Lulandala acha kumchamba Mbowe. Siasa za mipasho ya kitaarabu hazifai.

Lulandala acha kumchamba Mbowe. Siasa za mipasho ya kitaarabu hazifai.

Idugunde

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2020
Posts
6,404
Reaction score
6,969
Fakii Lulandala, Katibu Mkuu Uvccm amesema kuwa "CCM ni chama kikubwa chenye watu wengi wenye sifa na uwezo na karama za uongozi, hakina historia ya kuruhusu ung'ang'anizi kwenye nafasi za uongozi kama kule kwa kwa jirani ,nakishukuru sana Chama changu (CCM) kuona kwamba kwa muda huu ninafaa kukitumikia kwenye nafasi hii kwa muda ambao itakipendeza, baada ya kuteuliwa nimesoma mitandaoni kuna wengine wanasema mimi ni mzanzibari, hata ningekuwa mzanzibari nisingejisikia vibaya lakini mimi nimezaliwa Ilembula wilayani Wanging'ombe Mkoa wa Njombe ndio ninapotoka"



20231005_135143.jpg
 
actually kuna kana kaukweli kanachungulia apo,
ukiachana na mbowe, Ibrahimu Haruna Lipumba, John Momose Cheyo, Hashimu Rungwe Spunda na wengine wote katika vyama 22 vya sisa vyenye usajili wa kudumu na vingozi hawa wamedumu katika uongozi tangu kuanzishwa kwa vyama vyao na kama si hivyo basi ni viongozi waliong"ang"ana kwa muda mrefu mno uongozini kwenye vyama vyao na hili ni janga sugu ndani ya vyama.

Tz Ikitokea mwenyekiti muanzilisha kang"olewa then chama kinapotea kwenye medani, kinapasuka na kusambaratika au kina kufa kabisa. Hiki kikubwa cha ccm unaweza kusema ni afadhali...

Na kuna viongozi wajanja wameanzisha nafasi kwenye vyama vyao, mathalani nafasi ya kiongozi wa chama na mwenyekiti wa chama,
ili hatima akingatuka huku anaweza kwenda kwenye nafasi hiyo nyingine ndani ya chama hicho hicho.
 
Atakuwa ameishiwa moyoni na akilini. Hawa ndio wanafiki wanaoifaa CCM. Alipokuwa CHADEMA, aliponda kila kitu cha CCM. Leo yupo CCM, atasifia upuuzi na ushenzi wote wa CCM. Akinyimwa uongozi huko CCM, ataitusi CCM kwa kila inachokifanya. Hii ndiyo tabia ya wanasiasa tumbo au wanasiasa malaya aliowatamka mwalimu Nyerere, wanasiasa wanaonunulika, wanauza utu wao na kubakia kama fisi kushangilia chakula, hata kama ni mzoga.
 
Back
Top Bottom