelewa na mapenzi mema kwa nchi yao.

Huko nyuma, licha ya bwana Lukuvi kuhangaika sana akizunguka nchi nzima kutatua migogoro ya ardhi, kwa mshangao wa wengi, aliwekwa pembeni, na wananchi bila shaka waludanganywa kuwa eti amepewa nafasi maalum ya ushauri.

Hivi majuzi, katikati ya kashfa ya kuigawa bandari yetu kwa mwarabu, tunaambiwa kuwa eti Lukuvi ameteuliwa kuwa mshauri. Mara ya kwanza tuliambiwa ameondolewa kwenye uwaziri na kupewa nafasi ya ushauri. Kama alikwishapewa nafasi ya ushauri wakati anaondolewa kwenye uwaziri, imekuwaje tena na safari hii apewe nafasi ya kuwa mshauri wakati tayari alikwishakuwa mshauri? Au dhamira ni kumfanya kuwa mpini wa MTi kwenye shoka ili ukakate MITI?

Maswali ni mengi, muda ni kidogo.
 
Watanzania wengi tumeupinga huu mkataba haijalishi mafisadi yamenunua wanasiasa na vyombo vikuu vya habari.
 
Huko Ukraine Wagner na Jeshi la Urusi wanahujumiana.
Kingine ni Aerial Recon, CIA
HIMARS katika ubora wake. Wagner na RAF hawajawahi kuwa maadui. I repeat: Wagner PMC are not in conflict with Russian armed forces.

You may choose to believe whatever else you want. That's your freedom.
 
Binafsi siuoni huo uadui wa Lukuvi na Samia kama kweli upo, na hata kama upo, sioni nguvu yake kumtisha Samia kwa sasa.

Hili jambo lingekuwa na uzito wakati ule Samia anahangaika kutengeneza timu yake ya ushindi, alipokuwa anamtoa anawatoa wizarani na kuwaaogeza ikulu.

Kwa mtazamo wangu naona mpaka kufikia pale alifanikiwa kumaliza ule mchezo, lakini kwake ghafla kuonekana kumkumbuka tena Lukuvi wakati huu wa sakata la bandari, ni wazi Samia ameona hali yake kwa wabara sio nzuri.

Haaminiki tena, anaonekana dalali wa mali zetu, ametusaliti, sasa anachofanya ni kujaribu kuwasogeza karibu kimawazo wale aliowaona mwanzo ni maadui wake kisiasa, ghafla wamegeuka marafiki, ndio anataka kusikiliza ushauri wao, ili arudishe imani yake iliyopotea kwa wabara.
 
Ifike mahali shuleni watoto wajifunze ushupavu na misimamo wakiwa watu wazima wasiwe mburula yaani saa nyingine mtu mzima ujue kusema "nashukuru LAKINI hapana".
Mtu umetangazwa hadharani kuwa unatamaa na cheo chamtu alafu kesho anakuchoresha eti 'kuwa mshauri wangu' mtu njaa njaa lazima akubali!!!
 
Kwa ccm hii kuna litakalo badilika? Sanasana tutasikia uvccm, uwt, na ccm kwa ujumla wakiandamana kumpongeza Rais kwa uwekezaji mzuri.
 
Mamburura yanaruka na kukanyagana.....in nature's voice.
 
Ifike mahali shuleni watoto wajifunze ushupavu na misimamo wakiwa watu wazima wasiwe mburula yaani saa nyingine mtu mzima ujue kusema "nashukuru LAKINI hapana".
Mtu umetangazwa hadharani kuwa unatamaa na cheo chamtu alafu kesho anakuchoresha eti 'kuwa mshauri wangu' mtu njaa njaa lazima akubali!!!
Hii ndio sample ya Watanzania.
 

Attachments

  • Screenshot_20230605-192423.jpg
    Screenshot_20230605-192423.jpg
    23.4 KB · Views: 3
Ukiwa mwanasiasa mwenye ushawishi halafu ukawa muoga basi utatumika kama toilet paper. Ndicho kinachompata Lukuvi.

Lukuvi alipaswa jasiri wa kukataa kutumika kama karai tangu siku ananondolewa uwaziri.
Lukuvi ana ushawishi kwa watu gani? Na akina nani? Huyo punga kwanza ni mdini balaa labda wewe umetoka nae kijiji kimoja uko kwenu isimani
 
Hili ni swali. Naungana na bwana Pascal Mayala kuwa swaki siyo statement.

Ukitaka kummaliza adui yako ni vizuri umpate kibaraka wa kupandikiza kwa adui yako.

Unasikia huko Ukraine, makamanda kadhaa wa kirusi wa ngazi za juu walivyouawa kwa makombora ya Ukraine. Hatujawahi kusikia makamanda wakubwa wa Ukraine wakitunguliwa kwa makombora. Swali la kujiuliza, hao wapigaji wa makombora wa Ukraine wanajuaje kwamba leo kuna kamanda mkubwa wa majeshi ya Ukraine anatembelea komandi fulani? Jibu ni rahisi. Ni lazima Ukraine imepenyeza watu wake ndani ya jeshi la Russia.

DP walipojua kuwa mkataba wao ja Tanzania ni mbaya, na hakuna mwenye akili anaweza kuukubali, ilitumia mbinu ya kuwapenyeza watu wake ndani ya vyombo vya maamuzi vya Tanzania na vyombo vya habari. Ndiyo maana watanzania wakilalamika dhidi ya maamuzi hayo ya hovyo, tayari kuna watu wa mwarabu waliopandikizwa kwenye jamii yetu, watapiga kelele kutetea na kutoa sifa juu ya DP, sifa ambazo hata DP wenyewe wanazisikia kwa mara ya kwanza.

Ni ukweli kuwa kelele za hao makywadi wa mwarabu hazijaweza kubadili msimamo wa watanzania wengi wenye akili, uelewa na mapenzi mema kwa nchi yao.

Huko nyuma, licha ya bwana Lukuvi kuhangaika sana akizunguka nchi nzima kutatua migogoro ya ardhi, kwa mshangao wa wengi, aliwekwa pembeni, na wananchi bila shaka waludanganywa kuwa eti amepewa nafasi maalum ya ushauri.

Hivi majuzi, katikati ya kashfa ya kuigawa bandari yetu kwa mwarabu, tunaambiwa kuwa eti Lukuvi ameteuliwa kuwa mshauri. Mara ya kwanza tuliambiwa ameondolewa kwenye uwaziri na kupewa nafasi ya ushauri. Kama alikwishapewa nafasi ya ushauri wakati anaondolewa kwenye uwaziri, imekuwaje tena na safari hii apewe nafasi ya kuwa mshauri wakati tayari alikwishakuwa mshauri? Au dhamira ni kumfanya kuwa mpini wa MTi kwenye shoka ili ukakate MITI?

Maswali ni mengi, muda ni kidogo.
Lukuvi akiamua kwa akili zake anaweza kuwa amechagua kuwa dodoki ngoja tusubiri tuone mtu anayeteuliwa nafasi ya kushauri mara mbilimbili.ngoja tusubiri msimamo wake.
 
Back
Top Bottom