Lulu sasa abadilishiwa mashtaka

Lulu sasa abadilishiwa mashtaka

Ndiyo maana kuna baadhi ya wapinzani wanasema majaji wengi wa Kikwete ni vilaza. Utamfunguliaje mtu mashitaka kama hakuna ushahidi tosha? Bongo hii, tunaishi basi tu.

hilo sio kosa la majudge ni uzembe wa upande wa mashtaka na ukumbuke hii case ina public interest..kwa hiyo upande wa mashtaka unajua unachofanya
 
Maskini, ujana wake unapotea tu huko ndani. So unfortunate!

Kwa kweli ni kama Watanzania wengi achilia mbali wapenda sanaa,wako upande wake wakimuombea kunusurika na janga lililomkuta,na kuwa akitoka abadili mienendo yake.
 
Kwa nchi za wenzetu nadhani angeachiwa huru kabisa , maana wenzetu huwa hawana muda wa kuendesha kesi za kusadikika zisizo na ushahidi kama hii ya Lulu ambayo mwisho wa kesi hii hukumu yake itakuwa Lulu kuachiwa huru.

Sasa hivi na swala la muda kujuwa Lulu ni lini ataachiwa na Mahakama Kuu, kwa mfumo wa Tanzania kuuwa bila kukusudia wala siyo kesi ndio maana Ditopile walimsevu kumpa hii hili baadaye ashinde wakati ukweli ni kwamba Ditopile aliuwa kwa kukusudia.



Walichokua wanafanya ni ku buy time ili wananchi wasahau sahau,maana wananchi walikua wanahasira kali kweli na lulu,wangemmaliza mtaani.

Wamekimbiza kimbiza kakesi kidogo ili wananchi waone kua anashurutishwa, its just a matter of time before u see her soon on the streets. TANZANIA OYEEEEE!!
 
Japo namuonea huruma, lakini mnakumbuka wanajeshi watatu waliohukumiwa kifo kwa kuhisiwa wamemuua mtoto wa Fundikira kama mwezi umepita sasa? Walikuwa ni watu wa mwisho kuwa na marehemu na hakukuwa na evidence concrete zaidi ya hiyo. Mimi sio mwanasheria, lakini tunayaona sana hayo.

Pengine kwa wale motive ilikuwepo,ila kwa huyu binti, motive haikuwepo kabisa!
 
Nimefurahi kesi hii imekuwa ikiendeshwa kwa kasi ya ajabu sana sijui ni kwa maslahi ya nani ukilinganisha na kesi nyingi za mauaji, Sinashaka ripoti ya madaktari imeshamuepusha na mkono wa jela...tunajua mahakama haipendi maongeleo ya mambo ambayo hayajaamuliwa ila kwa hili liko dhahiri, ni sinema kidogo ili watu waonekane wapo siriasi mwisho wa siku yale yale...
 
Ndiyo maana kuna baadhi ya wapinzani wanasema majaji wengi wa Kikwete ni vilaza. Utamfunguliaje mtu mashitaka kama hakuna ushahidi tosha? Bongo hii, tunaishi basi tu.
Mkuu hapo ni tatizo la majaji au waendesha mashitaka?
 
hajaepuka adhabu ya kunyongwa, hajawahi kuwa convicted.

Magazeti yetu yanatuandikia madudu.


Usishangae mkuu, ni hilo hilo mwananchi ndiyo lilikurupuka na habari za Tyson kubadili jinsia. Full makanjanja!!
 
Walichokua wanafanya ni ku buy time ili wananchi wasahau sahau,maana wananchi walikua wanahasira kali kweli na lulu,wangemmaliza mtaani.

Wamekimbiza kimbiza kakesi kidogo ili wananchi waone kua anashurutishwa, its just a matter of time before u see her soon on the streets. TANZANIA OYEEEEE!!

Ulivyoandika ni kama vile unamuona ana hatia. Kwa lipi? Inaitwa motive.. Arithi mali,au analipiza kisasi fulani,au kwa lipi?
Huenda ye mwenyewe anafeel msiba wa mpenzi wake.
Kifupi hakukuwa na MOTIVE!
 
Hatimaye Mkurugenzi wa Mashtaka nchini,Eliezer Feleshi Mbuki (sasa naye Wakili),amembadilishia shtaka Msanii Elizabeth Michael almaarufu kama Lulu kutoka kuua kwa kukusudia hadi kuua bila ya kukusudia. Lulu anashtakiwa kwa kumuua Msanii mwenzakwe Marehemu Srtephen Kanumba.

Jambo kama hilo lilifanywa pia katika kesi ya Marehemu Kapteni Mkiwaona Ditopile Mzuzuri aliyekuwa akishtakiwa kwa kumuua dereva wa daladala kwa kumpiga risasi.

Hii ndio kusema,sasa mlango wa dhamana kwa Lulu uko wazi kwakuwa kosa analoshtakiwa kwalo si kati ya yale yasiyo na dhamana. Sinema hii ndio inaelekea patamu
 
Nimefurahi kesi hii imekuwa ikiendeshwa kwa kasi ya ajabu sana sijui ni kwa maslahi ya nani ukilinganisha na kesi nyingi za mauaji, Sinashaka ripoti ya madaktari imeshamuepusha na mkono wa jela...tunajua mahakama haipendi maongeleo ya mambo ambayo hayajaamuliwa ila kwa hili liko dhahiri, ni sinema kidogo ili watu waonekane wapo siriasi mwisho wa siku yale yale...

Mimi nikielezwa motive ya muuaji,labda nitakuwa convinced.
 
Na mimi niungane na watanzania wenzangu kukupa pole elizabeth michael/lulu..kuna wakati natizama the whole saga that erode you, then nahis imy be I m watching a certain horror film but narealize ni kweli basi naingiwa imani lakini ukweli anaujua Mungu, kama ulimkosea ni vyema una nafasi ya kumwomba msamaha..na wakati huu hasa unaposoma hili bandiko, tambua kuwa segerea sio kutengwa na dunia hii bali upo nasi sema kwa kipindi kufupi upo na jamii nyingine! Kesi yako ni rahisi sana..in political context hapo ulipo ni sahihi hasa ukizingatia hamaki ya wananchi wenye hasira,sasa hasira zao zimepungua na wanakuonea huruma! Mda sii mrefu utakua mtu huru
 
Kwanini Mkuu?
Nakiri kutofatilia shauri hili, ila nafikiri ni mapema sana DPP kufanya hivyo, japo kuwa sheria inamruhusu na kumpa mamlaka hayo, still iko kwenye committal proceedings... Anyways, labda ushahidi umekamilika na hautoshi kumtia hatiani...ila naona ni mapema sana!! Na kuna mashauri mengi tu ya vifo vya utata, ila hayatolewi nolle mapema hivi...
 
Nakiri kutofatilia shauri hili, ila nafikiri ni mapema sana DPP kufanya hivyo, japo kuwa sheria inamruhusu na kumpa mamlaka hayo, still iko kwenye committal proceedings... Anyways, labda ushahidi umekamilika na hautoshi kumtia hatiani...ila naona ni mapema sana!! Na kuna mashauri mengi tu ya vifo vya utata, ila hayatolewi nolle mapema hivi...
Ukweli mtupu Counsel
 
Back
Top Bottom