Lulu sasa abadilishiwa mashtaka

Dah! Afadhali aisee! Wamemchelewesha ili ajifunze!
Muacheni mtoto wa watu arudi uraiani!
 
Vichwa vya magazeti habari kubwa ya leo ni kwa msanii wa filamu nchini Lulu kubadilishiwa mashtaka kutoka kuua kwa kukusudia hadi kuua bila kukusudia.

Wanajamii, DPP kwa kufanya hivo tayari ameishatoa hukumu kwa mtuhumiwa. Hili suala lipo beyond judicial descretion power. Mahakama ndiyo yenye power ya kutafiti km mtuhumiwa aliua kwa kukusudia ama la.

Tunavyopeleka mashtaka mahakamani ya mauaji huwa hakuna shitaka la kuua bila kukusudia "manslaughter". Je ikitokea ushahidi ukapatikana mahakamani kwamba Lulu aliua kwa kukusudia! Sina haja hapa ya kumkandamiza Lulu ila napinga ukiukaji wa sheria alioufanya DPP. Huu ni ukiukwaji wa utawala wa sheria.

Ni ukiukwaji pia pale watendaji wa serikali wanapoingilia mamlaka za mahakama.
 
Nahisi kunatatizo kubwa katika ofisi ya DDP lakini kuna tatizo kubwa sana la maadali ya watendaji wakuu wa serikali na vyombo vyake. Siamini kama makosa haya yanatokea kwa bahati mbaya kwakuwa yanajirudia rudia sana bila ya wakubwa wao kuingilia kati. Hii haitofautiani na lile la mkuu wa kaya na uteuzi wa majaji. Tulimsikia werema alivyojibu
Chamoto tutakiona watanzania
 
Mimi sioni kama kuna ukiukwaji wa sheria uliofanywa na Mkurugenzi wa Mashtaka, mshtakiwa hufunguliwa shtaka kulingana na ushahidi uliopo, kama DPP hana ushahidi unaoweza kuthibitisha kwamba Lulu ameua kwa makusudi na aliua bila ya kukusudia kuna haja gani ya kuendelea kumshtaki Lulu kwa mauaji ya kukusudia. Ukiangalia jinsi tukio lenyewe lilivyotokea ni wazi kwamba kuna ugumu kwa DPP kuweza kuthibitisha mauaji ya kukusudia. Ni mamlaka yake na nakubaliana nae kwa kitendo hichi cha kubadilisha shtaka. Hakuna mamlaka yoyote ya Mahkama yaliyoingiliwa hapo.
 

kwa hiyo ameweza kuthibitisha(beyond reasonable doubts) kuwa mauaji hayakuwa ya kukusudia!! tunapoandika tusome na kukielewa tulichokiandika kabla ya kupost.
 
Lakini kama ameuwa kwa kukusudia na ushahidi/vielelezo vikawasilishwa mahakamani. Bado Mahakama inaweza kumuhukumu kwa usahihi ama aliuwa kwa kukusudia ama bila kukusudia. Katika maswala tata kama haya ni bora tukaviachia vyombo husika vikayashughulikia kwa uhuru na taratibu zao. Kinachotakiwa ni uadilifu wa watendaji husika katika nyanja zote zinazoshughulikia jambo hili.
 
yametimia, muda c mrefu ataachiwa ,bongo bana naskia kuna mjombaa anamkata kulekule pa gereza
 
akitoka apewe scenes za lupango ataigiza vizuri sana.
 

mkuu, hakuna shitaka la kuua bila kukusudia! Ila mahakama baada ya kupelekewa kesi ya mauaji. Hupunguza kosa 'mudder' kuwa 'manslaughter'. Huwezi kupeleka 'manslaughter' km kosa mahakamani. Sijawahi ona zaidi ya kesi ya uncle Dito na hii hapa.
 
mkuu unajua nguvu ya forensic pathology kwenye mambo kama haya?ile postmortem ilifanyika kabla ya lulu kushtakiwa iweje katikati ubadilishe hati ya mashtaka?
 
katika watu ambao wana power kubwa ktk nchi zetu za dunia ya tatu basi ni DPP, its unbelievable yeye anaweza kuamua kumshtaki au kutomshtaki mtu yoyote alafu funny enough hakuna wa kumuuliza!!!!

Rais wa Tanzania unamuacha wapi?!
Huyu anaweza kumwachia huru mtu aliyetiwa hatiani na mahakama,na hata kumtoa gerezani mfungwa kwa wakati wowote bila kuhojiwa na chombo chochoteg
 
Akitoka ntatamani nimuone. Atakavyokuwa mpole. Ataheshimu kila mtu.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Umenena ukweli mtupu, yale maringo na kujisikia lazima vitakuwa vimekwisha atajifunza kuthamini na kujali yeyote......jela ni mafunzo
 
Tatizo la nchi zetu kwenye kesi za jinai wanashtaki kwanza na baadae ndio wanafanya upelelezi. Kuthibitisha kosa la mauaji ya kukusudia inahitaji ushahidi tofauti na ule wa kesi ya kuua bila ya kukusudia. Sasa kama hakuna ushahidi wa kuthibitisha murder ilikuwa ni bora kesi iachwe hivyo na mwisho wa siku mshtakiwa aachiwe huru au ni bora kumshatki na kosa stahili angalau anaeshkaki akiwa anajua nini anafanya. Mwenye mamlaka ya kushtaki ni DPP na kwenye kesi hii ambayo kupitia vyombo vya habari vilivyotujuvya kwa muhtasari tu juu ya tukio lenyewe lilivyotokea ni vigumu sana kuthibitisha mauaji ya kukusudia.
 
Kikao kijacho cha mahakama lazima nikutoe kwa dhamana. Mapumziko yetu China. Nikupe pole kwa kutenganishwa na sisi kwa siku zote hizo. Mzee wako tutapita kumsalimia. Hii itakusaidia kuwaepuka paparazi wa bongo kwa muda mpaka wazoee kuwa kwako nje ya gereaza. Pole honey kwa yooote. Maisha ni hatua.
 
Hivi kwa mfano mtu amemfumania mkewe akiliwa uroda na njemba nyingine halafu akaiua hiyo njemba inakuwa kuua bila kukusudia au kukusidia?
 
Nakumbuka siku moja tukiwa mahali tumekaa na Jaji mmoja mbaye ni miongoni mwa Majaji wapya wa JK, alikuwa anampigia simu sana Dr. Twalib ili apate kumweleza ni vitu gani ambavyo vinahitajika ili kuweza kumfanya Lulu apate dhamana? At the same time alikuwa alimpatia maagizo mama Lulu ya nini afanye. Hapo ndipo nilipoona kwamba huku kwetu, Sheria ni kiini macho tu. Inasikitisha lakini ni kitu ya kweli nimeishuhudia mwenyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…